MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 28
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +25571441948
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
Kwa bahati mbaya sheby alipopiga aliambiwa simu inatumika,... Sasa shadi alikuwa akiongea na zaituni
"eee shost mambo"
"safi shadi mzima wewe"
"salama tu... Nahisi upo nyumbani ee"
"yes nipo hapa naangalia tv huku nikipata juice baridiii"
Zai alikuwa akizidi kumringishia mwenzie na maisha mazuri, yaani sasa kule kwa shadi kumringishia mwenzie mavazi na pesa, sasa kumemgeukia yeye....
"ok sasa skia zai... Ivi yule kijana aliokuuliza kuhusu mimi vipi? Ivi bado anaendelea kukusumbua tu"
"yaani shadi umeikosa bahati wewe,.. Yule boy alinipigia jana, ila nikamwambia hutaki"
"ooohhh shit, sorry naomba namba yake nimcheki"
"ati nini"
Zai alishtuka kwa kuskia shadi kakubali kuwa na huyo kijana wanaomsemea
"nipe namba zake basi"
"ok poa ngoja nikutumie"
Zaituni aliitafuta namba ya huyo jamaa aliompenda shadi na shadi kukataa,.. Shadi alitumiwa namba ya huyo kijana na kuisevu kabisa,... Sasa akawa anasita kupiga, mana mwanamke kumtongoza mwanaume ni ngumu, sasa wakati huo huku kwa sheby nae akarudia tena kupiga, mana mwanzo aliambiwa kiwa namba aliopiga ilikuwa ikitumika,.. Wakati huo huku kwa shadi nae kabonyeza kitufe cha kupigia kana kwamba kaamua kumpigia huyo boy amwambie keshamkubalia.... Sasa hapo sijui kachelewa au kawahi, mana ikiingia simu ya sheby tu basi kapata bahati, lakini kama kawahi basi simu ya sheby hawezi kuipata tena... Sasa kila mmoja akawa anasikilizia kama itaita au vipi
ENDELEA..........
Katika maisha wahenga walisema kuwa kuna mafungu saba ya bahati kwa binaadam, na kila fungu huja kwa wakati maalumu na kwa miaka tofauti tofauti, ukichezea fungu moja basi jua yapo mengine yaliyobaki kwa ajili yako, hivyo usikate tamaa katika maisha,... Kijana sheby ni kijana ambae wengi tunamjua kuwa ana mke, lakini mke alienae pia tunamjua, hamtimizii haki za ndoa ugomvi haushi visa ndani ya nyumba haviishi, binafsi yake yeye alitaka kuoa kimya kimya bila hata ya wazazi wake kujua kuwa kijana wao kaoa, na ndio mana siku zote anakuwa mstari wa mbele kutafuta mke bora kwa kuibadiri hali yake kuwa hali ya watu wengine ili apate mke atakaeridhika na maisha anayoishi kijana sheby, lakini kila akijitahidi kutafuta hapati mke bora, mchumba aliomgharamikia macho leo kamuona hana maana kisa kapata mtu mwenye maana kuliko sheby,..
Lakini kijana sheby hakukata tamaa, bado anaamini riziki ni mafungu saba huenda hilo lilikuwa sio fungu lake,... Zaituni ana rafiki aitwae shadi na ndio aliopewa kazi na sheby kuwa amdanganye kama ataweza kudanganyika ili ajue kuwa anampenda au laa,.. Mschana huyo aitwaye shadi nae alikuwa ni mtu wa dini hivyo kazi aliopewa na kijana sheby ilikuwa ni ngumu kwake kwasababu dini yake haikuruhusu kuvaa nguo fupi.. Ila ilimlazimu kufanya hivyo kwasababu nae alishaanza kumpesha sheby, hivyo hata kule kumkuadia zaituni, alikuwa akifanya kqa juhudi zote ili yeye awe na sheby.... Lakini sasa kosa la sheby alilofanya ni kumsahau shadi baada ya kujua zai keshaharibika na haambiliki tena... Sheby alikuwa hata simu kwa shadi hapigi mana hana kazi nae tena na hata shadi kama unavyojua maisha yake ni ya chini sana, na wakati huo zai keshahamia mjengoni tayari, kamwacha mwenzake kwenye nyumba za udongo, na sheby nae akasusa kuja uswahilini kwasababu hakukua na mtu wa kumleta huko, na alikua hajui kama shadi nae kampenda,.. Maskini shadi anakula msoto na kujikuta anairudia kazi yake ya kushona nguo, mana aliacha kwasababu alikuwa akipewa pesa na sheby... Lakini sasa kumbe kipindi wakati shadi anamtembeza mwenzie kwa wanaume yeye alikuwa pembeni na hataki tabia hio ila alifanya kwa kutumwa, katika moja ya wanaume walikutana na zai mana zai si keshakuwa mjanja wa mjini baada ya kujua utamu wa pesa,... Kijana huyo alimuuliza zai kuhusu rafiki yake ambae ni shadi,... Zai aliona shadi ni mtu wa mambo haya hivyo hawezi kukataa... Shadi alipoambiwa kuwa kuna mwanaume kampenda, shadi alikataa katu katu, mpaka zai akashangaa mtu aliomfundisha kujua wanaume leo anakataa mwanaume, ila hakutaka kujua sana wakaachana ila yule kijana alikuwa bado anamsumbua zai kuhusu shadi..
Sasa leo shadi kaamua kumtafuta yule kijana mwenyewe mana hali ya maisha kwake anahisi imekuwa ngumu,... Lakini sasa huku shadi anawaza kumtafuta huyo kijana, na huku sheby anawaza kumtafuta shadi,... Na hapo ndipo simu zilipoanza kupigwa hivyo kila mmoja alikuwa akisikilizia kama itaita au vipi,
"haloo Jackson mambo"
Ilikuwa ni sauti ya shadi ikimsalimia Jackson ambae ndio kijana alimpenda sana kutoka moyoni,...
"safi tu nani mwenzangu"
"mmmh shadi hapa naongea"
"aaahhhh rafiki wa zai si ndio eee"
"ndio"
"oooohhh mambo vip mrembo"
"hahahahaha safi tu"
"mbona wacheka kuna kipya"
"i think kuna kipya"
"basi tukutane mjini au vipi shadi"
Wakati huo huku kwa sheby simu inamwambia kuwa namba aliopiga inatumika hivyo asubiri kidogo au akate apige tena... Sheby kwa hasira aliipigiza simu chini, alichoambulia ni laini tu, alichukuwa laini yake na kuondoka.... Sasa huki kwa shadi mambo yameiva
"sawa nikukute wapi sjui"
"aahhhh ebu chagua hoteli kubwa unayoipenda"
"Novo hotel, panatufaa kiukweli"
"eti eee"
"yes"
"basi njoo pale nami najiandaa kuja"
"sawaaa"
Jackson alifurahi sana mpaka akampigia simu zaituni na kumshukuru kwa kumpata shadi,... Shadi alikuwa ni mschana mzuri mwenye sifa kila kona ya mwili wake, yaani yeye na zaituni wametofautiana rangi tu lakini uzuri sheby yaani wapo vizuri kiukweli... Sheby alijikuta anakosa kila kitu... Mawazo kwake ndio chakula, mana hayaishi kichwani mwake...
HAPO NDIO MWISHO WA KUMBUKUMBU KABLA YA MIEZI MIWILI ILIYOPITA.... NA KUMBUKUMBU HIO ILIANZA PALE ZAITUNI NA SHADI WALIPOSHIKA KWA KUPIGANA KISA KUKUADIANA
"niachie sasa si nimeshakwambia ukweli"
Aliongea shadi, mana zaituni alikuwa bado kamshika shadi...
"lakini shadi ulichokifanya kwangu sio kizuri, umenikosea sana"
"sikiliza zaituni... Unajua hata mimi nilikuwa nampenda sana sheby vile vile na umaskini wake, lakini hata mimi nimemkosa mana alishawahi kuniona nikiwa na Jackson"
"weeeee wacha uongo shadi"
"kweli, tena alinikuta sehemu za starehe tu"
"mmmhhh basi ndio hivyo tumeshamkosa wote... "
"lakini zai we mwongo kusema sheby ni tajiri"
"kwani we ulivyokutana nae alikuwa katika hali gani"
"alikuwa na mkokoteni wake"
"ndio hivyo sasa, sheby sio muuza viazi wala nini, bali alikuwa anatafuta mke"
"lakini wewe ndio roho itakuuma mana alikuwa mchumba wako yule"
Zaituni alikasirika kuskia maneno hayo
"shadi naomba tuepushe shari mana tutapigana hapa nikuuwe bure"
"umuuwe nani bwana we nenda kwako bwana"
"sawa... Lakini dhambi ulizonazo za kivunja uchumba wa watu, yaani utachomwa mpaka basi wewe"
"nyoooo, utajiju bibie si umalaya wako mwenyewe"
"sawaaaa"
Wakati huo ni mida ya saa 12 kasoro sheby akiwa ofisini anasubiria gari ije aondoke, mana gari aliichukuwa saidi na kusema anakwenda kutambulishwa kwa wazazi wa mpenzi wake,.. Sheby akiwa kakaa zake ofisini kwake, tena alikuwa peke yake mana wafanyakazi wote walishaondoka mida ya saa 11 kamili za jioni,.. Hivyo yeye alikuwepo wakati wa kusubiria gari
"piiiiiiii"
Ilikuwa ni honi ya gari iliosikika nje ya geti la ofisini
Sheby alichukuwa kibegi chake na kutoka nje mana gari hio iliopiga honi ilikuwa ni gari yake,...
"aaahhhh sorry boss Nilikawia kidogo"
"hakuna shida,... Twende"
Basi saidi aligeuza gari kisha haoo wakaondoka zao
Tukija huku kwa wazazi wa mwai waliokuwa na shamra shamra za sherehe juu ya kupata mimba kwa mtoto wao,.. Mana sasa mimba ya mwai yapata miezi miwili sasa na kila mtu anajua, lakini ukweli wa hio mimba sisi tunaijua sio ya sheby, bali ni mimba ya mpenzi wake mwai lakini kabebeshwa sheby kuwa ni yake,... Na shamra shamra hizo ina maana sherehe ni kesho, sheby kufika nyumbani alikuta nyumba imepambwa pambwa, na anajua fika kuna sherehe ya kupata mimba salama tena akiwa ndani ya ndoa yake, sheby siku zote yeye sio mtu wa raha kama ilivyo katika simulizi zingine ila hiii kachapika haswa...
"mambo"
Mwai alimsalimia mume wake kihivyo, lakini sheby hakuiyikia kabisa,.. Sasa huezi amini mwai toka siku ile afanye mapenzi na sheby, kwa sasa kidogo ana heshima kwa sheby yaani yale maujeuri JEURI hakuna tena siku hizi kawa mpole
Sasa hivi sheby ndio kiburi, mana mwanzo kiburi alikuwa ni mwai lakini kwa sasa kiburi ni sheby haitikii wala nini... Sheby alioga kisha akaja zake sebuleni na kufungulia tv ili aangalie taarifa za habari,..
"unawekaje michaneli yako na wakati mi naangalia chereko chereko, Ebu yoa ITV yako niwekee send off zangu niangalie mimi..... Afu kesho hakuna kwenda kazini,... Kesho ni sherehe ya mtoto wetu kufikisha miezi miwili tumboni"
Sheby alimuangalia sana huyu mwanamke na asimpatie jibu.. Sasa sheby kuna CD alikuja nayo kutoka kazini, aliinunua mida ya mchana hivi sasa aliiweka kwenye gari sasa alipofika nyumbani akaitupia mezani
"hiii ni cd gani.. Ya Bongo movie au ni ngumi zako tu"
Mwai aliongea hivyo huku akiichukuwa hio cd na kuifungua kava ili atoe ile cd yenyewe,... Lakini sasa ile anafungua tu, kuna karatasi ilidondoka mezani, kana kwamba ilikuwa ndani ya lile kava....
Sheby nae alishangaa mana aliponunua hio cd alifungua na hakukuwa na karatasi, yeyote sasa nani kaweka hio karatasi.. Lakini sheby hakuwa na wasiwasi sana kana kwamba huenda ni karatasi ya maelezo ya hio cd....
"heeeee cd za siku hizi zina maelezo"
Aliongea mwai huku akiifungua ile karatasi
"mbona una Kiherehere we mwanamke, kwani nimekuletea wewe hio cd
"hata kama, kwani si umeiingiza ndani... Haaaaaaaaaa"
Sasa ghafla mwai anastuka kwa kusoma hio karatasi, hata sheby akapatwa na wasiwasi juu ya karatasi hio....
"ina mana kumbe ulikuwa unatafuta mke mwingine???"
Sheby alishtuka kuskia mwai kasema hivyo,..
Je? Hio karatasi imeandikwa nini?? Na je? Ni nani kaandika huo ujumbe na kuuweka kwenye cd??..... Je? Mwai atafanyeje??