Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20181005-063001.jpeg
 
Aliyekuwa kiongozi wa kundi la wanamgambo wa kiislamu nchini Somalia, Alshabab ametangaza kuwa atawania uongozi serikalini.

Mukhtaar Roobow anayefahamika pia kama Abu Mansur, alijitoa katika kundi la Alshabaab mwaka wa 2012 lakini akajisalimisha kwa serikali ya Somalia mnamo Agosti mwaka jana.

Atawania urais wa jimbo la Kusini Magharibi mwa Somalia katika uchaguzi wa kieneo mwezi ujao.
Screenshot_20181005-063911.jpeg
 
Tazama mkate huu kwenye picha. Bila shaka unakaa kama mkate mwingine wowote wa kawaida.

Hatahivyo umepikwa kwa unga wa kombamwiko.

Watafiti wa vyakula Brazil walivumbua unga huu kama suluhu kwa tatizo la uhaba wa chakula duniani. Mkate wa kawaida wa gramu 100 ulikuwa na gramu 9.7 za protini.

Mkate wa kombamwiko wa gramu 100 una gramu 22.6 za protini. Amua wewe je, upo tayari kula mkate wa kombamwiko?
Screenshot_20181005-064032.jpeg
 
Maajabu!!
Jamaa ya mtu mmoja alifariki kutokana na ugonjwa hatari wa Ebola katika kijiji kimoja Mashariki ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo,waliwashambulia na kuwajeruhi vibaya wahudumu wa afya waliokuwa wameuchukua mwili huo kwa ajili ya kuuzika kwa njia itakayozuia maambukizi zaidi.

Wenyeji wa kijiji cha Butembo wanasema kuwa hawaamini kuwa ugonjwa wa ebola upo !!

Hata baada ya watu takriban 100 kufariki Shirika la afya duniani WHO linasema imani potofu zinachangia kuenea kwa ugonjwa huu unaoua na kuenea haraka kwa kuugusa mtu aliyeambukizwa. Jamani ulimwengu umepasuka wapi?
Screenshot_20181005-064140.jpeg
 
Gwiji wa nyimbo za Benga Joseph Kamaru kutoka Kenya amefariki.

Mwanamuziki huyu 79, anayejivunia zaidi ya nyimbo 2,000 katika lugha ya kikikuyu alitamba katika miaka ya 1980 kwa kibao maarufu “Tiga Kuhenia Igoti” (Usihadae mahakama)

Rais Uhuru Kenyatta ni miongoni wa mashabiki waliotuma rambi rambi zao.
Screenshot_20181005-064316.jpeg
 
Mwanamke wa pili amefariki baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio maarufu kama ”Brazilian Butt Lift ” BBL.

Upasuaji huu umeibuka kuwa maarufu miongoni wanawake kutokana na shinikizo la jamii na baadhi ya wanawake kutaka kuwa na muonekano wa kuvutia.

Watu maarufu kama vile Kim Kardashian , Kylie Jenner na Cardi B wana umaarufu mkubwa katika mitandao ya kijmaii ambapo huchapisha picha zao wakionyesha makalio yao yalio mviringo.

Je ni wakati wa serikali kote duniani kutoa muongozo ili kuokoa maisha ya dada zetu ?

Nyie wanaume wapenda chura mmeona sasa mnasababisha watu kufanya operation ya kuongeza chura wengine mpaka wanakufa cc Behaviourist
Screenshot_20181005-064424.jpeg
 
Mke wa rais wa Marekani Donald Trump Melania anatarajiwa kuwasili Nairobi Kenya leo jioni katika ziara yake ya kwanza barani Afrika.

Bi Melania anatarajiwa kuangazia masuala ya afya na elimu chini ya kibwagizo bebest.

Ziara hii ya juma moja ilianzia ghana
Screenshot_20181005-064643.jpeg
 
“USIENDE NYAMA KWA NYAMA”

Hiyo ndio kibwagizo cha mifuko ya kondomu zilizozinduliwa na jeshi la Uganda katika kambi ya kijeshi ya UPDF Bombo.

Brigedia Leopoldo Kyanda alisema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila yake wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi.

Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi.

Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.

Je hatua hii itaimarisha vita dhidi ya ukimwi jeshini?

Haya sasa wazee wa kupiga kavu ujumbe wenu wazee wa nyama kwa nyama
Screenshot_20181005-064751.jpeg
 
Hauzimiiiiiiiiiiiiiiiiiii moto hauzimiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii uwake motoooooooo moto na uwakeeeeeeeeeeeee
tapatalk_1536779357107.gif
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom