Makapuku Forum

Makapuku Forum

TUOMBE:Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Bwana Mungu wa Majeshi asante kutuamsha salama Jumapili ya leo tarehe 14 OKTOBA 2018..Si kwa wema wetu Baba ni kwa Upendo na Neema kuu..wako watu wengi walitamani kuiona leo hawajaweza..tunakuja mbele zako kwa shukurani kuu.Jumapili ya leo tunaomba tusamehe Baba turehemu twakusihi...tupe moyo safi Mfalme wa Amani.Bariki kuingia na kutoka kwetu Bariki Sadaka zetu na tusaidie tusamehe wengine.
Bariki watumishi wa Mungu watulishe neno kadri ulivyowaandaa .Asante Baba kwa kuwa utakuwa nasi katika Ibada zote.Endelea kutukumbatia Baba na kutufariji kwa misiba yote,Endelea kutuponya magonjwa yote na imarisha afya za mwili na roho zetu endelea kuwapa tumaini wajane,wagane yatima na wote wanaopitia changamoto mbalimbali..asante kwa ajili ya ndugu zetu jamaa zetu marafiki zetu ambao ni zawadi kuu katika maisha yetu wanatupa furaha na Amani na kutukumbatia katika mapito yetu wapiganie katika kazi,biashara,maisha ,familia,afya na wape kibali katika hatua zote za maisha.Roho Mtakatifu kaa nasi katika kila jambo.Tunaomba katika jina la Yesu Kristo Amen

JUMAPILI NJEMA NA IBADA NJEMA YA KIBALI DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ITUFUNIKE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom