Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Nafunga Wiki Tanzania 2038

Kwanza nijipongeze, nimeandika kipengele hiki kwa siku zote za kazi Jtatu-Ijumaa. Inawezekana kabisa kutokana na namna ushiriki wa wengi umeonekana kupunguza hapa, nimepata nguvu zaidi ya kuandika na kusoma mwenyewe, tafasiri Unavyoweza. Soma mpaka mwisho.

Kupanga mipango ni jambo zuri, iwe ya kibinafsi, familia, jamii na nitaongelea zaidi mipango kama jamii/taifa ya Tanzania. Shirika la Idadi ya Watu linaonesha takwimu kuwa tumekuwa na ongezeko kubwa la watu nchini, tunazaana sana, hili si jambo baya. Kati ya 2002 -2012 Idadi ya watu iliongezeka kwa asilimia 30 (34mil hadi milioni 45. Na kwa kiwango cha 2.7 tunachozaliana basi mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tuombe uzima.
Mipango ya muda mrefu ikoje, au ndo habari za kuendeleza DSM peke yake huku mikoa mingine ikiachwa hohehahe bila miundombinu ya maana. Kilimo je, siasa ya kilimo inayomfanya mkulima aonekane mjinga itabadilishwa? Kama tukidharau na kutoa bajeti ndogo ya kilimo, serikali ina mpango wa kutufanya 'tukulane wenyewe' . Fikiria Unavyoweza , nachokoza tu.

Elimu tunaitizama vipi kwenye zama hizi za kufyatua tu, utawala bora je! Umeme wa kusuasua unaofaidisha kimkono wa birika asilimia 41 tu ya wananchi. Pato (GDP) kwenye Kilimo haliko imara kisa madini.
Fikiria Unavyoweza, nafunga wiki na Tanzania mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tunza afya.
Tafakari njema
 
Muziki: FurahiDay Mdau Mwaminifu


...maneno machache kwa sababu ya ukimya unaoendelea kutamalaki humu jamvini. Hakijaharibika kitu maana bado wengi wetu tukipata muda tunachungulia na kusmile kisha tunaendelea tunapotaka kwenda, JF ni kama bahari, kubwa mno kuanzia jukwaa la juu hadi la chini, hapo sijaoongea vijijukwaa vya msimu. Uzuri ni kuwa Makapuku ilionekana kuwa ya msimu lakini imesimama kuliko moja. Hongera kwako unayelifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo.


Muziki sasa, sijaacha kuwakumbuka hata kidogo, mnalijua hilo. Nakutakia wikend njema mdau mwaminifu


Asante kwa muziki Obe
 
Zaburi 131

1 .BWANA, moyo wangu hauna kiburi, Wala macho yangu hayainuki. Wala sijishughulishi na mambo makuu, Wala na mambo yashindayo nguvu zangu.

2 .Hakika nimeituliza nafsi yangu, Na kuinyamazisha. Kama mtoto aliyeachishwa Kifuani mwa mama yake; Kama mtoto aliyeachishwa, Ndivyo roho yangu ilivyo kwangu

3 .Ee Israeli, umtarajie BWANA, Tangu leo na hata milele.

JUMAPILI NJEMA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom