Makapuku Forum

Makapuku Forum

TUOMBE

Baba ni siku nyingine mpya ya Jumatano Desemba 20 ,2017 Baba umetuamsha tena tukiwa ni wenye Afya njema na nguvu

Tunakushukuru sana Baba wa Mbinguni kwa wema wako unaotutendea siku hadi siku Baba wako wengi walitamani kuiona siku ya leo hawajaweza Baba tunakuomba Uwapokee wapumzike kwa Amani

Sisi umetuamsha salama Baba Tunakurudishia Sifa Utukufu Shukurani na Heshima Mfalme wa Amani

Baba tunakuomba Utusamehe Makosa yetu tunayotenda kwa mawazo maneno na matendo tushike mwenendo Mpya Nasi Tunawasamehe wote waliotukosea walioomba Msamaha na wasioomba msamaha.

Baba walinde wote ndani ya nyuwa zetu Watoto, Waume ,Wake, Ndugu, Wasaidizi wa ndani ,Jamaa na Marafiki zetu wajenge wakujue na wakupende wewe

Baba tuondolee dhiki taabu uchungu unafiki magomvi dharau kiburi tujaze
UPENDO wa kweli .

Asubuhi hii ya leo tunawaombea wagonjwa wote majumbani na mahospitalini Damu ya Yesu inene mema Baba ukawaponye gusa dawa wanazotumia gusa wanaowahudumia na wakuone wewe Mfalme wa Amani

Kwa namna ya pekee tunasema asante kwa uponyaji unaoendelea kwa wagonjwa wote.

Tunaomba uponyaji unaoendelea uwe wa kudumu Mfalme wa Amani.

Wabariki madaktari na manesi watoe huduma njema na uwaepushe na madhara yote wanayowapata wakati wa kutoa huduma kwa wagonjwa

Baba yetu mwema tunakuomba ubariki mipango yetu yote ya Ajira zote Ujasiriamali Biashara Kilimo Mifugo Masomo


Tunakuomba ukaguse kila kazi za mikono yetu na ukaonekane Baba tukapokee kila lililo jema kutoka kwako

Baba Waangalie kwa wema Wasafiri wote wa Majini Nchi kavu Angani ukawe dereva wa kila chombo popote waendako na warudipo epusha ajali za aina zote Baba Damu ya Yesu itufunike

Tubariki Baba Tudumishe Amani na Mshikamano kusiwe na mafarakano ya aina yoyote.

Mungu wetu na Baba yetu unafahamu mahitaji yetu yote kabla hata hatujatamka Baba tujaze Roho Mtakatifu ili tukutafute kwa bidii
Baba Wakumbuke Wafiwa Wajane Wagane Yatima Wenyeshida mbalimbali Wanaohitaji Watoto Wanaohitaji Wachumba wanaotafuta wenza Wanaotafuta kazi Wanaotafuta kuongeza vipato majumbani na makazini Wakumbuke na uwaopoe katika midomo ya Mwovu

Nakuomba walinde wajawazito na wanaojifungua wawe salama wao na uhai uliowapa waubebe maana wanashiriki kazi kubwa ya uumbaji ambayo umeianzisha ndani yao mfalme wa Amani Asante baba maana umewapa jukumu kubwa katika maisha ya binadamu na wasaidie wote wanaotafuta kubeba jukumu hili Baba walipate kwa utukufu wako.

Baba nakushukuru kwa kuwa utatenda sawasawa na mapenzi yako Amen

Tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo Mpatanishi na mwokozi wetu Amen.
 
Muziki: Ni Likizo, Toa Zawadi

Niko kwenye utalii wa ndani, yeah, mambo ya likizo haya, natalii tu na kuona navyomiss kuviona nikiwa mjini. Si mnajua ninakaa mjini mimi, na nikisema mjini simaanishi Dar maana kuna watu wanadhani Dar yote ni mjini, tembea uone, kuna mitaa Dar hawajawahi kuona gari, na hawajui kama chipsi ni viazi, usiniulize ni wapi utanichosha niko likizo. Ukiondoa hii hali ya mvua lakini ninafaidi mengi sana likizo hii yanayonijenga kiimani, kimwili na kiakili. Nakutana na mazingira halisi na sio feki na hata maisha yangu fake ninayoishi mjini nimeyaacha niliposhuka hapa kijijini. Huku ni uhalisia na sio hisia, kuna tofauti.

Kama ujuavyo kipengele hiki huwa ni kukumbushana na kusogoa kidogo juu ya maisha na hasa maisha yangu ambayo kama yalivyo yako yametawaliwa na vitu hivi, elimu, biashara, teknolojia na mahusiano na utani sijauweka kando. Sasa basi hebu niandike nilichonuaia leo. Likizo ni muhimu, shitaji kukukumbusha hili na kwa wote tunaosafri kuja likizo hata kwa wasiosafir ni vizuri kutoa zawadi, maana kuna vingi tunavyo na hata kama hatuna unaweza kununua vichache ukawazawadie likizoni. Kwanini, likizo ndo muda ambao uanenda kukutana na marafiki ambao waliamua kufanya maisha yao hapo hapo ulipoondoka, wengi ulisoma nao msingi, ukaenda nao sunday school au chuo (madrasa) na zaidi mkaenda kuogelea bwawani pamoja, siongelei jando hapa maana kila mmoja ana kabila lake.

