Makapuku Forum

Makapuku Forum

Everton inatafakari uhamisho wa aliyekuwa kiungo cha kati wa Arsenal na Manchester City Samir Nasri, mwenye umri wa miaka 31. Marufuku ya kutumia dawa za kutitimuwa misuli iliyomkabili mchezaji huyo raia wa Ufaransa inakamilika mwezi ujao. (Daily Mail)
 
Manchester United inataka kufanya mazungumzo mapya ya mkataba na Juan Mata mwezi huu. Mkataba wa mchezaji huyo wa miaka 30 wa kiungo cha kati raia wa Uhispania unamalizika msimu huu wa joto. (Sun)
 
Tottenham inatumai kumsajili mlinzi wa Manchester United na Ivory Coast Eric Bailly, mwenye miaka 24, mwezi Januari. (Daily Express)
 
Tottenham pia ina hamu ya kumsajili kiungo cha mbele wa Beijing Guoan - Cedric Bakambu. Guoan iliilipa Villarreal zaidi ya £ milioni 35 kwa mchezaji huyo wa miaka 27 kutoka Jamhuri a Kidemokrasi ya Congo mnamo Februari. (L'Est Republican, kupitiaTalksport)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom