MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 29
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
"unawekaje michaneli yako na wakati mi naangalia chereko chereko, Ebu yoa ITV yako niwekee send off zangu niangalie mimi..... Afu kesho hakuna kwenda kazini,... Kesho ni sherehe ya mtoto wetu kufikisha miezi miwili tumboni"
Sheby alimuangalia sana huyu mwanamke na asimpatie jibu.. Sasa sheby kuna CD alikuja nayo kutoka kazini, aliinunua mida ya mchana hivi sasa aliiweka kwenye gari sasa alipofika nyumbani akaitupia mezani
"hiii ni cd gani.. Ya Bongo movie au ni ngumi zako tu"
Mwai aliongea hivyo huku akiichukuwa hio cd na kuifungua kava ili atoe ile cd yenyewe,... Lakini sasa ile anafungua tu, kuna karatasi ilidondoka mezani, kana kwamba ilikuwa ndani ya lile kava....
Sheby nae alishangaa mana aliponunua hio cd alifungua na hakukuwa na karatasi, yeyote sasa nani kaweka hio karatasi.. Lakini sheby hakuwa na wasiwasi sana kana kwamba huenda ni karatasi ya maelezo ya hio cd....
"heeeee cd za siku hizi zina maelezo"
Aliongea mwai huku akiifungua ile karatasi
"mbona una Kiherehere we mwanamke, kwani nimekuletea wewe hio cd
"hata kama, kwani si umeiingiza ndani... Haaaaaaaaaa"
Sasa ghafla mwai anastuka kwa kusoma hio karatasi, hata sheby akapatwa na wasiwasi juu ya karatasi hio....
"ina mana kumbe ulikuwa unatafuta mke mwingine???"
Sheby alishtuka kuskia mwai kasema hivyo,..
ENDELEA........
Katika maisha unaweza kufanya kitu bila kujua kuwa kinaweza kumuathiri mtu mwingine, kumbuka unapofanya jambo angalia na mbele kutakuja kutokea nini,... Kijana sheby mchana wa leo aliingia katika Library ya kuuza CD ili ile siku ya sherehe ambayo ni kwsho awe ndani tu anaangalia zake muvi, mana hajaipenda na hatamani kuhudhuria,.. Sheby alinunua cd moja iliomvutia sana iitwayo THE BEST WIFE... Aliiweka kwenye gari yake kisha huyo kaelekea kwenye mizunguko yake,... Sasa muda huu ndio anashangaa kumsikia mke wake anasema mambo ya kutafuta mke mwingine,..
"ina mana kumbe ulikuwa unatafuta mke mwingine???"
Sheby alishtuka kuskia mwai kasema hivyo, mana kwake analifanya kama siri na hataki hata wazazi wake wajue kama anatafuta mke mwingine, ili siku akimbwaga mwai aje mwingine,...
"we umeikuta wapi hio karatasi"
"si huku ndani ya cd uliokuja nayo"
"yaani umekosa cha kuniongelesha sasa umeona uandike upumbavu wako afu ujifanye ilikuwa kwenye cd"
Aliongea kijana sheby huku akiwa na hasira mno,
"heeeeeeee ina maana mimi ndio nimeandika hivi"
"hebu lete hio karatasi"
Sheby aliichukua ile karatasi tena kwa kumpokonya mwai,... lakini sasa sheby anazidi kushangaa mbona mwai siku hizi kapunguza ukali, yaani ni tofauti na mwanzoni mwa ndoa yao mana kuna muda sheby anashikwa tai kabisa na kutaka kupigwa, lakini sasa hivi ukali umepungua,... Sasa sheby kuangalia ule muandiko ulioandikwa pale, ni muandiko anaoufahamu kabisaa...
"ina maana yeye ndio kaandika hivi,.. Na nilimpakia lini"
Sheby alikua anajiuliza huyo myu alimpakia lini mana hajawahi kumpakia kwenye gari hio
"zaituni nilimpakia lini mungu wangu, mana huu ni muandiko wake kabisa huuu... Au ni huyo demu wa saidi ndio mwenye muandika kama wa zaituni"
Sheby alizidi kujiuliza sana kimoyomoyo na wakati huo mwai ndio anaondoka kwenda kulala zake mana siku hizi kapunguza ukali na alijua tu huo ujumbe huenda haujui na ndio mana kaacha, na pia mpaka hapo sio tabia yake, kapunguza sana tu.... Sheby alijua kabisa huo ujumbe haukuwa ukimuusu yeye japo hata yeye anatafuta mke mwingine... Ujumbe uliandikwa hivi...
SAWA NASHUKURU KWA KUNIFANYIA HIVYO,... KWANZA SIAMINI KAMA UNA MKE... ILA NISAMEHE SANA MANA HUENDA NIMEKUPOTEZEA MUDA NA PESA ZAKO,... HATA MIMI NILIKUWA NAKUPENDA SANA, ILA TAMAA YA MAISHA... BINAFSI NI KWAMBA TAYARI NIMEKUKOSA,.. LAKINI NAKUOMBEA KWA MUNGU UPATE HUYO MKE WA PILI,... MANA SIAMINI KAMA NINGELIKUJA KUWA MKE WA PILI.... SAMAHANI SANA, NAJUTA KUKUHISI FUKARA.... NAKUOMBEA UPATE MKE MWENYE HESHIMA KULIKO MIMI,.. NA PIA NAOMBA UENDELEE KUUZA VIAZI ILI UPATE MKE BORA... AHSANTE SANA.... NAKUTAKIA BAHATI NJEMA
Sasa sheby ndio kajua sababu ya mke wake kuachana na ujumbe huo ni kwasababu ya pale aliposema, usiache kuuza viazi ili upate mke bora.... Mwai akajua hio sms wala haimuusu mana sheby sio muuza viazi, lakini sasa sheby kajua fika huo ujumbe unamuusu yeye, sema alikuwa anazuga zuga tu... Ila kichwa chake kinatafakari sana, je huyu zai kapanda lini gari yake? Kila akifikiria juu ya zaituni kupanda gari yake hapati picha kabisa.... Sheby aliangalia simu yake haoni, akajua kaiacha chumbani,.. Aliamka na kwenda chumbani,... Alipofika alimkuta mke wake anachati Instagram yupo na laptop yake,.. Sheby kaka kwenye kitanda chake na kumpigia saidi...
"oya saidi vp hali"
"safi boss, vp saa hizi kuna nini tena"
Saidi alipata hofu baada ya kuona simu ya boss mdogo usiku...
"ivi mke ulioenda kutambulishwa kwao anaitwa nani"
"hahahahahaha, mtoto wa Kiislamu mtoto anaitwa zaituni"
Sheby alishtuka lakini hakuonyesha kama kashtuka... Ila akatumia maneno ya kawaida ya kumchombeza saidi ili atume picha ya huyo zaituni
"waapi wewe usikute umeoa kimbaumbau hana hata nyama"
"aaahhhh weweeee, boss ivi mi unanionaje vile... Ngoja nikuonyeshe mtoto,.. Nilimpiga picha akiwa kwenye vazi la kimjini mjini"
Sheby hivyo ndivyo alivyotaka picha itumwe na ni kweli inatumwa... Sheby kwa uchokozi akamchokoza mke wake mana siku izi kapunguza ukali
"vipi umeujua huo ujumbe ni wa nani, mana umeniacha ghafla tu"
"niliposoma tu neno usiache kuuza viazi nikajua sio wewe wala haikuusu hio"
Ghafla simu ya sheby ikaingia meseji, kuangalia alikuwa ni saidi kamtumia picha.... Laaaaa Haulaaaa alikuwa ni zaituni kweli, tena mtoto alivaa tishet kubwaa zile za kike ambayo imefika mpaka mapajani, tena ilikuwa imembana, hivyo umbo lake lote unaliona kwa ramani tu ya ile tishet mana ilimchora haswa,... Sheby alishikwa na hasira sana, yaani kumbe saidi ndio katongoza demu ambaye sheby alimtazamia kuwa mke, ila kwa mapepe ya mwanamke huyo ikashindikana,...
BAADA YA USIKU HUO KUPITA
Na leo ni asubuhi sheby akiwa anajiandaa kwenda kazini
"hee hee hee, unakwenda wapi"
Aliongea mwai huku akiwa kasimama mlangoni,...
"ina maana nikae nyumbani kama wewe si ndio eee"
"ina maana hii sherehe ya mtoto wetu haikuusu"
"mtoto wenu na nani"
"jamani, kwaio mimi nimejitia mimba mwenyewe si ndio"
"jiulize mwenyewe usiniulize mimi"
"sasa hutoki hapa, na ninapiga simu kwa baba mkwe"
Sheby kiskia simu inapigwa ikabidi awe mpole, mana baba yake sheby akiskia mwai katutuluguswa na sheby, kinachofata kwa sheby ni kufokewa bila sababu za msingi... Hivyo sheby akawa mpoleee,...
Watu walizidi kuingia katika jumba hilo lenye uwanja mkubwa sana,... Mwai alikuwa akikaribisha wageni, chakula chenyewe hakipikiwi hapo chakula kinaletwa spesho kwa ajili ya watu kula... Sheby kwakuwa kazuiwa kwenda kazini hivyo alitoka kidogo nje, wakati huo inaendea mchana, na jukwaa linapambwa, na hio yote ni sifa ya mke wake, sasa kama mimba tu ni hivi, je akizaliwa itakuwaje??... Watu walizidi kumiminika kutoka sehemu mbali mbali walizoalikwa kwa sherehe hio, wengine walibeba zawadi nyingi sana, kama unavyojua mambo ya mjini ni kujishebedua tu... Wakati huo wamama wa uswahilini walikiwa wakicheza muziki taratibu kabisa.... Sasa sheby kutembea kwake alifika mpaka barabarani, alikutana na vilema wengi sana, mana toka ahamie kwenye huo mtaa hajawahi kuuzunguukia na kujua hata majirani, yeye na gari gari na yeye..... Vaa yake tu iliwajulisha wale vilema kiwa huyu ni mtu mwenye wadhifa fulani katika hii dunia....
"seidia ndugu yangu"
Aliongea maskini mmoja aliokuwa hana hata vidole,... Sheby ana huruma sana na watu hao, akiangalia wamama wenye watoto juani,.. Watoto wanalia kwa jua kali
"kwanini msitafuta mahali kwenye kivuli"
Aliongea sheby huku akiwa kainama ili kwenda sambamba na wao,..
"baba, sasa tukikaa kwenye kivuli, nani atatuseidia"
Sheby alitamani hata kulia mana kila kilema hapo ana matatizo yake,..... "Hakuna shida, nitawaseidia ila kwanza mkapate chakula kwanza"
"wapi baba"
"hapo nyumbani kwangu kuna sherehe, na kuna chakula kingi tu kwanini msiende kula"
"ni mbali?"
"wala, ni hapo tu"
Ghafla kuna wengine wakatoa kauli ya kwamba
"na sisi vipofu tutapajuaje baba, tuna njaa"
Aliongea mwanamke mmoja wa makamo, sheby alishindwa kuvumilia, vimachozi vilimtoka kwa kiasi fulani..
"ninyi ambao mnaona mtawaseidia wenzenu kuwashika hata mikono sawa,... Afu mimi nakwenda huku juu nikirudi mmeshakula nawapa pesa kila mmoja pesa yake sawa"
"sawa kijana Tunashukuru sana baba"
Waliongea hivyo huku wakitaka kujiandaa kwenda kula katika nyumba ya sheby ambako kuna sherehe ya kukua kwa mimba ya mwai,.. Sasa ile sheby anataka kuondoka aliona gari ya saidi ikiwa inakuja huku alipo sheby,...
"huyu saidi kaambiwa na nani kiwa nina sherehe huku kwangu"
Aliongea hivyo huku akiwa karibu na wale omba omba.... Sasa wale omba omba walipoona gari wakaamka na kuanza kuomba, vipofu nao waliomba kwa kusikia sauti ya gari,.. Vilema walijikongoja mpaka kwenye gari, lakini sasa cha ajabu na cha kishangaza sheby alishangaa kuona vioo vya gari vinafungwa kabla hajafika eneo la omba omba... Sheby alikasirika sana yaani saidi leo ni wa kufunga vioo vya gari..... Lakini sasa kadri gari inavyozidi kusogea sheby ndio anazidi kumuona dereva.... Laaa haulaaa kumbe hakuwa saidi,.. Dereva alikuwa ni zaituni, sheby haamini macho yake leo anamuona zaituni, mana ni miezi miwili hajawahi kumuona ila leo anamuona tena akiwa na gari ya saidi... Sasa zai kutahamaki mbele anamuona sheby kasimama mbele ya omba omba, tena akiwa kavalia mavazi yake ya kitajiri.....
"haaaaaaaaaaaa.... Huyu ni sheby au macho yangu"
Aliongea zai na kushika breki ya ghafla,.... Zai yeye aliambiwa tu kiwa sheby ni tajiri mkubwa, lakini hajawahi kumuona kwa macho yake akiwa kwenye hali hio, sasa leo ndio anamuona live bila chenga... Yeye sheby hajashtuka kumuona zai,... Sasa zai aliposhika breki, omba omba nao wakajua kasimama kwa ajili yao,.. Sasa wakalizunguka gari ya zaituni na kuanza kuomba, lakini zai macho yake yalikuwa kwa sheby tu... Sheby yeye alikuwa anatabasamu tu muda wote toka alipomuona zaituni..
"ivi huyu ndio yule muuza viazi kweli??? Siamini macho yangu.... Sasa nitamwambia nini sheby mimi... Naona hata aibu kushuka kwenye gari..."
Zaituni alitamani kuondoka lakini alishindwa kwasababu mbele kulikuwa na omba omba.... Alipiga honi ili watoke lakini wapi, yaani walikuwa kama wametumwa vile
"piiiiiiiii piiiiiiiii... Piiiiiiiii..... Piiiiiiii"
Omba omba waliokaa mbele walikuwa ni wale viziwi na mabubu kabisaa, hivyo hawakiwa wakiisikia honi... Waliosikia honi waliondoka lakini ambao hawajasikia waliendelea kukaa mbele ya gari kwa kidhani kuwa boss huyo angeshuka na kuwapatia chochote kitakachokidhi mahitaji yao ya kimaisha....
Huezi amini kijana sheby alikuwa analia kabisa... Hali aliomkuta nayo zai, leo ni mtu wa kupiga honi ili omba omba waondoke,.... Na hoa masikini walijua gari imesimama kwa ajilo yao kumbe ilisimama kwa ajili ya sheby.... Sasa zai baada ya kuona kuna ambao hawaondoki mbele ya gari yake.... Zaituni aliamua ku
Je? Nini kilitokea hapo.... Zaituni atashuka au ataondoka... Na sheby atamwambia nini zaituni... Na zai atajibu nini pale atakapoulizwa na sheby?