Tafasiri Unavyoweza: Nafunga Wiki Tanzania 2038
Kwanza nijipongeze, nimeandika kipengele hiki kwa siku zote za kazi Jtatu-Ijumaa. Inawezekana kabisa kutokana na namna ushiriki wa wengi umeonekana kupunguza hapa, nimepata nguvu zaidi ya kuandika na kusoma mwenyewe, tafasiri Unavyoweza. Soma mpaka mwisho.
Kupanga mipango ni jambo zuri, iwe ya kibinafsi, familia, jamii na nitaongelea zaidi mipango kama jamii/taifa ya Tanzania. Shirika la Idadi ya Watu linaonesha takwimu kuwa tumekuwa na ongezeko kubwa la watu nchini, tunazaana sana, hili si jambo baya. Kati ya 2002 -2012 Idadi ya watu iliongezeka kwa asilimia 30 (34mil hadi milioni 45. Na kwa kiwango cha 2.7 tunachozaliana basi mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tuombe uzima.
Mipango ya muda mrefu ikoje, au ndo habari za kuendeleza DSM peke yake huku mikoa mingine ikiachwa hohehahe bila miundombinu ya maana. Kilimo je, siasa ya kilimo inayomfanya mkulima aonekane mjinga itabadilishwa? Kama tukidharau na kutoa bajeti ndogo ya kilimo, serikali ina mpango wa kutufanya 'tukulane wenyewe' . Fikiria Unavyoweza , nachokoza tu.
Elimu tunaitizama vipi kwenye zama hizi za kufyatua tu, utawala bora je! Umeme wa kusuasua unaofaidisha kimkono wa birika asilimia 41 tu ya wananchi. Pato (GDP) kwenye Kilimo haliko imara kisa madini.
Fikiria Unavyoweza, nafunga wiki na Tanzania mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tunza afya.