Makapuku Forum

Makapuku Forum

Isaya 62:6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya


ULINZI WA MUNGU BABA WATUZINGIRA..TUSHUKURU,USIKU MWEMA WAPENDWA DAMU TAKATIFU YA YESU ITUFUNIKE
 
Muziki: Chana Shati, Likizo Inaanza

...u khali gani Kapuku mwenzangu, ninajiaminisha uko sawa sana na umekuwa na wakati mzuri siku ya leo. Upande wangu leo ni kama ilivyokuwa jana na juzi, niko likizo na rasmi kabisa nimeanza kuhesabu leo kama siku yangu ya kwanza ya likizo. Ndo maana sikuonekana wikend maana tulikuwa na party ya kufunga mwaka ambao haujaisha. Yeah, mapumziko maana kumtumikia baniani mwaka mzima si mchezo na hasa ukizingatia kuwa kwa sisi watu wa hand to mouth paycheck tunajua kabisa December ndo tunagundua tunalipwa kidogo sasa.
Eeeh, kuna miezi miwili ya mwaka huwa tunajikuta tunasema matajiri zetu wanatulipa kidogo, June na December na ikifika mwezi wa 12 ndo akili zinakaa sawa kujua kwamba malipo tunayopewa ni kidogo, yaani ...the employer is pretending to pay us and you know what we like to do, we pretend to work. Jino kwa jino, jifanye unanilipa nami najifanya kufanya kazi. Sio kwa waajiriwa tu, hata ndani kama gia haziingia kila mmoja anafake kuanzia chumbani hadi sebuleni hii yote ni kuwa sikukuu na bills zimependana against us.
Muziki sasa, pamoja na yote, lakini December ni mwezi mtamu sana, ni mwezi wa kula na kuliwa, kulala na kulaliwa na ni wmezi kama mwaka jana ulipata mapacha basi unajitahidi kufanya kwa tahadhairi ili mapacha wasitokee tena, so unafanya kwa tahadhari, ukijiona unataka kufikia mshindo unasubiri aanze kwanza yeye. Najua unajua nachosema, likizo hii chana shati vaa vest, kuvaa kiprofesheno nyumbani ni kuchafua hewa ndani ya nyumba


Coupe bibamba, wenda sukuma, coupe bibamba eeh

Koma tuta pel, zhumapel, kupekupe bibamba, sema nayo, zinaboyi abibi na malembe..


Umenikumbusha mbali sana mkuu..
 
Amen ubarikiwe..nipo msibani kuna kijana polisi kagongwa na gari juzi ..tunamsindikiza,atapumzishwa huko Arusha ..naamini utamfahamu...hapo Kigamboni kituo cha polisi so sad..apumzike kwa Amani.

Oh! Pole sana, sijasikia hilo yawezekana ni kwa kuwa nimeanza likizo na nakaa mbali na simu muda mwingi. Mwendazake apate mapumziko mazuri (RIP, note, mwendazake=marehemu)
 
Utasikia tu hapo veterans na hakika utamfahamu..apumzike kwa amani...

Habari ya likizo..unapumzikia wapi?Mungu akubariki


...yeah, nitamsikiza mdau wangu hapo bwana Nshimbi atanipa A-Z, huu msimu wa ajali tuombeane uzima tu.
Likizo nimekuja huku Nachingwea then narudi mjini, yaani likizo nimekuja na sukari kilo saba zikiisha tu naamini likizo itakuwa imeisha.

Mmmh, ila nitawaachia kilo nyingine ili wasione sukari imeisha nami naondoka
 
Muziki: Watambue, Uwachunge

...likizo inaendelea, yaani sijui kama nikianza kukuambia kapuku mwenzangu nitamaliza. Hii likizo ni tamu sana maana niko huku kijijini, nimekumbuka mengi sana, mengi mazuri na machache yananyong'oza lakini yote kheri tu, historia inatukumbusha, kututia moyo na kusahihisha pale tunapokosea. Likizo hii tunazunguka na family yangu na juzi nimempeleka pale niliposoma shule ya msingi, kashangaa kuona ile ringi la tairi kutumika kama kengele.

Japo niko likizo lakini naona kama nimechukua kazi ya walimu wanaomfundisha huyu ambaye jina la pili ni la kwangu, maswali kibao na kama kawaida ya sisi wahenga, hakuna ambaye alikuwaga wa mwisho. Basi ninafurahi kufanya hivi na ndiyo nashare nawe leo. Kuna sheria hazifuatiliwi kivile hapa kwetu na hasa umri wa kunywa pombe, kisheria ni miaka 18 lakini unakutana kidume kinagonga vyombo na kiko under 16, wazazi, walezi ni jukumu letu kuhakikisha mtoto hakutani na pombe hata kama wewe unaiona tamu kiasi gani. Msimu huu wa likizo tuwafundishe wanaotutazama tuwaambie kuhusu Ngorongoro crater, je unaweza kupata mraba kwenye duara?

Muziki sasa, likizo lazima iwe na mafanikio na si kukaa tu bila kufanya lolote, ni wakati wa kuangalia matokeo ya wanaokuhusu na kuwaelekeza nini wafanye kuanza mwaka mwingine kwa mafanikio, kumbuka kujipanga mwenyewe maana kuna maana gani kuhuburi usiyoyaishi!!!

 
...yeah, nitamsikiza mdau wangu hapo bwana Nshimbi atanipa A-Z, huu msimu wa ajali tuombeane uzima tu.
Likizo nimekuja huku Nachingwea then narudi mjini, yaani likizo nimekuja na sukari kilo saba zikiisha tu naamini likizo itakuwa imeisha.

Mmmh, ila nitawaachia kilo nyingine ili wasione sukari imeisha nami naondoka
Itapendeza
 
Muziki: Watambue, Uwachunge

...likizo inaendelea, yaani sijui kama nikianza kukuambia kapuku mwenzangu nitamaliza. Hii likizo ni tamu sana maana niko huku kijijini, nimekumbuka mengi sana, mengi mazuri na machache yananyong'oza lakini yote kheri tu, historia inatukumbusha, kututia moyo na kusahihisha pale tunapokosea. Likizo hii tunazunguka na family yangu na juzi nimempeleka pale niliposoma shule ya msingi, kashangaa kuona ile ringi la tairi kutumika kama kengele.

Japo niko likizo lakini naona kama nimechukua kazi ya walimu wanaomfundisha huyu ambaye jina la pili ni la kwangu, maswali kibao na kama kawaida ya sisi wahenga, hakuna ambaye alikuwaga wa mwisho. Basi ninafurahi kufanya hivi na ndiyo nashare nawe leo. Kuna sheria hazifuatiliwi kivile hapa kwetu na hasa umri wa kunywa pombe, kisheria ni miaka 18 lakini unakutana kidume kinagonga vyombo na kiko under 16, wazazi, walezi ni jukumu letu kuhakikisha mtoto hakutani na pombe hata kama wewe unaiona tamu kiasi gani. Msimu huu wa likizo tuwafundishe wanaotutazama tuwaambie kuhusu Ngorongoro crater, je unaweza kupata mraba kwenye duara?

Muziki sasa, likizo lazima iwe na mafanikio na si kukaa tu bila kufanya lolote, ni wakati wa kuangalia matokeo ya wanaokuhusu na kuwaelekeza nini wafanye kuanza mwaka mwingine kwa mafanikio, kumbuka kujipanga mwenyewe maana kuna maana gani kuhuburi usiyoyaishi!!!


Asante Obe,msalimie huyo anaetumia jina lako la pili..na Mungu awabariki katika likizo yenu msafiri salama,mrudi salama sukari acha angalau kg mbili ....stay Blessed
 
Muziki: Watambue, Uwachunge

...likizo inaendelea, yaani sijui kama nikianza kukuambia kapuku mwenzangu nitamaliza. Hii likizo ni tamu sana maana niko huku kijijini, nimekumbuka mengi sana, mengi mazuri na machache yananyong'oza lakini yote kheri tu, historia inatukumbusha, kututia moyo na kusahihisha pale tunapokosea. Likizo hii tunazunguka na family yangu na juzi nimempeleka pale niliposoma shule ya msingi, kashangaa kuona ile ringi la tairi kutumika kama kengele.

Japo niko likizo lakini naona kama nimechukua kazi ya walimu wanaomfundisha huyu ambaye jina la pili ni la kwangu, maswali kibao na kama kawaida ya sisi wahenga, hakuna ambaye alikuwaga wa mwisho. Basi ninafurahi kufanya hivi na ndiyo nashare nawe leo. Kuna sheria hazifuatiliwi kivile hapa kwetu na hasa umri wa kunywa pombe, kisheria ni miaka 18 lakini unakutana kidume kinagonga vyombo na kiko under 16, wazazi, walezi ni jukumu letu kuhakikisha mtoto hakutani na pombe hata kama wewe unaiona tamu kiasi gani. Msimu huu wa likizo tuwafundishe wanaotutazama tuwaambie kuhusu Ngorongoro crater, je unaweza kupata mraba kwenye duara?

Muziki sasa, likizo lazima iwe na mafanikio na si kukaa tu bila kufanya lolote, ni wakati wa kuangalia matokeo ya wanaokuhusu na kuwaelekeza nini wafanye kuanza mwaka mwingine kwa mafanikio, kumbuka kujipanga mwenyewe maana kuna maana gani kuhuburi usiyoyaishi!!!

Wooooooozaaaa mambo yangu haya watoto wa mjini kila jumamosi tunakutana kiwanja chetu cha nyumbanii binamu huyo aliyechukua jina lako la pili mpendwa wako husna muba eenh
 
Asante Obe,msalimie huyo anaetumia jina lako la pili..na Mungu awabariki katika likizo yenu msafiri salama,mrudi salama sukari acha angalau kg mbili ....stay Blessed

...zimemfikia tayari na keshamaliza kula kitambo sasa tunaangalia tu katuni, wageni tunamiliki tv ya wenyeji na bibi hana noma inabidi tu azizoee katuni
 
Ameen mama mama hiyo salaam ya kumsalimia anayetumia jina la binamu umetoa kwa roho moja eenh

...huchelewi kuniharibia kwa BH, ujue BH ndo roho yangu mimi, haya maandishi mwingine hayamuhusu, ni mawazo yangu tu.

Huyu anayetumia jina langu la pili ni mtoto majirani huwa wananisingizia kuwa ni wangu, nami ninamuogopa Mungu sijamkataa ninaishi naye
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom