Muziki: Wikend ya Sikukuu
...habari za Ijumaa Makapuku wenzangu, sijambo na kadri mwaka unavyoelekea kuisha ndo najiona hikma (wisdom) nazo zinazidi kuongezeka kwa hiyo kwa wote wenye kutaka ushauri nasaha basi ninawakaribisha kwa a very reasonable fee, yeah, utalipia hekima utakazokutana nazo kwenye ushauri wangu. Hakuna cha bure, kama vyuma vimekaza tafuta plastic yenyewe inafuata unavyoielekeza.
TGIF na kama unavyojua huwa ni wakati wa kujirusha bakulutu kidogo, kusikiza story za wadau na zaidi kulichangia kodi taifa letu kwa kunywa na kula. Sio unakula nyumbani Monday to Sunday, siku nyingine unavamia kwa friends mida ya msosi na unawaharibia ratiba zao. Ndo utamaduni huo. Na Ijumaa unakaa sehemu na friends unaangusha moja moja pamoja mmojammoja. Kama una mpango wa kutegemea mfuko wa mwenzako basi mjulishe mapema usijekutana na wasio na haya kama anko wangu ambaye yeye anaweza kuagiza bia mbili kwa mkupuo na akazinywa huku anakuangalia kwa tabasamu ambalo ni kama linasema 'mhudumu huyu hapo, muite uagize mbili kwa hela yako'.
Muziki sasa, ninakukumbuka wakati wote kapuku mheshimika na sitochoka kukwambia kuwa bila wewe jukwaa hili linabaki kuwa debe tupu, lakini kwa uwepo wako hapa, tumekuwa sio mfano tena bali original. It's furahiday and wishing you a happy almost Christmas with love