Muziki: Chana Shati, Likizo Inaanza
...u khali gani Kapuku mwenzangu, ninajiaminisha uko sawa sana na umekuwa na wakati mzuri siku ya leo. Upande wangu leo ni kama ilivyokuwa jana na juzi, niko likizo na rasmi kabisa nimeanza kuhesabu leo kama siku yangu ya kwanza ya likizo. Ndo maana sikuonekana wikend maana tulikuwa na party ya kufunga mwaka ambao haujaisha. Yeah, mapumziko maana kumtumikia baniani mwaka mzima si mchezo na hasa ukizingatia kuwa kwa sisi watu wa hand to mouth paycheck tunajua kabisa December ndo tunagundua tunalipwa kidogo sasa.
Eeeh, kuna miezi miwili ya mwaka huwa tunajikuta tunasema matajiri zetu wanatulipa kidogo, June na December na ikifika mwezi wa 12 ndo akili zinakaa sawa kujua kwamba malipo tunayopewa ni kidogo, yaani ...the employer is pretending to pay us and you know what we like to do, we pretend to work. Jino kwa jino, jifanye unanilipa nami najifanya kufanya kazi. Sio kwa waajiriwa tu, hata ndani kama gia haziingia kila mmoja anafake kuanzia chumbani hadi sebuleni hii yote ni kuwa sikukuu na bills zimependana against us.
Muziki sasa, pamoja na yote, lakini December ni mwezi mtamu sana, ni mwezi wa kula na kuliwa, kulala na kulaliwa na ni wmezi kama mwaka jana ulipata mapacha basi unajitahidi kufanya kwa tahadhairi ili mapacha wasitokee tena, so unafanya kwa tahadhari, ukijiona unataka kufikia mshindo unasubiri aanze kwanza yeye. Najua unajua nachosema, likizo hii chana shati vaa vest, kuvaa kiprofesheno nyumbani ni kuchafua hewa ndani ya nyumba