Muziki: Kuhama Makazi
...nimekaa hapa Container pub naangusha mbuyu, nishakata mibuyu minne hadi sasa na wa tano unatabasamu mbele yangu, unaonesha manjonjo yake ya ubaridi wenye jasho. Yeah, unashangaa ninaanza kuandika bila kukusalimia, bhasi ndo hivyo, siku ilikuwa nzuri sana tangu asubuhi, kuanzia bosi hadi karani na Kapuku mimi full smile utasema nimeshinda Biko- hela na kishtobe. Sasa kwanini imetokea badala ya kula vitu laini nimeamua kukata vitu vigumu, subiri kwanza nitakupa sababu.
Pale nilipopanga ninaheshimiana sana na baba mwenye nyumba na ana binti yake anatimiza amri ya kufanya mitihani ya fomu four. Huyu dent na wengine wadogo huniita anko Obe nami sina noma nagawa Hi naendelea na mishe zangu, sasa shida imekuja juzi anko wangu si kaja kutoka kanda ya kaskazini, yeye alisema anakuja na surprise na atafikia kwangu kwanza na ugeni wake (nina vyumba vitatu). Hataki aunt ajue, maana aunt ana black belt mambo ya judo na shotokan yamelala. Nikasema haina noma karibuni, mimi nitakuwa Nachingwea wikend hii navuna korosho. Kafika na ugeni wake ambao hataki aunt yangu aujue, ile kufika tu kamkuta binti wa fomu four anapika na haya mambo ya asili hayana mjita, binti kaingia kingi, mgeni alokuja na aunt kumbe kungfu zimelala kaliamsha dude, kajaza watu pale kwangu. Simu ya baba mwenye nyumba inanitaka nihame, anko hapatikani, kamuacha mgeni ndani nikirudi naenda kumchukua maelezo kabla sijahama makazi.
Muziki sasa, leo wikend, sieleweki hueleweki, ngoma droo na ujue nini Kapuku mheshimika, wewe ni mtu bora sana na ndiyo maana uko hapa. Mesejinyingine ya baba mwenye nyumba imeingia anasema anakuja hapa nilipo tuongee maana anajua kabisa mimi huwa sicheleweshi kodi na huwa tunaassistiana sana. dalili za kuendelea kuishi nilipo zinaonekana na nimemtext anko kuwa waziri kasema binti asiolewe bila kuwa na cheti cha fomu foo. Tumuache binti asome na atimize ndoto zake. Wikend njema