MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 31
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
Sasa wakati huo sheby akiwa kasimama na zaituni... Na zai alikuwa akilia mana alikuwa awe mume wake lakini kwa tamaa alijikuta anamsahau na kutokumbuka msaada aliompa...
"binafsi mimi nakutakia maisha mema na saidi wako... Ila kuwa makini sana, kama saidi nae utamchezea utakuwa kama dada yako Zainabu"
Aliongea kijana sheby kisha huyoo akaondoka zake.. Hata lile swala la kwanini aliandika ujumbe hakutaka kumuuliza, mana zaituni alikuwa akilia sana.. Na lawama zote alimshakizia shadi, mana ndio aliomshawishi kuingia kwenye ujinga na kumsahau sheby...... Zaituni aliingia katika gari huku akifuta machozi ya uchungu.... Sheby yeye alichukuwa toyo impeleke nyumbani mana walikuja umbali wa kilometa tatu hivi... Sheby alikuwa akiwahi kule nyumbani ili kuiwahi sherehe japo hapendi kuwepo kwenye sherehe hio...
Baada ya dakika kadhaa sheby anakaribia nyumbani kwake, alishangaa kuona wale omba omba wanatolewa nje ya geti tena walikiwa wakifukuzwa haswa.... Sheby alitoa macho kwa kitendo kile kilivyokuwa kikiendelea pale getini kwake.. Kijana alishuka kwenye pikipiki na kwenda mpaka getini kwake, na kukuta baadhi ya vipofu waliokuwa wakisukumwa na wengine wasioweza kutembea walitolewa kama maji taka.....
"heee hawa nao walialikwa na nani hawa laana kum"
ENDELEA.........
Kijana akiwa katika toyo kwa mbaali aliweza kushuhudia wale watu ambao ni omba omba na wana matatizo yao tofauti tofauti katika miili yao,.. Kutokana na huruma za kijana huyo watu wale waliweza kuelekezwa sehemu ya kula baada ya wao kudai wana njaa kwa wakati huo, kijana huyo aliwaamuru waende nyumbani kwake kuna sherehe ya mkewe kwa kukuza ujauzito wake, watu wale walikubaliana na kauli ya kijana huyo na wao kufunga safari na pia aliwaahidi kuwa naye yupo nyuma yao, lakini kwa bahati mbaya alikutana na zai, mchumba wake mtarajiwa.. Walichukuana na zai na kuwaacha wale watu wakienda wenyewe kule... Sasa wakati anarudi akiwa katika usafiri wa pikipiki alishangaa kuona wale watu walikuwa wakifukuzwa tena wengine walikuwa wakipigwa virungu na mlinzi,... Sheby alitamani kuruka kutoka juu ya pikipiki lakini hakuweza mpaka pale aliposhushwa kwa utaratibu mzuri..
Baada ya kushuka kwenye pikipiki alikwenda mpaka getini kwake, na kukuta baadhi ya vipofu waliokuwa wakisukumwa na wengine wasioweza kutembea walitolewa kama maji taka.....
"heee hawa nao walialikwa na nani hawa laana kum"
Ilitoka sauti kwa ndani ya nyumba ya sheby, na wakati huo sheby alitamani sana kuiona hio sura ya huyo mtu alio ongea ujinga huo...
"we, ebu acha kupiga hawa watu"
Aliongea sheby huku akifungua geti ili amwone yule aliosema hawa watu ni laana kum,..... Laaa Haulaaa sheby alishindwa kusema lolote baada ya kukuta alioongea hivyo alikuwa ni mama mkwe wake, yaani mama yake na mwai
"shkamoo mama"
"Marahaba,... Mbona huku ndani huonekani baba"
Aliongea mama mkwe huku akimtaka aachane na hawa watu aingie ndani,..
"nipo mama na nakuja sasa hivi"
Ndani akina rose na mary wapo wote katika sherehe ya rafiki yao, na hawajui kama sheby huyo boss wao ndio mwenye huyo mke.... Lakini huezi amini kutolewa kwa vipofu wale kulimfanya kijana huyo aache kuingia ndani na kuanza kudili na wale watu
"baba achana na hao watu watakusumbua tu"
"mama... Mimi ni mtu wa watu, naomba nikawapatie chakula hotelini, mana ninyi mko tayari kumwaga chalula kuliko kuwapa watu hawa"
"sio hivyo baba... Lakini si unajua waalikwa wenu walivyo wa heshma, hivyo tusingeweza kuwaruhusu hawa waingie"
Aliongea mama huyo na kumfanya sheby kutomsikiliza kwa lolote,
"Twendeni ndugu zangu, wamekataa na chakula chao"
Sheby aliondoka na watu wake mpaka kwenye hoteli moja hivi
"he he he he wale wanaenda wapi wale wazuieni"
Aliongea mmoja kati ya wahudumu waliopo katika hoteli hio,...
"weeeeee, weka rungu lako pembeni we mshenzi nini... Ivi nyie, hawa sio binaadamu hawa, hawa ni mambwa kwani???... Nawauliza hawa sio watuuuuuuuu"
Watu wote kimya,...
"lakini ndugu"
"hakuna cha ndugu hapa.... Kwa mfano ni wewe afu ndio unatengwa kiasi hiki utajiskia vipi, na hapo ulipo tu ni muhudumu je ungekuwa tajiri ungelikuwaje wewe... Mimi nalipia bili yao yote waache wale wanavyotaka... Wape makuku kuku kila kitu wanachotaka nitalipa mimi"
Watu wote kimya, wahudumu walianza kuchangamka na kuweka viti vizuri,.. Walikaa sehemu moja wao na kijana sheby,.. Kila mteja akija anashangaa jamaa kakaa na hawa omba omba wenye matatizo tofauti tofauti katika miili yao,.. Wengine walemavu wa miguu wengine hawana macho ni vipofu wengine hawana hata vidole, yaani ilikuwa ni huruma iliojitosheleza kiukwe, lakini tunashangaa sana baadhi ya watu kutowajali watu kama hawa,.... Ukumbuke leo wewe ni mzima lakini huijui kesho yako itakuwaje, mpende binadamu mwenzio, kama huna huna tu na Mwenyezi Mungu anajua huna... Lakini sio kuwachukia na kuwaona kituko,... KABLA HUJAFA HUJAUMBIKA sasa kwanini leo umuone kilema au kipofu kama taka taka kwako.......
Hoteli hio ilikuwa na ukimya wa halo ya juu sana mana kila tajiri akitaka kuingia anasita kutokana na watu waliokuwa wanakula pale,... Walichukuwa lisaa lizima mana kuna wengine walikuwa wanakula kwa hisia, hususan vipofu,... Baada ya lisaa limoja kupita walimaliza na kila mmoja alishiba haswa kwa siku hio
"ndio, hata siku moja moja na wao waonje radha ya maisha, sio wasikie harufu tu"
Aliongea sheby na kuwafanya baadhi ya watu wacheke kwa maneno yake
"haya we muhudumu nadaiwa shilingi ngapi"
"yule kala kuku mzima na yule kala ku... "
"ah ah ah... Sikusema utaje walichokula, waote najua wamekula makuku mazima mazima na misoseji kibao... Mimi nataka gharama tu achana na vitu walivyokula"
"ni laki moja na nusu"
"enheeee hapo sawa sasa... Pesa kidogo tu unataka kuliiia"
Sheby alitoa waleti na kulipia bili ya chakula cha watu hao wapatao 20, waliokuwa wakiomba sehemu moja mana kila mmoja na riziki yake....
Walitoka pale taaratibu mpaka pale kwenye eneo lao wanaloombea pesa
"jamani ndugu zangu si mumeshima au kuna mtu ana njaa turudi tena"
"hapana baba, tunakushukuru"
Maskini ya mungu sheby aliwaahidi kuwapa pesa, baada ya kula, lakini wenyewe walisahau kutokana na hisani ya kupata mlo mmoja tu uliowafanya kujijua kuwa na wao wana uwezo wa kula makuku kama wao
"sasa nataka niwapati hata elfu kumi kumi kila mmoja, mana bize yangu mimi aipiti hapa kila siku"
Aliongea hivyo kijana sheby huku akitoa noti ya elfu kumi na kumkabidhi kila mmoja note yake,.. Ili gharimu kiasi cha laki mbili lakini sheby hajali kutoa mana nao ni binaadamu.... Laki mbili jumlisha laki moja na nusu... Ni upendo wa hali ya juu, kijana sheby anataka kuvunja ule usemi usemao TAJIRI NI VIGUMU KUINGIA KWENYE TUNDU LA SINDANO neno hilo likiwa na maana kubwa sana katika dunia hiiiiii.....
"jamani ndugu zangu tutaonana siku nyingine"
Aliongea kijana sheby huku akipiga hatua na kuondoka zake....
Wakati huo huku nyumbani kwake sherehe imekwisha na tayari watu walikuwa wakiondoka,... Wale watu wa jirani ndio waliobakia kwa ajili ya kufanya fanya usafi, wakati huo akina rose ndio wanapanda gari la mwax. X i, na mwai ndio aliokuwa dereva wa gari hio, anawapeleka rafiki zake,..... Sasa wakiwa barabarani walipishana na sheby bila kumjua, lakini mwai yeye kamuona mume wake...
"baba tifa huyo apo"
Aliwaonyesha rafiki zake lakini hawajaona kwasabu alionyesha gari ikiwa ndio inampita,..
"yupo wapi"
"aaahhhh keshapita.... But msijali mtakuja kumuona tu"
Aliongea mwai kitendo kilichowashangaza akina rose,...
"lakini dada mwai, now nakuona kama umepunguza ukali juu yake"
Aliuliza mary huku wakitamani jibu toka kwa mwai
"ni kweli mary... Yaani toka siku ile nimelala nae Kimapenzi,.. Kiukweli nilianza kumueshim kidogo kutoka pale, na nilitamani nilale nae kila siku lakini sasa hataki"
"si utimie ile njia ya mganga"
"kule kwa mganga nilikwenda, lakini akasema nilikosea mana nilitaka dawa ya siku moja.. Nami sikutaka kuendelea na sheby kwasababu simpendi,.. Lakini utamu wake, rose we ni mkubwa mwenzangu, kiukwe kale katoto ni katamu kwenye mapenzi... Sijapata picha.. Na licha ya hivyo mpaka sasa nafsi inanisuta niitoe hii mimba mana nitakuwa namuonea mume wangu"
Akina rose walishangaa sana kuskia kauli ya mwai,...
"kwahio unataka kusema kwa sasa unamjali"
"nilikuwa staki kupika lakini sasa hivi napika nyumbani na yeye pia anakula japo kishingo upande tu"
"kambembeleze mganga"
"rose, Mganga kasema mizimu imegoma mana siku ile nilitaka dawa ya siku moja tu, tena nikaulizwa mara mbili mbili unataka dawa ya siku ngapi nikakazania dawa ya siku moja mana sikua nataka kufanya mapenzi na sheby wa siku zote, ila kwa utamu nilioupata... Waaalahi vile natamani hata leo nikirudi nimpe anifurahi mie mkewe"
"Heheheeeeeeeee haaaalooooo.... Eti leo ndio. Unajua umuhimu wa mume.. Ulimchezea mwenyewe"
"lakini sio mimi tu rose.. Hata yeye hakuwa akinipenda na hata mimi sikuwa nikimpenda... Na hata hii mimba natamani niitoe eti"
"we... Weee... We... Mwai usijaribu huo ujinga, hii mimba imeshakuwa kubwa, ukiitoa tu utakufa wewe,.. Jikaze uzae mtoto mpe baba yake wa kweli, we rudi kwa mumeo"
"heeeeeeeee... Na familia yake itanichukulia vipi mtoto sio wao"
"hapo kazi unayo, na hio ndio kero ya kuoana bila kupendana"
Rose aliongea hivyo huku wakikaribia kufika nyumbani,....
Sasa huku nyumbani sheby anarudi anakuta watu wamesha sambaratika kila mtu kwao waliobakia ni wachache tu,...
Sheby kaingia na kumkuta mlinzi pale ndani
"ivi nani alikupa ruksa ya kuwatimua wale watu"
"ni boss ndio kasema niwatoe, na wakikataa niwapige virungu"
"nawe ukawa unawatandika haswa si ndio eee"
"ni amli kutoka kwa boss"
"Oooohhhh sawa, ni kutoka kwa boss eee"
Sheby aliachana na mlinzi kisha akaingia zake ndani, wala hakutaka kujua watu waliobaki katika jukwaa ambao ni watu wa karibu tu,..
"baba mkwe"
Aliita mama yake mwai na kumfanya sheby atoke,
"naam mama"
"wale watu wapo wapi,... Chakula kimebaki kinataka kumwagwa... Waite waje wale.. Chakula Kile pale chini kinadorola na nzi t