Makapuku Forum

Makapuku Forum

Agenti wa Zinedine Zidane, 46, kocha wa zamani wa Real Madrid ambaye amehusishwa na Manchester United, amesemahuenda asiiongoze klabu hiyo inayocheza katika ligi kuu ya England. (Marca)
 
Paul Pogba aliisaidia Man Utd kupata ushindi wa kusisimua wa mabao 3-2 wa dhidi ya Newcastle baada ya Jose Mourinho kumshauri kuhusu mbinu za mchezo huo wakati wa muda wa mapumziko. (Sun)
 
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal anapigiwa upato kuwa meneja wa Aston Villa huku John Terry, 37, akitarajiwa kuwa msaidizi wake. (Express na Star)
 
Arsenal huenda ikamsajili mshambuliaji wa Paraguay Miguel Almiron mwezi Januari mwakani. Mchezaji huyo wa miaka 24 amefunga mabao 12 mwaka huu kwa akiwa na MLS Atlanta United.
 
West Brom itarejea na ofa nyingine kwa Bradley Dack wa Blackburn mwezi Januari msimu wa uhamisho wa wachezaji baada ya juhudi zao za kumchukua kugonga mwamba kiungo huyo wa kati wa miaka 24 msimu wa joto. (Birmingham Mail)
 
Mshambuliaji Manolo Gabbiadini amekiri kuwa angelitafakari ofa alizopata msimu wa jota laiti angelijua ataendelea kusalia Southampton. Mchezaji huyo alianza kucheza katika ligi ya Premia msimu huu siku ya Jumapili lakini akatolewa uwanjani kabla ya mechi kumalizika. Watakatifu hao wa St Mary's waslishindwa 3-0 na Chelsea.
 
Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri amedokeza kuwa Ruben Loftus-Cheek aliachwa nje ya kikosi katika mechi dhidi ya Southampton kwa sababu kiungo huyo alicheza dakika 70 siku ya Alhamisi.
 
Mshambuliaji Manolo Gabbiadini amekiri kuwa angelitafakari ofa alizopata msimu wa jota laiti angelijua ataendelea kusalia Southampton. Mchezaji huyo alianza kucheza katika ligi ya Premia msimu huu siku ya Jumapili lakini akatolewa uwanjani kabla ya mechi kumalizika. Watakatifu hao wa St Mary's waslishindwa 3-0 na Chelsea.
Sarriball itawauwa wengi
 
England na Tottenham wana hofu kuhusiana na hali ya Danny Rose baada ya Mauricio Pochettino kuthibitisha kuwa mchezaji huyo wa miaka 28 anakabiliwa na tatizo la mara kwa mara la kinena (London Evening Standard)
 
Meneja wa Crystal Palace Roy Hodgson anasema hakuna miujiza itakayobadilisha mkondo wa mchezo wao baada ya kushindwa mara tatu katika mechi nne katika uga wa Selhurst Park (Football London)
 
Lucas Digne wa Everton, 25, amepuuzilia mbali uwezekano wa kuzuka uhasama kati yake na Leighton Baines,33, kuhusiana na nafasi ya beki wa kushoto baada ya kuishindia nafasi katika kikosi cha kwanza (Liverpool Echo)
 
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero, kipa wa Liverpool Alisson, mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema na straika wa Paris St-Germain Edinson Cavani ni miongoni mwa wachezaji walioteuliwa kushindania tuzo ya Ballon d'Or mwaka huu.

Mshambuliaji wa Wales Gareth Bale anayechezea Real Madrid pia ameorodheshwa kushindania.
 
Waandalizi wa tuzo hiyo watakuwa wakiwatangaza wachezaji watakaowania tuzo hiyo mwaka huu kwa mafungu siku yote hadi wafike wachezaji 30.


Ballon d'Or ni tuzo mashuhuri ambayo imekuwa ikitolewa tangu mwaka 1956 na hutolewa kwa mchezaji bora zaidi wa mwaka wa kiume duniani.

Sherehe ya kumtangaza mshindi itafanyika mjini Paris mnamo 3 Desemba.

Mchezaji bora wa kike duniani pia atatunukiwa kwa mara ya kwanza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom