Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Kutofautiana na Watawala ni Afya ya Utawala

Mada ngumu hii na ugumu umeanza na kichwa cha habari, tafasiri unavyoweza. Tunatofautiana kwa mengi, kibinafsi yaani mmoja mmoja hata kama tuko pamoja sembuse kutofautiana na utawala. Najiaminisha ushawahi kusikia hii kauli ya kukubaliana kutokubaliana. Kama ndo unaisoma leo hapa basi una mengi ya kukielewa kipengele hiki na kama kawaida Makapuku Forum ipo makini kuongeza pale ulipoishia na itapokea kutoka kwako pale ilipoishia. Tafasiri unavyoweza.

Wengi wengi tunadhani kukubaliana katika kila kitu ndo kuelewana, la hasha na hasa inakuja upande wa kukubaliana na utawala. Utawala una mawazo yake, yapo tunayokubaliana nayo na yapo ambayo hatukubaliani nayo. Tambua tu kuwa tawala kutawala si mara zote zinakuwa na ruhusa yako na zikitaka kufanya jambo, japo zinapaswa kukuuliza lakini mara nyingi hujifanyia zinavyoona zenyewe na hapa ndipo hoja yangu inasimamia, kutokubaliana na utawala na wenyewe ukajua kuwa hukubaliani nao ni afya njema ya jamii inayotaka kusonga mbele.

Jefferson (1743-1826) aliwahi kuwa rais wa Marekani na moja ya nukuu zake ni kuhusu kukinzana kimtizamo na serikali ni jambo lenye afya kwa maendeleo ya taifa. Hatuwezi kukubaliana kwa kila kitu, wanaotuongoza na madhamana wetu madarakani si malaika hata kama watajiona wana hadhi hiyo. Kiongozi anayeongoza kwa utashi binafsi ukimwambia umekosea atakutumia vyombo vya usalama lakini usipochoka kumwambia atajirudi maana anajua nguvu uliyo nayo ukiamua kusimama na kusema hiki ndicho nataka na si hicho unachokitaka kukifanya. Tuna katiba na sheria, tumeweka vyombo vya kuangaliana na sisi wananchi ndo tuna nguvu zaidi ya polisi na wasalama wengine. Historia haidanganyi, rudi darasani na kama huridhiki basi endelea kulalamikia mtungini na ukiweza, tafasiri unavyoweza.

1af8f60bd8e673b01755507145c16401.jpg
 
Muziki: Mheshimu Anayekujengea Kujiamini

...u khali gani Kapuku mheshimika, natumaini ulikuwa na wikend nzuri na hasa kama wewe ni shabiki wa Manchester United na Arsenal na kwa Kujiamini ulibet 🙂. Mimi wikend ilikuwa nzuri sana maana "zis iz Simba bhana" tulifanya yetu pale tuliposimamia shoo ya bao nne.

Nimefurahi leo kiukweli tangu mornie pale nilipomsoma anko wangu Lyon Lee akituletea magazeti. Ujue anko alinilalamikia kuwa auntie Shunie ambaye ana app ya kubet, mkeka umetakata na alipovuta mpunga basi simu akaweka silence, ukipiga hakusikii, labda utume meseji. Hongera kwa wote wenye ujasiri wa kubet. Mheshimu sana aliyekujengea uwezo wa kujiamini kubet.

Muziki sasa, burudika na ngoma hii kuusindikiza usiku wako.

BTW, nimefurahi kukuona tena BlessedHope na kesho kutwa ndo VD, nakutafutia zawadi, nitawajulisha wote wanaosema kwa namna navyokufuatilia Basi nastahili phd

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom