Muziki: Jumamosi ya Uzalendo
...hii si sawa na Jumamosi nyingine, fyi. Hii imekaa kiuzalendo zaidi na ndiyo maana wote tunakaa chini kutafakari kama taifa tunataka kwenda wapi maaana tulikotoka tunakujua. Kibinafsi ukitaka kwenda unapotaka sio shida, kuna vitu lazima uvifanye, mfano kama mwanafunzi, jitahidi kusaka maarifa ili ufaulu, mfanyakazi fanya kazi kwa bidii, hii inajulikana. Familia, mnakaa chini mnajipanga na kuchagua. Ila kama taifa sasa, hapa ndo tunaweka zile siasa zetu uchwara na kuwa na imani moja ya kujenga taifa na si wengine kujidai ni wazalendo zaidi ya wengine. tiiza wajibu wako
Muziki sasa, Babu Seya Na Papii Kocha wamepewa msamaha wa rais wanarudi uraiani, ni faida za kuwa rais, unafanya kile kinachokupendeza ikiwa tu kinaruhusiwa kikatiba na sheria. Wanarudi na kukuta mabadiliko mengi na mengine ni yale yale.
Kwako
Tumosa (umebadili avatar-cute as always) na our very own
makaveli10 papa mopao muzee ya tukutuku na makapuku wote nawatakia mwendelezo mzuri wa wikend. Upendo na uungwana ndo uwe imani yetu