Jukumu kubwa hapa ni kutambua aina tatu za vifaa ambavyo vinafanya kazi hio navyo ni ,
Mawazo au fikra.
Maneno.
Matendo.
Tumefungwa kwenye vitu hivyo, kitu tunachokifikiria, maneno tunayoongea, na kitu unachokifanya. Kwa mfano,
Mtu anasema kuwa Mungu nipe chakula cha leo, si ndio kitu unachowaza na kukitaka? Mungu jibu lake ni ndio umepata, Nahitaji pesa nyingi, ukweli hata mimi nahitaji pesa nyingi, lakini jibu lake ni hilo hilo ni kweli unahitaji pesa na umekuwa ukisema mara nyingi, Ugonjwa huu utaniua, ni kweli kabisa huo utakuua, Ndoa yangu mbaya, ni kweli ni mbaya, ndio ni mbaya, kazi hii siipendi,nimechoka na maisha haya, ndio umechoka na maisha hayo, ni kweli kabisa.