
TUOMBE Baba katika jina la Yesu Kristo ni siku mpya kabisa ya ALHAMIS NJEMA BABA UMETUAMSHA TENA SALAMA Tunasema Asante Baba Sifa Shukurani Heshima Utukufu ni kwako peke yako wewe uliye Alfa na Omega Wapo wengi walitamani kuiona leo Baba hawajaweza sisi ni nani Baba ?Hakika TUNAKUSHUKURU tunakuomba Utusamehe Dhambi zetu tulizofanya kwa Mawazo na Maneno na Matendo ,kwakujua na kutojua ,Tushike Mwenendo Mpya
Baba wasamehe na uwabariki wote walioko majumbani kwetu waume zetu ,wake zetu ,watoto wetu, ndugu ,jamaa ,marafiki zetu na wasaidizi wetu siku zote wakutafute wewe
Ponya ndoa zetu Baba
Ponya Familia zetu
Tunaomba ponya Wagonjwa bariki dawa wanazokunywa na wote wanaowahudumia wawahudumie kwa Upendo
Walinde Wasafiri wote wa Nchi kavu Majini na Angani Bwana Yesu awe dereva wa kila chombo na pia Damu ya Bwana Yesu iwafunike
Wafariji Wafiwa Watie moyo Wajane, Wagane, Yatima , Walioachwa, Waliotelekezwa, Wasio na Makazi, Wafungwa, Wakukimbilie wewe Mfalme wa Amani
Baba Bariki Uchumi wetu ukakue kazi za Mikono yetu Ajira Ujasiriamali Biashara Mashamba Bariki Masomo ya kila mmoja Baba ukaonekane kwetu Mungu wetu
Epusha migogoro, magomvi, chuki, dharau, mikosi, balaa zote, ukatukinge na pepo wachafu
Tutakase Baba tunayo mahitaji mengi na kila moja unalifahamu Tunaomba Uonekane katika kila eneo
Asante kwa sababu utatupatia sawa na Mapenzi yako.
TUNAOMBA,TUNASHUKURU TUNAAMINI KATIKA JINA LA YESU AMEN.
SHALOM Muwe na siku njema Mbarikiwe


