Makapuku Forum

TUOMBE:

Baba yetu uliye Mbinguni Asante kwa Asubuhi ya leo Jumanne tarehe 17 Julai 2018...ni kwa huruma yako iliyo kuu Mungu umetupa tena siku ya leo ya kupendeza Asante Baba hakuna cha kukulipa ila kukutukuza tu.

Tunaomba Toba Baba mwema uturehemu twakusihi na utufanye kuwa wanafunzi wema na kuiishi neema hii ya uzima kwa Upendo na Nidhamu ...mioyo yetu ikuzalie matunda mema.

Tunashukuru kwa uponyaji wa wagonjwa,asante kwa kuwaponya waliojeruhiwa na kupondeka mioyo,asante kwa baraka tele za kimwili na kiroho Asante kwa kuendelea kutupigania katika safari yetu hii ya maisha asante kwa ajili ya wenza wetu na zawadi kubwa ya upendo na uvumilivu kutoka kwao, asante kwa ajili ya watoto na wajukuu na vizazi ulivyotupa na asante kwa ajili ya baraka ya masomo,kazi,biashara,
nyumba ,magari,pikipiki,
baiskeli hata miguu ambayo tunatumia kutembelea popote Baba tunaendelea kukuinua katika maisha yetu kila iitwapo leo.

Tunaomba uanze nasi na kumaliza nasi siku ya leo gusa kila eneo tutakapokua leo na tuendelee kukuinua na kukutumikia mikono yetu,mawazo yetu,miili na roho ikuzalie matunda mema.Bariki wasafiri majini,nchi kavu,angani tuende na kurudi salama.Damu Takatifu ya Yesu Kristo itufunike.

Baba tunaomba utusaidie kuwa na uvumilivu kwa kila gumu tunalopitia kila tuwapo tuuone USHINDI kupitia wewe.
Tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo Amen.

JUMANNE NJEMA DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ITUFUNIKE.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom