Wafuasi wa chama tawala cha Paul Biya wanamuita mgombea wao kama shujaa,lakini kwa vijana wengi wanahoji kwamba kumekuwa na ahadi nyingi ambazo hazitekelezeki,wao wanahitaji mabadiliko
Pamoja na hali ya vurugu na matumizi ya nguvu kutoka vyombo vya dola,upinzani wanaomuunga mkono mgombea wa CRM Maurice wanasema zama za raias Biya zimekwisha na kwamba ni wakati wao sasa.
Mgombea wa upinzani wa kiti cha urais kwa mara ya kwanza Joshua Osih, wa chama cha SDF ametamba kwambva ana uwezo wa kutatua matatizo ya Cameroon ndani ya siku 100.
Kuna jumla ya wagombea tisa wa nafasi ya urais katika uchaguzi huo mkuu wa Cameroon,huku taifa hilo likionekana kuwa na mgawanyiko mkubwa kwa misingi ya lugha.