Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Weka Bustani Mezani

Mlo uliokamilika haushibishi tumbo tu, unaupa mwili nguvu, joto na mengine mengi tunayohitaji kama binadamu. Utakuwa umegundua kuwa kipengele Cha leo hakiongelei mlo shibisha tumbo bali mlo mwili unahitaji.
Bustani unaweza itafasiri unavyoweza, ipo ya wanyama, maua, mboga n.k. Nitajikita kwenye maana ya mazoea , Bustani ya mbogamboga.

Imekuwa ni kawaida sana kwa sasa family nyingi wakati wa mlo kusahau mbogamboga na matunda, mazao ya bustani. Mlo umekuwa ni mzito na unasukumizwa na maji au vinywaji vingine. Tunasahau kabisa kula mboga mboga na matunda kukamilisha mlo kamili.

Tafasiri Unavyoweza, ni wakati wa kuileta bustani mezani. Mlo wowote uendane na mazao ya bustani. Ni suala la mlo kamili na tambua kabisa tomato sauce (ketchup) si mbadala wa bustani. Jipe nafasi usome inanini ndani yake, ukiweza waweza tushirikisha umekutana na nini ndani ya sauce tunayoipenda kwenye viepe
 
Habari wana JF
Habari Makapuku wenzangu
Matumaini yangu wote mko poa kabisa.

Uzi huu ni kwaajili ya makapuku wote. Lengo ni kujadili changamoto zinazotukabili, pia Kupeana support katika mambo yetu hapa JF. Tupeane mbinu za kukabiliana na mambo yote humu.

Makapuku natumaini nyote tutashirikiana katika jambo hapa JF. Bila kumsahau founder wa makapuku Bitoz shukrani kwake

Karibu sana makapuku katika mjadala. Wengine nitawaongeza hapo baadae.

Karibu sana

Bitoz
JF Makapuku Founder

Jimena
JF Makapuku assistant Founder

Th Name JF Makapuku assistant Founder
Ushauri kwa Mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya, Wizara ya michezo, TFF pamoja na BMT
 
Tafasiri Unavyoweza: Nafunga Wiki Tanzania 2038

Kwanza nijipongeze, nimeandika kipengele hiki kwa siku zote za kazi Jtatu-Ijumaa. Inawezekana kabisa kutokana na namna ushiriki wa wengi umeonekana kupunguza hapa, nimepata nguvu zaidi ya kuandika na kusoma mwenyewe, tafasiri Unavyoweza. Soma mpaka mwisho.

Kupanga mipango ni jambo zuri, iwe ya kibinafsi, familia, jamii na nitaongelea zaidi mipango kama jamii/taifa ya Tanzania. Shirika la Idadi ya Watu linaonesha takwimu kuwa tumekuwa na ongezeko kubwa la watu nchini, tunazaana sana, hili si jambo baya. Kati ya 2002 -2012 Idadi ya watu iliongezeka kwa asilimia 30 (34mil hadi milioni 45. Na kwa kiwango cha 2.7 tunachozaliana basi mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tuombe uzima.
Mipango ya muda mrefu ikoje, au ndo habari za kuendeleza DSM peke yake huku mikoa mingine ikiachwa hohehahe bila miundombinu ya maana. Kilimo je, siasa ya kilimo inayomfanya mkulima aonekane mjinga itabadilishwa? Kama tukidharau na kutoa bajeti ndogo ya kilimo, serikali ina mpango wa kutufanya 'tukulane wenyewe' . Fikiria Unavyoweza , nachokoza tu.

Elimu tunaitizama vipi kwenye zama hizi za kufyatua tu, utawala bora je! Umeme wa kusuasua unaofaidisha kimkono wa birika asilimia 41 tu ya wananchi. Pato (GDP) kwenye Kilimo haliko imara kisa madini.
Fikiria Unavyoweza, nafunga wiki na Tanzania mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tunza afya.
 
Tafasiri Unavyoweza: Nafunga Wiki Tanzania 2038

Kwanza nijipongeze, nimeandika kipengele hiki kwa siku zote za kazi Jtatu-Ijumaa. Inawezekana kabisa kutokana na namna ushiriki wa wengi umeonekana kupunguza hapa, nimepata nguvu zaidi ya kuandika na kusoma mwenyewe, tafasiri Unavyoweza. Soma mpaka mwisho.

Kupanga mipango ni jambo zuri, iwe ya kibinafsi, familia, jamii na nitaongelea zaidi mipango kama jamii/taifa ya Tanzania. Shirika la Idadi ya Watu linaonesha takwimu kuwa tumekuwa na ongezeko kubwa la watu nchini, tunazaana sana, hili si jambo baya. Kati ya 2002 -2012 Idadi ya watu iliongezeka kwa asilimia 30 (34mil hadi milioni 45. Na kwa kiwango cha 2.7 tunachozaliana basi mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tuombe uzima.
Mipango ya muda mrefu ikoje, au ndo habari za kuendeleza DSM peke yake huku mikoa mingine ikiachwa hohehahe bila miundombinu ya maana. Kilimo je, siasa ya kilimo inayomfanya mkulima aonekane mjinga itabadilishwa? Kama tukidharau na kutoa bajeti ndogo ya kilimo, serikali ina mpango wa kutufanya 'tukulane wenyewe' . Fikiria Unavyoweza , nachokoza tu.

Elimu tunaitizama vipi kwenye zama hizi za kufyatua tu, utawala bora je! Umeme wa kusuasua unaofaidisha kimkono wa birika asilimia 41 tu ya wananchi. Pato (GDP) kwenye Kilimo haliko imara kisa madini.
Fikiria Unavyoweza, nafunga wiki na Tanzania mwaka 2038 tutakuwa milioni 90, tunza afya.
Shikamoo binamu
 
Muziki: FurahiDay Mdau Mwaminifu


...maneno machache kwa sababu ya ukimya unaoendelea kutamalaki humu jamvini. Hakijaharibika kitu maana bado wengi wetu tukipata muda tunachungulia na kusmile kisha tunaendelea tunapotaka kwenda, JF ni kama bahari, kubwa mno kuanzia jukwaa la juu hadi la chini, hapo sijaoongea vijijukwaa vya msimu. Uzuri ni kuwa Makapuku ilionekana kuwa ya msimu lakini imesimama kuliko moja. Hongera kwako unayelifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo.


Muziki sasa, sijaacha kuwakumbuka hata kidogo, mnalijua hilo. Nakutakia wikend njema mdau mwaminifu

 
Muziki: FurahiDay Mdau Mwaminifu


...maneno machache kwa sababu ya ukimya unaoendelea kutamalaki humu jamvini. Hakijaharibika kitu maana bado wengi wetu tukipata muda tunachungulia na kusmile kisha tunaendelea tunapotaka kwenda, JF ni kama bahari, kubwa mno kuanzia jukwaa la juu hadi la chini, hapo sijaoongea vijijukwaa vya msimu. Uzuri ni kuwa Makapuku ilionekana kuwa ya msimu lakini imesimama kuliko moja. Hongera kwako unayelifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo.


Muziki sasa, sijaacha kuwakumbuka hata kidogo, mnalijua hilo. Nakutakia wikend njema mdau mwaminifu


Na kwako mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom