Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Sunday Mduara

Ninaamini kabisa ushapangilia wiki hii iweje upande wako na wanaokuzunguka. Mimi wikend ilikuwa nzuri sana na inaendelea kuwa nzuri maana kuna mambo mazuri yametokea na mojawapo ni la kukuona wewe hapa Jukwaani. Asane sana kwa kuwepo hapa. Mbarikiwe sana mlioenda masjid Jumaa ya jana, kanisani Jumamosi na kanisani Jumapili. hongera kwenu mlioenda nyumba za ibada na bado mkawa na muda wa kwenda bar kunjenga uchumi wa nchi, ya kaisari mpeni kaisari. wenye ratiba za kibaiolojia wikend ndo muda mzuri wiki hii kujenga mwili.

Nilikuwa na anko mkubwa tunatazama soka hapa Chelsea akifanya mauaji ya kimbari (naelewa it sound not okay, lakini hapa maana ya kimbari ni ya kisoka zaidi si yale mauaji ya watu 800,000 kule Rwanda) kwa timu ya Man U. Hongera pia Arsenal kwa kilichowapata, ndo maisha na huu huwa ni mwezi wenu.

Muziki sasa, tulipiga story kidogo na anko zaidi akitaka mbinu za kujieleza namna akirudi kwa aunt yangu maana inaonekana majirani wameanza kung'amua kuwa hayupo kwa mkewe. Nikaskuti weee, ushauri wangu akabaki ananitolea macho tu maana ushauri nilioutoa hakuamini kama unaweza kutoka kwangu mimi mtaasisi na mshauri nasaha napima kwa macho. Anko tuwaroge majirani wasiseme ulikokuwa umetekwa. Punguza miduara upate mzingo


 
Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Bwana Mungu wa Majeshi Asante kwa Upendo wako,fadhiki zako na kutuamsha tukiwa wazima na Afya njema,wapo watu wengi walitamani kuiona siku ya leo Baba hawajaweza ,tunatoa Sifa ,Shukurani,Heshima na Utukufu kwa Neema hii.

Tunakuja Mbele zako tukikukabidhi siku ya leo ya Jumatatu 6 Novemba 2017 ikawe njema na ya kukupendeza.
Tunaomba toba kwa yote tuliyokosea.Kwa mawazo ,maneno na matendo Uturehemu twakusihi.
Tuimarishe ili tukupende,
tukuheshimu na kuishi maisha ya kukupendeza wewe tu.
Tunaikabidhi Nchi yetu iwe na Amani.
Tunazikabidhi Familia zetu zidumishe Upendo na Mshikamano.
Tunawakabidhi wagonjwa na wenye shida mbalimbali majumbani na mahospitalini Baba ukawaponye miili na roho pia.
Baba wasafiri wote majini,nchi kavu,angani ukawe nao waende na kurudi salama.Na familia zote Baba mwema zikawe salama na Amani itawale.
Watoto wetu popote walipo makazini,majumbani na mashuleni ukawasimamie wakawe vichwa si mikia wafanye mambo yote kwa ufanisi na mafanikio.Tunaendelea kuwakabidhi watoto wetu wa kidato cha nne onekana kwao Baba.
Baba Mungu tunazikataa kazi zote za shetani zisipate nafasi katika maisha yetu tunazivunja kazi zote hizo katika jina la Yesu Kristo tunamwaga damu ya Yesu Kristo ikatakase kila pando na kuling'oa na kulitupa kuzimu Mfalme wa Amani.
Tunakabidhi kazi zote za mikono yetu zikapate kibali mbele yako nawale wasio na kazi na shughuli za kufanya Baba wape kazi na maarifa ili wauone Utukufu wako, tuingiapo na kutoka utubariki.
Baba Asante kwa Matendo yako Makuu yasiyo na mwisho,tunauona ukuu wako siku zote za maisha yetu tunasema Asante Baba na tunaomba uzidi kutuimarisha imani zetu zipande na kuwa viwango vya juu ili tuweze kushuhudia matendo yako siku hadi siku.Roho Mtakatifu tutie nguvu.
Nakushukuru maana utatenda yote sawa na mapenzi yako
Katika jina la Yesu Kristo naomba naamini na nashukuru Amen

SIKU NJEMA WAPENDWA MBARIKIWE
Amen, Asante kwa sala ya asubuhi mama mchungaji, ubarikiwe sana
 
IMG-20171106-WA0007.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom