Tatizo hili halipo hapa nchini lakini wapo walionitupia swali na sasa inabidi nikiri kuwa lipo sana Marekani na mpasuaji wa masuala ya urembo wa Miami Dk Constantino Mendieta amethibitisha.
Mtaalam huyu amezungumzia sana utunzaji wa makalio daraja la kwanza ndiyo yanayotakwa sana. Ni kama vile umeuchukua moyo halafu ukaugeuza chini juu,haya ndio dizaini ambayo Marekani wanalilia sana.
Watu wa huko wanajimwaga katika majumba ya upasuaji kupata shepu hiyo adimu, na anayewachengua sana.
Kama unataka kuwa na shepu bomba fuata hatua zifuatazo:
1. Fanya masaji na losheni zinazoimarisha na kutengeneza ngozi nyororo katika mapaja yako,ukianzia chini ya makalio mara mbili kwa siku.