Makapuku Forum

Makapuku Forum

Inawezekana hujawahi kutambua kabisa kuwa kila kitu kipo kwa ajili yako.Yaani Afya, furaha, amani, upendo, pesa, heshima ,hekima na mengine katika maisha .
Mungu anasema kila kitu unachotaka,unachohitaji tayari unacho hata kabla hujaomba nimekupa vyote, lakini hujaelewa jinsi system inavyofanya kazi na huna uzoefu na hilo.
Hapa hata mimi palikuwa pananichanganya sana, hongera wewe ambaye ulikuwa tayari umegundua hili. Kwa sababu anasema kila kitu kinachotokea sasa kilikuwepo tayari ila ni wewe tu hujui na hukuona kuwa vipo.
 
Jukumu kubwa hapa ni kutambua aina tatu za vifaa ambavyo vinafanya kazi hio navyo ni ,

Mawazo au fikra.
Maneno.
Matendo.
Tumefungwa kwenye vitu hivyo, kitu tunachokifikiria, maneno tunayoongea, na kitu unachokifanya. Kwa mfano,
Mtu anasema kuwa Mungu nipe chakula cha leo, si ndio kitu unachowaza na kukitaka? Mungu jibu lake ni ndio umepata, Nahitaji pesa nyingi, ukweli hata mimi nahitaji pesa nyingi, lakini jibu lake ni hilo hilo ni kweli unahitaji pesa na umekuwa ukisema mara nyingi, Ugonjwa huu utaniua, ni kweli kabisa huo utakuua, Ndoa yangu mbaya, ni kweli ni mbaya, ndio ni mbaya, kazi hii siipendi,nimechoka na maisha haya, ndio umechoka na maisha hayo, ni kweli kabisa.
 
Majibu ya Mungu siku zote ni Ndio, hata kama ni kitu kizuri au kitu kibaya, Positive au Negative yeye ni ndio. Maana yeye ni wa kila kitu , wa kila mtu.
Kitu cha muhimu cha kuzingatia hapa ni katika Msingi wako wa mawazo.Najua si kitu rahisi kwa mtu ambae hana msingi mzuri wa mawazo yake, lakini nguvu huvuta kila kitu, ukiwa na nia ya kubadilika utaanza pale ulipo kuweka msingi ulio imara kwa sababu ni msingi wa kila kitu hapo.
Usihukumu kwa mwonekano.
 
MGONGO ni moja ya kiungo cha mwili ambacho kinahitaji uangalizi mzuri.Bila hivyo huleta tabu hasa pale mgongo unapokuwa hauko katika muonekano mzuri.

Uchafu unaoganda kwenye mgongo hupelekea muwasho wa mara kwa mara na mgongo kuwa na mabaka mabaka .
 
Ukweli ni kuwa jaribu kuangalia mgongo wako na kuona kama unastahili kuwa hivyo na kama haustahili basi chukua hatua kwa kuhakikisha mgongo unakuwa msafi na kutafuta tiba ya chunusi au mabakamabaka yaliyo mgongoni mwako.


Unapoufanyia tiba mgongo kwa kutumia sabuni za dawa au lotion utaufanya uwe na muonekano mzuri na hata kuwa huru kuvaa nguo yoyote
 
Wengi wanashindwa kuvaa nguo za wazi kutokana na muonekano wa ngozi zao za mgongoni kuwa mbaya zenye vipele, chunusi na kupauka.Madoa kwenye mgongo yamekuwa yakikosesha wengi raha kutokana na suala la utunzaji mgongo halitiliwi maanani kama ilivyo kwenye utunzaji wa uso au miguu.


Tumia brashi laini lenye sababu ya kutosha katika kusugua mgongo wako. Kisha paka mafuta.
 
Kama huwezi kufikia vizuri mgongo kwa kutumia blashi basi unaweza kuomba msaada ili mradi mgongo utakate na kuwa katika sura ya kupendeza.


Wengi wanashindwa kuvaa nguo za wazi kutokana na migongo yao kuwa na sura isiyopendeza
 
Ni muhimu ukazingatia usafi wa mgongo ili uwe huru kuvaa nguo za wazi bila kuwa na mashaka kuwa kuna watu wanautazama vibaya mgongo wako na wengine wameanza kucheka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom