BlessedHope
JF-Expert Member
- Jan 29, 2016
- 7,988
- 32,649
TUOMBEKwajina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu Amen
Baba katika Jina la Yesu Asante kwa siku mpya ya leo Ijumaa tarehe 19 JANUARI
2018 ambayo umetuchagua tena tuweze kuuona Utukufu wako.
watu wengi walitamani nafasi hii hawajaweza kuiona siku ya leo uliwatwaa Baba .
Karibu Roho Mtakatifu shusha Mapaji tuwe Imara siku ya leo
BABA Tunakuomba Utusamehe makosa yetu yote ambayo tumetenda kwa mawazo kwa maneno kwa matendo na kutotimiza wajibu wetu mbalimbali tulionao.
Uturehemu twakusihi Baba yetu
Tunaomba utusaidie kuwasamehe wale wote waliotukosea Mfalme wa Amani walioomba msamaha na wale ambao hawajaomba msamaha tuwasamehe na kuyasahau yote waliyotutendea
Wabariki wote katika Ndoa na nyua zetu familia zetu Waume Wake Watoto Wasaidizi wa ndani Ndugu Jamaa Marafiki Wachumba wakutafute wewe kwa bidii Baba
Bariki viongozi wa Serikali wakutafute kwa
Bidii Nchi iwe na Amani wakatende haki na kuwa na hofu yako itawale kwao.
Baba Ponya Wagonjwa na ponya dawa wanazotumia na wanawauguza waweze kutoa huduma kwa Upendo wasipungukiwe.
Tunakushukuru kwa uponyaji unaoendelea Baba kwa wagonjwa wetu wote tunaomba afya zao zizidi imarika
Walinde wajawazito wote na wanaojifungua Baba umewapa kibali cha kushiriki kazi ya uumbaji kila walichobeba ni wazo lako Baba tunaomba wawe salama mikononi mwako wao na viumbe ulivyowakabidhi mfalme wa Amani
Asante kwa uwepo wako katika hatua zote za uumbaji na ushiriki wao.
Baba Bariki wasafiri na vyombo Majini Nchi Kavu na hata Angani ukawe Dereva mwema Damu ya Yesu itufunike tuendako na tunakotoka tuwe salama.
Baba wafariji Wafiwa Wajane Wagane Yatima Wafungwa Mahabusu Wenye huzuni na wahitaji wote Walioachwa Waliotelekezwa wasio na chakula Waliodhurumiwa wakuangalie na kukutegemea wewe tu maana imeandikwa Heri aliyemfanya Bwana kuwa Tumaini lake.
Baba tunakuomba Tupatane na Wenzetu Tuwasamehe Tuwapende daima.
Tujalie Amani Mfalme wa Amani ,tupe faraja Mfariji mwema tunakutegemea wewe tu.
Bariki kila kazi za mikono yetu ziwe Halali na za kukupendeza na wasio na kazi na shughuli halali wakumbuke baba yetu mwema.
Baba Asante kwa Sababu Unatupenda na utajibu sawasawa na mapenzi yako Amen
Tunaomba yote haya kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth Mpatanishi Mfariji na Mwokozi wetu Amen
DAMU YA YESU ITUFUNIKE

SHALOM




