Obe
Platinum Member
- Dec 31, 2007
- 10,278
- 35,639
Muziki: Zamani Kidogo Jana
Sio zmani sana lakini, kilikuwa ni kipindi kama jana tu wakati huwa kwa sisi wa mikoani na mawilayani tukienda kuangalia video (sio sinema) kwenye kumbi za CCM, shuleni, maghala ya ushirika au kumbi za harusi ambazo nyingi zilikuwa chini ya wakatoriki. So kwa wengine sie tulishangaa misalaba na picha za Yesu mzungu. Anyway si lengo langu kuandika niliyoandika bila kukusalimia wewe Kapuku tunayeheshimiana. U khali gani? Mimi sijambo na asante kwa kutouliza, maisha yanasonga.
Muziki sasa, ni muda mzuri wa kukumbuka zamani, kipindi LY inasifika si kidogo mikoani, ukiwa darasa la saba (standard seven) unajiita LY na mwalimu anakufundisha kuwa msafi na kukufuatilia kwa ukaribu maana ndo wengine tulianza kupevuka, ndoto nyevu na oh, nilisahau, likizo ya kuingia LY ndo unapelekwa kijijini kutahiriwa ili uruhusiwe kwenda kuoga ziwani na kushangaashangaa shanga za wadada waliokuwa nao wakija kuoga ziwani. Nimetokea ziwani na nimekumbuka leo nikaona nikuburudishe na muziki mzuri
Sio zmani sana lakini, kilikuwa ni kipindi kama jana tu wakati huwa kwa sisi wa mikoani na mawilayani tukienda kuangalia video (sio sinema) kwenye kumbi za CCM, shuleni, maghala ya ushirika au kumbi za harusi ambazo nyingi zilikuwa chini ya wakatoriki. So kwa wengine sie tulishangaa misalaba na picha za Yesu mzungu. Anyway si lengo langu kuandika niliyoandika bila kukusalimia wewe Kapuku tunayeheshimiana. U khali gani? Mimi sijambo na asante kwa kutouliza, maisha yanasonga.
Muziki sasa, ni muda mzuri wa kukumbuka zamani, kipindi LY inasifika si kidogo mikoani, ukiwa darasa la saba (standard seven) unajiita LY na mwalimu anakufundisha kuwa msafi na kukufuatilia kwa ukaribu maana ndo wengine tulianza kupevuka, ndoto nyevu na oh, nilisahau, likizo ya kuingia LY ndo unapelekwa kijijini kutahiriwa ili uruhusiwe kwenda kuoga ziwani na kushangaashangaa shanga za wadada waliokuwa nao wakija kuoga ziwani. Nimetokea ziwani na nimekumbuka leo nikaona nikuburudishe na muziki mzuri