Muziki sasa, likizo itumie vizuri kwa kuwa na muda zaidi wa familia, mazoezi kwa sana maana ni mwendo wa kula na kunywa tu na siku mbili hizi nakaona kakitambi kananijongea kiasi kwamba kujichungulia hadi nijiinamishe nyuzi 45. Likizo njema Kapuku mwenzangu shululu , Tumosa , Transcend , SHIMBA YA BUYENZE , BlessedHope , Shunie , makaveli10 , Lyon Lee , Sakayo , Nyagei , Gentries , dumejeuri , Mndali ndanyelakakomu , mzeewakungoa , moudgulf , husna muba , Werrason , Mussolin5 , Bitoz , Jimena , Mkushi wa kusi , na wewe ambaye hujaenda likizo

 
Muziki: Ni Likizo, Toa Zawadi

Niko kwenye utalii wa ndani, yeah, mambo ya likizo haya, natalii tu na kuona navyomiss kuviona nikiwa mjini. Si mnajua ninakaa mjini mimi, na nikisema mjini simaanishi Dar maana kuna watu wanadhani Dar yote ni mjini, tembea uone, kuna mitaa Dar hawajawahi kuona gari, na hawajui kama chipsi ni viazi, usiniulize ni wapi utanichosha niko likizo. Ukiondoa hii hali ya mvua lakini ninafaidi mengi sana likizo hii yanayonijenga kiimani, kimwili na kiakili. Nakutana na mazingira halisi na sio feki na hata maisha yangu fake ninayoishi mjini nimeyaacha niliposhuka hapa kijijini. Huku ni uhalisia na sio hisia, kuna tofauti.

Kama ujuavyo kipengele hiki huwa ni kukumbushana na kusogoa kidogo juu ya maisha na hasa maisha yangu ambayo kama yalivyo yako yametawaliwa na vitu hivi, elimu, biashara, teknolojia na mahusiano na utani sijauweka kando. Sasa basi hebu niandike nilichonuaia leo. Likizo ni muhimu, shitaji kukukumbusha hili na kwa wote tunaosafri kuja likizo hata kwa wasiosafir ni vizuri kutoa zawadi, maana kuna vingi tunavyo na hata kama hatuna unaweza kununua vichache ukawazawadie likizoni. Kwanini, likizo ndo muda ambao uanenda kukutana na marafiki ambao waliamua kufanya maisha yao hapo hapo ulipoondoka, wengi ulisoma nao msingi, ukaenda nao sunday school au chuo (madrasa) na zaidi mkaenda kuogelea bwawani pamoja, siongelei jando hapa maana kila mmoja ana kabila lake.

Muziki sasa, likizo itumie vizuri kwa kuwa na muda zaidi wa familia, mazoezi kwa sana maana ni mwendo wa kula na kunywa tu na siku mbili hizi nakaona kakitambi kananijongea kiasi kwamba kujichungulia hadi nijiinamishe nyuzi 45. Likizo njema Kapuku mwenzangu shululu , Tumosa , Transcend , SHIMBA YA BUYENZE , BlessedHope , Shunie , makaveli10 , Lyon Lee , Sakayo , Nyagei , Gentries , dumejeuri , Mndali ndanyelakakomu , mzeewakungoa , moudgulf , husna muba , Werrason , Mussolin5 , Bitoz , Jimena , Mkushi wa kusi , na wewe ambaye hujaenda likizo


Dj Obe
 
Muziki: Ni Likizo, Toa Zawadi

Niko kwenye utalii wa ndani, yeah, mambo ya likizo haya, natalii tu na kuona navyomiss kuviona nikiwa mjini. Si mnajua ninakaa mjini mimi, na nikisema mjini simaanishi Dar maana kuna watu wanadhani Dar yote ni mjini, tembea uone, kuna mitaa Dar hawajawahi kuona gari, na hawajui kama chipsi ni viazi, usiniulize ni wapi utanichosha niko likizo. Ukiondoa hii hali ya mvua lakini ninafaidi mengi sana likizo hii yanayonijenga kiimani, kimwili na kiakili. Nakutana na mazingira halisi na sio feki na hata maisha yangu fake ninayoishi mjini nimeyaacha niliposhuka hapa kijijini. Huku ni uhalisia na sio hisia, kuna tofauti.

Kama ujuavyo kipengele hiki huwa ni kukumbushana na kusogoa kidogo juu ya maisha na hasa maisha yangu ambayo kama yalivyo yako yametawaliwa na vitu hivi, elimu, biashara, teknolojia na mahusiano na utani sijauweka kando. Sasa basi hebu niandike nilichonuaia leo. Likizo ni muhimu, shitaji kukukumbusha hili na kwa wote tunaosafri kuja likizo hata kwa wasiosafir ni vizuri kutoa zawadi, maana kuna vingi tunavyo na hata kama hatuna unaweza kununua vichache ukawazawadie likizoni. Kwanini, likizo ndo muda ambao uanenda kukutana na marafiki ambao waliamua kufanya maisha yao hapo hapo ulipoondoka, wengi ulisoma nao msingi, ukaenda nao sunday school au chuo (madrasa) na zaidi mkaenda kuogelea bwawani pamoja, siongelei jando hapa maana kila mmoja ana kabila lake.

Muziki sasa, likizo itumie vizuri kwa kuwa na muda zaidi wa familia, mazoezi kwa sana maana ni mwendo wa kula na kunywa tu na siku mbili hizi nakaona kakitambi kananijongea kiasi kwamba kujichungulia hadi nijiinamishe nyuzi 45. Likizo njema Kapuku mwenzangu shululu , Tumosa , Transcend , SHIMBA YA BUYENZE , BlessedHope , Shunie , makaveli10 , Lyon Lee , Sakayo , Nyagei , Gentries , dumejeuri , Mndali ndanyelakakomu , mzeewakungoa , moudgulf , husna muba , Werrason , Mussolin5 , Bitoz , Jimena , Mkushi wa kusi , na wewe ambaye hujaenda likizo


Asante Obe ,Ubarikiwe Likizo njema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom