
TUOMBE:Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Bwana Mungu wa Majeshi Asante kutuamsha salama leo ALHAMIS Tarehe 11 oktoba 2018..Asante kwa pumzi hii Baba tunakuomba endelea kutulinda na kutusaidia tukutumikie Mfalme wa Amani maana wapo wengi walitamani kuiona siku ya leo wakiwa na mipango mingi na mizuri hawajaweza.Tunaomba Toba kwa yote tuliyoenda kinyume na Mapenzi yako kwa Mawazo Maneno na Matendo Uturehemu Eee Baba .Tunaomba Roho Mtakatifu Kaa nasi tufundishe kuwa wanafunzi wema tupiganie tuwe na mioyo safi ili siku ya mwisho tuingie Mbinguni.Asante kwa uponyaji wa wagonjwa Baba ..Endelea kutuimarisha miili na Roho zetu tuwe salama.Asante kwa Ufariji kwa wafiwa Baba endelea kuwa faraja kuu kwa wajane,wagane na yatima tupe tumaini lidumulo.Asante kwa Umoja,Upendo na Ushirikiano katika Mahusiano, familia na makundi mbalimbali Endelea kutupa moyo wa kuvumuliana na kumuona kila mmoja ni muhimu katika maisha haya.Bariki kazi za mikono yetu.Tunawafunika kwa damu Takatifu watoto na wajukuu wetu waendelee kuwa salama miili na Roho.Epusha wimbi la wizi wa watoto Baba Tunazifunga Roho zote za giza zinazoshiriki wizi huu ,zishindwe katika jina la Yesu Kristo na watoto wote waliopotea wawe salama na warudi kwao salama.
Baba Asante kwa Neema na Baraka zote unatugusa kwa namna ambayo hailezeki Asante kwa Upendo wa hali ya juu ambayo hauelezeki. Tunakushukuru kwa ajili ya Imani tuliyonayo kwako inatupa Amani na hakika Baba hatuna tunayemtegemea zaidi yako Yehova.Tunakabidhi kazi zetu,ratiba zetu ,mawazo yetu na kila tutakapo kuwa leo uwepo.Tunaomba kibali katika kika tufanyalo.
Tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo Amen
ALHAMIS NJEMA NA SHUKURANI KWA MUNGU KWA YOTE ANAYOTUTENDEA DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ITUFUNIKE

