
TUOMBE
Baba ni siku nyingine mpya ya Jumatano Desemba 20 ,2017 Baba umetuamsha tena tukiwa ni wenye Afya njema na nguvu
Tunakushukuru sana Baba wa Mbinguni kwa wema wako unaotutendea siku hadi siku Baba wako wengi walitamani kuiona siku ya leo hawajaweza Baba tunakuomba Uwapokee wapumzike kwa Amani
Sisi umetuamsha salama Baba Tunakurudishia Sifa Utukufu Shukurani na Heshima Mfalme wa Amani
Baba tunakuomba Utusamehe Makosa yetu tunayotenda kwa mawazo maneno na matendo tushike mwenendo Mpya Nasi Tunawasamehe wote waliotukosea walioomba Msamaha na wasioomba msamaha.
Baba walinde wote ndani ya nyuwa zetu Watoto, Waume ,Wake, Ndugu, Wasaidizi wa ndani ,Jamaa na Marafiki zetu wajenge wakujue na wakupende wewe
Baba tuondolee dhiki taabu uchungu unafiki magomvi dharau kiburi tujaze
UPENDO wa kweli .
Asubuhi hii ya leo tunawaombea wagonjwa wote majumbani na mahospitalini Damu ya Yesu inene mema Baba ukawaponye gusa dawa wanazotumia gusa wanaowahudumia na wakuone wewe Mfalme wa Amani
Kwa namna ya pekee tunasema asante kwa uponyaji unaoendelea kwa wagonjwa wote.
Tunaomba uponyaji unaoendelea uwe wa kudumu Mfalme wa Amani.
Wabariki madaktari na manesi watoe huduma njema na uwaepushe na madhara yote wanayowapata wakati wa kutoa huduma kwa wagonjwa
Baba yetu mwema tunakuomba ubariki mipango yetu yote ya Ajira zote Ujasiriamali Biashara Kilimo Mifugo Masomo
Tunakuomba ukaguse kila kazi za mikono yetu na ukaonekane Baba tukapokee kila lililo jema kutoka kwako
Baba Waangalie kwa wema Wasafiri wote wa Majini Nchi kavu Angani ukawe dereva wa kila chombo popote waendako na warudipo epusha ajali za aina zote Baba Damu ya Yesu itufunike
Tubariki Baba Tudumishe Amani na Mshikamano kusiwe na mafarakano ya aina yoyote.
Mungu wetu na Baba yetu unafahamu mahitaji yetu yote kabla hata hatujatamka Baba tujaze Roho Mtakatifu ili tukutafute kwa bidii
Baba Wakumbuke Wafiwa Wajane Wagane Yatima Wenyeshida mbalimbali Wanaohitaji Watoto Wanaohitaji Wachumba wanaotafuta wenza Wanaotafuta kazi Wanaotafuta kuongeza vipato majumbani na makazini Wakumbuke na uwaopoe katika midomo ya Mwovu
Nakuomba walinde wajawazito na wanaojifungua wawe salama wao na uhai uliowapa waubebe maana wanashiriki kazi kubwa ya uumbaji ambayo umeianzisha ndani yao mfalme wa Amani Asante baba maana umewapa jukumu kubwa katika maisha ya binadamu na wasaidie wote wanaotafuta kubeba jukumu hili Baba walipate kwa utukufu wako.
Baba nakushukuru kwa kuwa utatenda sawasawa na mapenzi yako Amen
Tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo Mpatanishi na mwokozi wetu Amen.