Makapuku Forum

Makapuku Forum

TUOMBE:Tunakushukuru Baba Mungu wa Mbinguni kwa kuwa Unatupenda sana umetulinda Usiku kucha na kutuamsha salama leo jumanne tarehe 20 Februari 2018
Kwa jina la Yesu Umetuzuilia hatari zote za mwili na za roho na maumivu yote .Tunaomba Roho Mtakatifu kaa nasi siku ya leo Utuongoze. Baba Tunaomba utusamehe makosa yetu yote tuliyotenda kwa mawazo Kwa maneno kwa matendo na kwakutotimiza wajibu wetu mbalimbali na Tunawasamehe wote waliotukosea.Tunakuomba utulinde mchana wa leo tusikose njia zako wala kupatwa na maovu Utupe kukupendeza wewe kwa maneno na matendo Mwenendo wetu uwe mzuri kwani mwili na roho vyote ni mali yako naviweka mikononi mwako. Malaika wako wawe pamoja nasi sote Shetani asitushinde Wafariji wafiwa wote wajane wagane na wahitaji wote ponya wagonjwa na waliovunjika moyo ondoa kiburi,masengenyo kujikweza na dharau tupendane na kuheshimiana kila mmoja amuone mwenzake kuwa wa thamani na ameumbwa kwa mfano wako Mfalme wa Amani.Walinde wasafiri wote wa majini Angani Nchi kavu ponya familia na ndoa zetu na wote wanaotusaidia katika kazi za kila siku wakujue wewe Baba Bariki kazi za mikono yetu na utupatie riziki halali tunaomba wabarki watoto wetu majumbani mashuleni na makazini waishi maisha ya kukupendeza na wakutumikie wewe Mungu wetu waepushe na hatari zote za miili na roho wafanikishe katika kila jambo Mungu wetu na katika masomo yao wawe kichwa si mikia.wape kibali mbele zako na watu wote na wawe na hofu yako Mungu wetu.Tubariki na kutulinda kila tuingiapo na kutoka bariki kazi za mikono yetu zizae matunda ya kukupendeza tujalie kila lililo jema Mungu wetu na Baba yetu.

Tunaomba haya Baba katika jina la Yesu Amen AMEN

SIKU NJEMA MBARIKIWE
 
Hahahaa...!
Mazoea mabaya
3efa5dd5ec30f44666a898ff5f99c24f.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom