Makapuku Forum

Makapuku Forum

BABA Yetu na Mungu wetu Tunakushukuru sana kutuamsha salama leo Jumatatu Tarehe 23 Julai 2018.Tunaomba Toba Baba kwa yote ambayo tumekosa kwa mawazo,maneno, matendo Uturehemu Baba.

Kaa nasi Baba ..Bariki kazi za mikono yetu.Bariki Familia zetu endelea kutupigania Mfalme wa Amani.

Asante kwa ajili ya uponyaji wa wagonjwa wetu na faraja kwa wafiwa ,wagane ,yatima na wote waliopondeka mioyo endelea kuwapigania Baba.

Asante kwa ajili ya watoto wetu wa kike na kiume Baba waoneshe njia iliyosahihi ili waje wakuone wewe.

Wiki hii na Jumatatu ya leo Roho Mtakatifu Tuongoze ,Tufundishe,
Tukumbushe kuwajibika na kutumikia bila kuchoka.

Malaika walinzi waweke vituo katika kila familia tuwe salama Damu ya Yesu Kristo itufunike na itukinge na hatari zote za mwili na roho.Wasafiri waende na kurudi salama tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo.
AMEN

JUMATATU NJEMA NA WIKI YA USHINDI DAMU TAKATIFU YA YESU ITUFUNIKE
 
Makapuku tupate Café kutoa ,mining'inio ya Jana ,kwa Shayo ,karibuni
IMG_20180723_112428.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom