Makapuku Forum

Makapuku Forum

The Graves of Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 9
ILIPOISHIA:
SIKUELEWA kwa nini wananiambia vile, ghafla niligeuka kutazama upande wangu wa kushoto, lori kubwa la mafuta, lilikuwa limeshanisogelea huku likiwa kwenye mwendo wa kasi kubwa, taa zote za mbele zikiwa zimewashwa.
“Mungu wangu!” nilisema kwani nilijua hakuna kinachoweza kuniokoa kutoka kwenye mdomo wa mauti, ilikuwa ni lazima linisagesage palepale kama chapati.
SASA ENDELEA...

KUFUMBA na kufumbua, hata sielewi baba alitokea wapi, akanipitia kwa kasi ya radi na kunivutia kule nilikotokea, nikaangukia pembeni ya barabara, lile lori likapita kwa kasi kubwa huku likipiga honi kwa nguvu. Kila mmoja aliamini limenipitia maana niliwaona watu wakishika vichwa, huku mama akianza kuangua kilio kwa sauti kubwa.
Mimi mwenyewe sikuelewa nini kimetokea, niligeuka huku na kule, baba hakuwepo tena, nikawa najitazama mwili wangu nikiwa kama siamini. Sikuwa na jeraha lolote, nikasimama, watu wote wakapigwa na butwaa, mama akaacha kulia na kujishika mdomo.
Nilijikung’uta mwili, nikatazama huku na kule, nilipoona hakuna gari, harakaharaka nilivuka na kwenda mpaka pale mama na ndugu zangu walipokuwa wamesimama, wakiwa ni kama hawaamini walichokuwa wanakiona.
“Togo!” aliita mama huku akinishika mkono, macho yakiwa yamemtoka pima. Nilimuitikia, akaniuliza kama nipo salama, nikamjibu nipo salama, akanikumbatia kwa nguvu huku akimshukuru Mungu wake.
Watu wote walikuwa wameacha kila walichokuwa wanakifanya, wakawa wananitazama mimi. Nadhani lile tukio la kukosakoswa na gari liliwashangaza sana. Hata mimi mwenyewe nilikuwa bado sijui baba aliwezaje kuniokoa.
“Kwani ulifuata nini kule ng’ambo ya barabara,” aliniuliza kaka yangu, nikamtazama usoni nikijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
“Halafu mbona ulikuwa unaongea peke yako?” alihoji kaka yangu mwingine, nikazidi kushangaa. Ni hapo ndipo nilipogundua kuwa kumbe hakuna mtu mwingine yeyote aliyemuona baba zaidi yangu, kwa tafsiri nyepesi ni kwamba baba hakuwa akionekana kwa macho ya kawaida.
Nilitamani kusema kitu lakini nilikumbuka kauli ya baba aliyekuwa akinisisitiza mara kwa mara kwamba lazima niwe na uwezo wa kukaa na vitu kifuani, siyo kuzungumza hovyo.
Waliniuliza maswali mengi lakini sikujibu lolote, nikawa namtazama yule daktari aliyekuwa akiendelea kumpa huduma ya kwanza yule dereva ambaye alikuwa amelazwa chini na kumgeuzia juu ili kuzuia damu isiendelee kumtoka puani.
Kwa hali niliyokuwa naihisi, niliona ni bora nipande kwenye basi na kwenda kukaa kwenye siti yangu kusubiri dereva apate nguvu tuendelee na safari. Hakuna kitu ambacho huwa sikipendi kama kukaa mahali kila mtu anakutazama wewe.
Basi watu waliendelea kunitazama mpaka namalizia kupanda ngazi za basi, kwa kuwa hakukuwa na mtu ndani ya basi, nilienda kukaa kwenye siti iliyokuwa nyuma ya dereva kama baba alivyonielekeza. Kwa bahati nzuri, siti hiyo ilikuwa kwa juu na ya dereva ilikuwa kwa chini, jambo ambalo lingenirahisishia kazi ya kumnyunyizia ule unga mweusi niliopewa na baba endapo kutatokea tena tatizo lolote.
Ilibidi niutoe kwa ajili ya kufanya majaribio, nikachukua kidogo nakujaribu kuunyunyiza kwenye kiti cha dereva, nikaona kumbe ni suala ambalo linawezekana kabisa, nikakaa vizuri kwenye siti yangu.
Sijui nini kilitokea kwani sekunde chache baadaye, niliona watu wote wakianza kuingia kwenye basi, nikasimama na kutazama pale dereva alipokuwa akipewa huduma ya kwanza, nikashangaa kuona tayari alikuwa amesimama na sasa alikuwa akijimwagia maji kichwani na kunawa uso.
Kila kitu kilitokea kwa kasi kubwa sana kiasi cha kunifanya nibaki na maswali mengi yasiyo na majibu. Nilichohisi ni kwamba huenda kile kitendo changu cha kuumwagia ule unga pale kwenye siti ya dereva ndicho kilichompa nguvu haraka dereva huyo.
Kwa kuwa siti hiyo haikuwa yangu, mwenye siti yake alipokuja na kutaka kukaa, nilimuomba akakae kwenye siti yangu, kwa bahati nzuri hata yeye kumbe alikuwa akiogopa kukaa mbele hasa kutokana na ile hali ya kunusurika ajali iliyotokea, nikamuonyesha siti yangu ambapo alienda kukaa.
Muda mfupi baadaye dereva aliingia ndani ya basi huku akijifuta maji aliyonawa kwa kutumia kitambaa kidogo, akakaa kwenye siti yake na kufunga mkanda lakini kabla hajawasha gari aligeuka nyuma, macho yangu na yake yakagongana.
“Sura yako kama siyo ngeni,” alisema huku akinitazama kama anayejaribu kukumbuka jambo fulani. Kiukweli mimi sikuwa namjua wala sikumbuki kama niliwahi kuonana naye sehemu yoyote, nikatingisha kichwa kumkatalia, akawa bado anaendelea kung’ang’aniza kwamba kuna sehemu tumewahi kuonana. Ilibidi nimkubalie tu huku tabasamu la uongo likiwa limechanua kwenye uso wangu.
“Jamani naomba kila mmoja asali kwa imani yake kabla hatujaendelea na safari,” alisema dereva, kweli kila mtu akaanza kusali kwa imani yake. Ilichukua kama dakika mbili hivi, kumbe mle ndani kulikuwa na walokole ambao nao walianza kunena kwa lugha.
Baadaye dereva aliwasha gari, akapiga ‘resi’ nyingi kisha akaliondoa gari kwa mwendo wa taratibu, akaliingiza barabarani na kuendelea kuliendesha kwa mwendo wa taratibu, watu wote ndani ya basi walikuwa kimya kabisa.
Tuliendelea kushuka kwenye mteremko wa Mlima Nyoka mpaka tulipofika chini kabisa, akabadili gia na tukaanza kuupandisha mlima mkali uliopo eneo hilo. Kwa wakazi wa Mbeya au watu waliowahi kufika huko, watakuwa wananielewa vizuri ninapouzungumzia Mlima Nyoka.
Safari iliendelea na hatimaye tukaumaliza mlima huo, nikaona kila mtu ndani ya basi ameanza kurudi kwenya hali yake ya kawaida, stori za hapa na pale zikaanza, wengi wakimshukuru Mungu wao kwani pengine muda huo tungekuwa tukizungumza mengine.
Dereva naye alizidi kutulia kwenye usukani, akaongeza mwendo na sasa tukawa tunaenda kwenye mwendo ambao mabasi ya mikoani hutumia. Safari iliendelea vizuri huku wengi wakianza kusahau kilichotokea. Kwa upande wangu muda wote nilikuwa makini kabisa kuhakikisha natekeleza kile nilichoambiwa na baba.
Kwa bahati nzuri, hakukuwa na kikwazo kingine chochote kilichotokea, majira ya kama saa nane mchana tukawa tayari tumewasili Ilula, Iringa mahali ambapo abiria hupata mapumziko mafupi ya chakula cha mchana.
Dereva alitutangazia kwamba tuna dakika kumi ya kwenda ‘kuchimba dawa’ pamoja na kununua vyakula, abiria wote wakaanza kushuka. Mama na ndugu zangu nao walishuka, na mimi nikaungana nao.
Jambo la kwanza tulienda kuchimba dawa, tuliporudi mama akawa anatuuliza kila mmoja anataka kula chakula gani. Tuliagiza vyakula, kila mmoja anachokitaka, mama akatunulia na soda kisha tukarudi ndani ya basi.
Muda mfupi baadaye, abiria wote walirudi ndani ya basi lakini kabla hatujaondoka, dereva alituambia kwamba tunaelekea kwenye Mlima Kitonga ambao ni mbaya kuliko Mlima Nyoka, akatuambia kwamba kila mmoja asali tena kwa mara nyingine kwa sababu hajui kama tutavuka salama. Sikuwahi kufika Kitonga lakini stori nilizokuwa nikizisikia, ni kwamba lilikuwa eneo la hatari sana ambalo mara kwa mara ajali mbaya zilikuwa zikitokea na kusababisha vifo vya watu wengi kila kukicha.
Nilijikuta nikitetemeka sana lakini nikajipa moyo kwamba kila kitu kitakuwa sawa. Tuliendelea na safari na muda mfupi baadaye, tulifika eneo ambalo bila hata kuuliza, nililitambua kwamba ndiyo Kitonga, kutokana na jinsi lilivyokuwa.
“Kuna tukio baya linataka kutokea, kuwa makini,” nilisikia sauti ya baba ikiniongelesha sikioni mwangu, nikageuka huku na kule, baba hakuwepo, nikajua kwa vyovyote lazima alikuwa ameona jambo ndiyo maana akanipa tahadhari, nikajiweka vizuri kitini, nikawa natazama huku na kule.
Je, nini kitaendelea? Usikose next issue!
 
The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 10
ILIPOISHIA:
“Kuna tukio baya linataka kutokea, kuwa makini,” nilisikia sauti ya baba ikiniongelesha sikioni mwangu, nikageuka huku na kule, baba hakuwepo, nikajua kwa vyovyote lazima alikuwa ameona jambo ndiyo maana akanipa tahadhari, nikajiweka vizuri kitini, nikawa natazama huku na kule.
SASA ENDELEA...

Niliingiza mkono mfukoni na kutoa ile dawa aliyonipa baba, nikaishika ili chochote kikitokea iwe rahisi kufanya kama nilivyoelekezwa. Tukaanza kuteremka kwenye mteremko mrefu, wenye konakona nyingi na makorongo ya kutisha wa Kitonga.
Nilielewa kwa sababu gani eneo hilo lilikuwa maarufu sana, barabara ilikuwa imechomngwa pembezoni mwa milima na mawe makubwa, hali iliyofanya kama upande mmoja kukiwa na ukuta wa mlima basi upande wa pili kuna bonde refu sana.
Yaani kwa kutazama tu urefu wa yale makorongo, nilijikuta nikihisi kizunguzungu, nikawa najiuliza ikitokea dereva akakosea na kupeleka gari kwenye yale makorongo nini kitatokea? Sikupata majibu.
Safari iliendelea, dereva akawa amepunguza sana mwendo, abiria wote ndani ya gari wakiwa kimya kabisa. Nadhani kila mmoja alikuwa na kumbukumbu ya kilichotokea Mlima Nyoka. Ghafla tulishtuka baada ya kuona kuna lori la mafuta, tena likiwa na trela kwa nyuma, likija kwa kasi kubwa nyuma yetu.
Tulishtushwa na kishindo kikubwa kilichosikika nyuma, wote tukageuka na kusimama kwenye siti, tukawa tunatazama nini kinachoendelea? Inavyoonesha, lile lori lilikuwa limepasuka tairi la mbele na kumshinda dereva, sasa likawa linayumba barabara nzima.
Abiria wote walianza kupiga kelele kwenye lile basi, hakuna ambaye alijua nini kitatokea kwa sababu kama lile gari lori lingeendelea kuja kwa mwendo ule, lingeligonga basi letu kwa nyuma na kwa ile kasi yake, maana yake lingeturushia kwenye korongo refu na kutuangukia kwa juu.
Sijui kama kuna mtu angepona, ukizingatia kwamba lilikuwa ni lori la mafuta na lilionesha kuwa na mzigo. Nilichokifanya, kwa haraka nilimnyunyizia ule unga dereva ambaye bado hakuwa akijua afanye nini. Nilipomnyunyizia tu, nilimuona akibadili gia haraka, akaongeza mwendo na kulifanya basi lianze kushuka mteremko ule kwa kasi kubwa.
Kuongeza kasi kwa ghafla kuliwafanya abiria wengine wazidi kuchanganyikiwa, kelele zikazidi ndani ya basi, lile lori nalo likawa linazidi kuja kwa kasi kubwa nyuma yetu.
Wakati dereva akizidi kukanyaga mafuta na kulifanya basi lishuke kwa kasi ya ajabu mteremko ule hatari, ghafla tulishtukia lori jingine likiwa limepaki mbele yetu, dereva na utingo wake wakiwa wamekata matawi ya miti na kusambaza barabarani, ishara kwamba lilikuwa limeharibika.
Kwa kasi ambayo gari tulilopanda lilikuwa likishuka nayo, hata mimi mwenyewe sikuamini kama dereva ataweza kulimudu na kulikweopa lile lori mbele yetu.
Hata hivyo, dereva alitumia kile ambacho wengi huita uwezo binafsi, bila kupunguza mwendo hata kidogo, alizungusha usukani kwa kasi, gari likageuka kama linaenda kugonga jiwe kubwa lililokuwa pemebini ya barabara, kisha akazungusha tena usukani kwa kasi, gari likageuka tena upande wa pili.
Kitendo kile kililifanya basi letu lipenye kwenye uwazi mwembamba uliokuwepo kati ya lile gari lililoharibika na ukuta wa upande wa pili, kufumba na kufumbua likapita pale katikati kwa kasi kubwa na kulipita lile gari bovu, dereva akaanza kupunguza mwendo huku akibadilisha gia.
Sekunde chache baadaye, kilisikika kishindo kikubwa nyuma yetu, lile lori la mafuta lilikuwa limeligonga lile lori jingine bovu kwa nyuma na kulisukuma mita kadhaa kabla ya yote mawili kuangukia kwenye korongo refu, watu wote wakawa hawaamini kilichotokea.
Cha ajabu sasa, wakati watu wote wakitazama kilichotokea kule nyuma, nilishtuka kugundua kwamba kumbe aliyekuwa akiendesha gari hakuwa yule dereva wetu bali baba, macho yakanitoka pima nikiwa siamini ninachokiona. Alipogundua kwamba namtazama, naye alinigeukia na kunitazama kwa sekunde chache, akawa aanendelea kubadili gia huku akifunga breki.
Mbele kidogo kulikuwana uwazi pembeni ya barabara ambao uliwekwa maalum kwa ajili ya magari yanayoharibika njiani, akaendelea kufunga breki na hatimaye, akalisimamisha kabisa basi letu. Wakati watu bado wakiwa bize kushangaa kule nyuma, alifungua mlango wa dereva, akashuka huku akiendelea kunitazama na kunionesha ishara kwamba nisiseme chochote.
Akapotea kwenye upeo wa macho yangu na kuniacha na maswali mengi yasiyo na majibu. Cha ajabu kingine, aliposhuka, pale kwenye siti ya dereva alikuwa amekaa dereva yuleyule, tena akiwa amefunga na mkanda kabisa lakini kama ilivyokuwa mara ya kwanza, naye alionesha kushtuka kama mtu aliyekuwa amelala usingizi mzito. Akageuka huku na kule, macho yangu na yake yakagongana.
‘Kwani kumetokea nini?” aliniuliza kwa sauti ya chini huku akitaka mtu mwingine yeyote asielewe. Nadhani hata yeye alishagundua kwamba kuna mambo yasiyo ya kawaida yalikuwa yakiendelea.
“Ajali, ajali mbaya sana,” nilimjibu huku nikimuonesha kule nyuma tulikotoka ambako moshi mzito mweusi ulikuwa ukifuka kutoka bondeni. Tayari abiria wengi walikuwa wameshashuka kwenye basi na kuanza kurudi kule eneo la tukio. Harakaharaka dereva alifungua mlango na kushuka, na mimi ikabidi nishuke tena safari hii nilipitia pale kwenye mlango wa dereva.
Tukawa tunakimbilia pale eneo la tukio. Trela moja la lile lori la mafuta, lilikuwa limekatika na kuanguka katikati ya barabara kimshazari, jambo lililofanya mawasiliano kati ya pande hizo mbili za barabara yakatike. Hakukuwa na gari ambalo lingeweza kuvuka tena mpaka trela lile liondolewe.
Ajali ilikuwa mbaya kiasi cha kumfanya kila mmoja aliyeshuhudia, ainue mikono yake juu na kumshukuru Mungu kwa sababu kama isingekuwa miujiza iliyotokea, ilibidi basi letu ndiyo ligongwe na kuangukia kule bondeni kisha kuanza kuungua kama ilivyokuwa imetokea.
Tukiwa bado tunaendelea kushangaa kilichotokea, tulishangaa kuona mtu akitoka ndani ya lile lori la mafuta lakini mwili wake wote ukiteketea kwa moto, akawa anajaribu kukimbia lakini hakufika mbali, moto ukamzidi na kumfanya aanguke chini.
Kwa jinsi magari hayo yalivyodondokea chini bondeni, hakuna mtu yeyote ambaye angewahi kwenda kumsaidia yule mtu kwa sababu kwanza eneo lenyewe lilikuwa haliwezi kupitika kirahisi, watu wakawa wanapiga kelele huku tukimshuhudia yule mtu ambaye sijui ndiyo alikuwa dereva au utingo wa gari lililopata ajali akiteketea bila msaada wowote.
Muda mfupi baadaye, magari mengine mengi yalishawasili eneo hilo na kwa sababu barabara ilikuwa imefungwa, yalisimama na kupanga foleni ndefu, abiria na madereva wakawa wanashuka kuja kujionea kilichotokea.
Kila aliyekuwa anaona kilichotokea, alikuwa haamini kabisa. Ilikuwa ajali mbaya mno ambayo kama ingehusisha gari la abiria, sidhani kama kuna mtu yeyote angetoka salama.
Kwa kuwa tulikuwa nyuma ya muda na bado tulikuw ana safari ndefu, ilibidi turudi kwenye basi letu, dereva naye akawa anaonekana kuwa na maswali mengi kuliko majibu.
Japokuwa kwa mara nyingine abiria wote walikuwa wakimsifia kwa jinsi alivyoweza kuepusha ajali ile, mwenyewe alikuwa akijua kutoka ndani ya moyo wake kwamba siyo yeye aliyefanya kazi hiyo na hakuwa akijua chochote kilichotokea.
Tulirudi kwenye basi na baada ya kuhakikisha abiria wote wameingia, dereva aliondoa gari kwa mwendo wa taratibu, gumzo kubwa ndani ya basi likawa ni juu ya ajali hiyo. Wakati watu wakiendelea kujadiliana kuhusu ajali hiyo, mimi bado nilikuwa na maswali mengi mno kuhusu baba.
Bado sikuwa na majibu na hakukuwa na mtu yeyote wa kunijibu zaidi ya baba mwenyewe. Jambo kubwa ambalo lilikuwa likijirudia ndani ya kichwa changu, lilikuwa ni je, kweli baba ni mchawi?
“Unasemaje?” nilisikia sauti ya baba akiniuliza kwa ukali, nikageuka huku na kule lakini baba hakuwepo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 11
ILIPOISHIA:
Bado sikuwa na majibu na hakukuwa na mtu yeyote wa kunijibu zaidi ya baba mwenyewe. Jambo kubwa ambalo lilikuwa likijirudia ndani ya kichwa changu, lilikuwa ni je, kweli baba ni mchawi?
“Unasemaje?” nilisikia sauti ya baba akiniuliza kwa ukali, nikageuka huku na kule lakini baba hakuwepo.
SASA ENDELEA...

“Sijaongea kitu,” nilijibu, nikasikia baba akiachia msonyo mrefu kisha ukimya ukatawala. Kumbe nilipotamka lile neno ‘sijaongea kitu’, niliongea kwa sauti kubwa kiasi cha kuwafanya abiria wengi ndani ya basi, wanisikie.
“Kaka, unaongea na nani?” sauti ya msichana aliyekuwa akicheka kwa sauti ilisikika, ikifuatiwa na abiria wengine, ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye lindi la mawazo. Nikashtuka na kukaa vizuri kwenye siti yangu.
“Anaogopa ajali huyo,” alipaza sauti abiria mwingine, watu karibu wote kwenye basi wakacheka. Nilimgeukia mama, nikamuona yeye yupo siriasi tofauti na abiria wengine, nikageuka na kukaa vizuri kwenye siti yangu.
Yule msichana aliyekuwa amekaa siti ya upande wa pili na pale nilipokuwa nimekaa, alivua ‘headphones’ zake, akawa anaendelea kunitazama huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.
Tangu tunaanza safari wala sikuwa najua kwamba kuna mtu kama yeye ndani ya gari, ni mpaka pale alianza kunicheka ndipo nilipoanza kumtilia maanani. Alikuwa ni msichana mdogo lakini wa kisasa, akiwa na simu ya kisasa mkononi, halafu akiwa amevalia mavazi kama wasichana wa mjini ambao nilizoea kuwaona kwenye TV.
Nilipoendelea kumtazama kwa macho ya kuibia, niligundua kwamba alikuwa na sura nzuri sana halafu akitabasamu kuna vishimo kwenye mashavu yake vinajitokeza, nikajikuta navutiwa kumtazama.
Safari iliendelea lakini mara kwa mara yule msichana alikuwa akinigeukia na kunitazama, tofauti na mara ya kwanza ambapo alikuwa kama anacheka kwa kunidharau, safari hii alikuwa akinitazama kwa makini.
Katika ujanja wangu wote niliokuwa nikiuonesha kijijini kwetu, makongorosi, Chunya, hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa kama kuzungumza au kujichanganya kwa namna yoyote na wasichana, hasa wa rika langu.
Tangu naanza kupevuka, mpaka namaliza shule ya msingi na hata baada ya kuanza maisha ya mtaani, sikuwahi kuwa na mazoea na msichana yeyote, zaidi ya dada zangu kwa hiyo kitendo cha msichana huyo kuwa ananitazama mara kwa mara, tena msichana mwenyewe mrembo kwelikweli, kilinikosesha mno utulivu.
Kuna wakati nilikuwa natamani hata nirudi kule kwenye siti yangu ya mwanzo, nilikokuwa nimekaa namama na ndugu zangu lakini nilipofikiria kuhusu kazi nzito niliyopewa na baba, ilibidi nijikaze kiume.
Nilipoona anazidi kunitazama, kuna wakati nilifumba macho na kujifanya nimelala lakini nikasikia ile sauti ya ajabu ya baba ikinijia, akaniambia sitakiwi kulala kwa sababu nina jukumu la kuhakikisha safari inakuwa salama.
Nikawa sina cha kufanya zaidi ya kujikaza kiume, safari hii na mimi niliamua kuwa namtazama. Kama kawaida yake, alinigeukia, akawa ananitazama kwa makini, ikabidi na mimi nimgeukie, tukawa tunatazamana. Cha ajabu, alipoona na mimi namtazama japo kwa uso uliojawa na aibu, aliachia tabasamu pana.
Nikajikuta na mimi nikitabasamu, haraka nikakwepesha macho yangu na kugeukia upande wa dirishani, nikawa natazama nje. Safari iliendelea huku nikiendelea kujishtukia, baadaye nilipomgeukia tena yule msichana, niligundua kwamba tayari alishalala huku headphones zake zikiwa masikioni.
Nikashusha pumzi ndefu kama mtu aliyetua mzigo mzito kichwani, nikakaa vizuri kwenye siti yangu na kuendelea nakazi niliyopewa na baba. Kwa bahati nzuri, safari hii hakukuwa na kipingamizi chochote, safari ikaendelea mpaka tulipofika sehemu maarufu iitwayo Chalinze Choma Nyama.
Dereva alipunguza mwendo na kusimamisha basi, akatutangazia abiria kwamba anatoa dakika kumi tukachimbe tena dawa na kujinyoosha. Bila kupoteza muda, abiria walianza kuteremka, mimi nikageuka na kutazama pale mama na wale ndugu zangu walipokuwa wamekaa, nikawaona nao wakiinuka.
Ilibidi nisubiri abiria wengine wapite, ndugu zangu walipokaribia, niliinuka na kuungana nao, tukawa tunataniana na kaka na dada zangu kama kawaida yetu tunapokutana. Cha ajabu, eti nao walikuwa wakinicheka kwamba woga wa kupata ajali ulisbabisha niwatie aibu kwa kupayuka kwenye basi.
Wakawa wananicheka na kunisukumasukuma, jambo ambalo sikupendezewa nalo. Tuliposhuka chini, waliendelea kunitania lakini kwa kuwa sikuwa naupenda utani wao, niliamua kujitenga nao, nikazunguka mpaka nyuma ya gari, nikasimama nikiegamia basi huku nikitazama kule tulikotokea, uso wangu ukiwa umekosa amani.
“Hawa washenzi wangejua mimi na baba ndiyo tuliowalinda wasipate ajali wasingekuwa wananicheka hivi,” nilisema huku nikikumbuka pia vicheko vya abiria wengine ndani ya basi, muda ule nilipopayuka kwa nguvu ndani ya basi.
Mawazo yangu yalizama kwenye hisia chungu, nikawa naendelea kuwaza mambo mengi ndani ya kichwa changu. Ghafla nilishtushwa na sauti ya kike pembeni yangu.
“Mambo!”
“Safi tu,” nilijibu huku nikianza kujichekesha, aibu zikiwa zimenijaa baada ya kugundua kuwa ni yule msichana wa kwenye basi aliyekuwa akinitazama sana.
“Mbona umekaa peke yako huku halafu unaonekana kama una mawazo sana?”
“Ahh! Kawaida tu, nahisi uchovu wa safari,” nilimjibu, huku lafudhi ya kijijini ikishindwa kujificha kwenye mazungumzo yangu. Aliendelea kunipigisha stori za hapa na pale, akionesha kuchangamka mno utafikiri tunafahamiana.
“Nisindikize kule upande wa pili nikanunue soda za kopo, naona huku hakuna,” alisema msichana huyo ambaye manukato yake mazuri aliyojipulizia, yalizifurahisha mno pua zangu.
Tulisimama pembeni ya barabara, akageuka huku na kule kuangalia kama hakuna gari linalokuja, na mimi nikawa namfuatisha kwa sababu sikuwa mzoefu sana wa barabara ya lami na sikuwa najua vizuri namna ya kuvuka barabara. Alipohakikisha kwamba hakuna gari, alinishika mkono, nadhani aliniona jinsi nilivyokuwa na hofu moyoni, tukaanza kuvuka.
Mikono yake ilikuwa laini mno kiasi kwamba nilifurahia jinsialivyonishika. Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nikaanza kuhisi hali isiyo ya kawaida. Tulivuka mpaka ng’ambo ya pili, akafungua pochi yake ndogo na kutoa noti ya shilingi elfu kumi, akampa muuzaji wa vinywaji aliyekuwa na kibanda chake pembeni ya barabara.
“Unakunywa soda gani?” aliniuliza huku yeye akichukua soda yake, nikakosa cha kujibu zaidi ya kuanza kuchekacheka tu.
“Nakuchagulia, nataka unywe ninayokunywa mimi,” alisema huku akinigeukia, akanipa soda ya Sprite ya kopo, akafungua ya kwake na kuingiza mrija, mimi nikawa nashangaashangaa kwa sababu sikuwahi kunywa soda ya kopo hata mara moja wala sikuwahi kutumia mrija.
Akiwa ameshapiga funda moja, alichukua lile kopo la soda mikononimwangu, anaipa ile ambayo alishaifungua na kunywa kidogo, nikawa namshangaa kwani hayo yalikuwa mambo mageni kabisa kwangu, nilizoea kuyaona kwenye video.
Alifungua na ile nyingine, nayo akapiga funda moja, nikawa sina cha kufanya zaidi ya kuendelea kunywa, akawa ananitazama kwa macho yaliyobeba ujumbe mzito.
“Unaitwa nani?”
“Togo,” nilimjibu kwa kifupi, akageuka kama anayetazama upande wa pili wa barabara, nikapata fursa ya kulisanifu vizuri umbo lake. Alikuwa ni msichana mzuri sana, upande wa nyuma alikuwa amejazia huku kiuno chake kikiwa kimegawanyika, kama nyigu ambao kule kijijini tulikuwa tukiwaogopa kutokana na sumu yao wanapokung’ata.
Suruali ya jeans aliyovaa, ililifanya umbo lake lijichonge vizuri, ghafla akageuka, akanibamba nikiwa namtazama kwa nyuma, nikazidi kujisikia aibu.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 12
ILIPOISHIA:
Alikuwa ni msichana mzuri sana, upande wa nyuma alikuwa amejazia huku kiuno chake kikiwa kimegawanyika, kama nyigu ambao kule kijijini tulikuwa tukiwaogopa kutokana na sumu yao wanapokung’ata.
Suruali ya jeans aliyovaa, ililifanya umbo lake lijichonge vizuri, ghafla akageuka, akanibamba nikiwa namtazama kwa nyuma, nikazidi kujisikia aibu.
SASA ENDELEA...

“Mbona unaniangalia hivyo?”
“Mimi?” Nilijifanya kuvunga, akanisogelea na kunipiga kakibao kepesi begani huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye kwenye uso wake. Na mimi nikawa nacheka huku aibu zikiwa zimenijaa.”
“Dar es Salaam unaishi sehemu gani?” aliniuliza swali ambalo lilikuwa gumu sana kulijibu kwani ukweli ni kwamba sikuwa naijua Dar wala sikuwahi kufika kabla. Nikawa nababaika mwenyewe, akajiongeza na kuniuliza:
“Kwani hii ndiyo mara yako ya kwanza kufika Dar?”
“Ndiyo,” nilijibu harakaharaka kwa sababu alikuwa amenipunguzia sana kazi ya kumjibu. Akaniambia kwamba yeye anaishi na wazazi wake Kijitonyama. Akaniambia kwamba alikuwa amemaliza chuo akisomea uhasibu na alikuwa anatoka Mbeya kuwasalimu bibi na babu yake wa upande wa mama.
“Wanaishi Mbeya sehemu gani?” nilimuuliza, akaniambia wanaishi Katumba, njia panda ya kwenda Mwakaleli. Maeneo hayo sikuwa nimewahi kufika zaidi ya kusikia tu kwa watu, nikawa natingisha kichwa kumkubalia. Akaendelea kunieleza kwamba mama yake alikuwa Mnyakyusa lakini baba yake alikuwa ni mtu kutoka Mkoa wa Pwani ingawa hakunieleza ni kabila gani.
Hatimaye dakika kumi ziliisha, dereva akaanza kupiga honi akitupa ishara kwamba muda wa kuingia kwenye basi umefika. Kwa hizo dakika chache nilizokaa na msichana huyo, niligundua kwamba alikuwa mcheshi, mchangamfu na asiye na maringo kama walivyo wasichana wengi warembo kama yeye.
“Lakini hujaniambia unaitwa nani.”
“Unataka kujua jina langu?”
“Ndiyo.”
“Sitaki,” alisema huku akinipiga tena begani, akaanza kukimbia kuelekea kwenye basi. Sikuelewa kitendo hicho kilikuwa na maana gani, wakati anakimbia nilishuhudua kitu kingine ambacho kiliusisimua sana moyo wangu, mpaka nikawa najiuliza zile hisia nilizokuwa nazisikia kwa wakati huo zilikuwa na maana gani?
Kwa kifupi nilijisikia raha sana kufahamiana na msichana huyo. Niliendelea kumtazama akikimbia mpaka alipofika kwenye ngazi za kupanga kwenye basi, akageuka na kunitazama kisha akapanda ngazi. Na mimi nilitembea harakaharaka huku nikiendelea kuchekacheka mwenyewe, mkononi nikiwa na kopo la soda ambayo nilikua nimeinywa nusu.
Nilipopanda na kuingia ndani ya gari, ndugu zangu wote walishangaa kuniona nikiwa na soda ya kopo, tena nikinywa kwa mrija.
Niliwaona wote walivyomeza mate, wakawa wanaulizana nimeipata wapi soda hiyo? Sikuwajali kwa sababu bado nilikuwa na hasira nao, nikakaa kwenye siti yangu, nikageuka na kumtazama yule msichana ambaye mpaka muda huo hakuwa amenitajia jina lake, nikashtuka tena kugundua kwamba kumbe alikuwa ametulia akinitazama kila nilichokuwa nakifanya.
Macho yangu na yake yalipogongana, aliachia tabasamu hafifu halafu eti na yeye akakwepesha macho yake kwa aibu, yaani mwanzo mimi ndiyo nilikuwa nakwepesha macho yangu lakini ghafla na yeye alianza kukwepesha macho yake kwa aibu. Dereva aliondoa gari na safari ikaendelea.
Safari hii umakini ulikuwa ukinipungua sana kichwani mwangu kwani mara kwa mara tulikuwa tukitazamana na yule msichana na kuishia kuchekacheka tu. Nashukuru hakuna jambo lolote baya lililotokea mpaka tulipoanza kuingia mjini.
Tulipofika Kibaha, gari lilisimama na yule abiria aliyekuwa amekaa pembeni yangu, alisimama na kushuka, harakaharaka nikamuona yule msichana akikusanya kila kitu chake na kuja kukaa pembeni yangu. Aliponisogelea tu, nilianza tena kusikia harufu ya manukato aliyojipulizia, ambayo kiukweli yalinivutia sana.
Akakaa pembeni yangu na kuniegamia kimtindo kabla ya kujiweka vizuri kwenye siti yake.
“Yule niliyekaa naye hata stori hana, muda wote analala tu bora nikae na wewe,” alisema huku akinipigapiga begani, nikawa natabasamu tu kwani kiukweli hata mimi nilikuwa napenda kukaa naye siti moja.
“Ulisema unataka kujua jina langu?” alianzisha mazungumzo, niikamjibu kwa kutingisha kichwa, akaniambia ananipa mtihani nitafute mwenyewe jina lake. Kiufupi ni kwamba, kwa muda mfupi tu niliokaa naye, alionesha kupenda sana urafiki wetu uendelee, jambo ambalo hata mimi nilikuwa nalipenda ingawa mara kwa mara nilikuwa najishtukia.
Hata nilipokuwa nacheka, sikuwa napenda ayaone meno yangu kwani ya kwake yalikuwa meupe sana na masafi lakini kwangu mimi, hata sikuwa nakumbuka mara ya mwisho kupiga mswaki ni lini, si unajua tena maisha ya kijijini.
“Una simu?” aliniuliza swali ambalo lilinifanya nijisikie tena aibu. Sikuwa na simu, sikuwahi kumiliki wala sikuwa najua namna ya kuitumia, nikawa natingisha kichwa kukataa, akaniambia alikuwa na simu mbili lakini hiyo nyingine hakuwa akiitumia kwa sababu ilikuwa ya kizamani.
“Basi nipe mimi,” nilisema kwa utani kwani nilijua ni jambo ambalo haliwezekani, akacheka na kufungua kibegi chake kidogo, akatoa simu ndogo aina ya Nokia ya tochi na kunipa.
“Chukua utakuwa unatumia,” alisema. Nikapigwa na butwaa nikiwa ni kama siamini. Kuna wakati nilihisi kwamba pengine alikuwa akinitania lakini mwenyewe alisisitiza kwamba ni kweli amenipa. Muda huo, tayari gari lilikuwa limeshawasili Ubungo, sikuwa napajua zaidi ya kusikia tu watu wakisema hapo ndiyo ubungo.
Tayari giza lilishaanza kuingia, taa nyingi zilizokuwa zinawaka kila upande zikanifanya nijihisi kama nilikuwa kwenye ndoto.
Waliosema mjini kuzuri hawakukosea, Dar ilikuwa na tofauti kubwa sana na kule kijijini nilikozaliwa na kukulia, kila kitu kilikuwa kigeni kwangu. Wakati nikiendelea kushangaashangaa, nilisikia mama akiniambia kwamba natakiwa kuwa makini kuchukua mizigo iliyokuwa imewekwa kwenye buti.
Harakaharaka nikateremka na abiria wengine, hata sikukumbuka nilipotezana saa ngapi na yule dada, ushamba wa mjini ulinipa mchecheto mkubwa ndani ya moyo wangu, nikaenda mpaka kwenye buti nikiwa na wale ndugu zangu wengine ambao nao walikuwa wakishangaashangaa, tukafanikiwa kushusha mizigo yetu yote na kuiweka pembeni.
“Twendeni nilisikia sauti ya baba akizungumza, kugeuka pembeni, sote tulipigwa na butwaa kumuona baba akiwa anafungua milango ya teksi. Hakuna aliyejua baba alifika saa ngapi Dar es Salaam kwa sababu kama aliweza mpaka kuzungumza na dereva wa teksi na kukaa pale wakitusubiri, maana yake ni kwamba aliwahi sana kufika.
“Unajua wewe huna akili kabisa,” baba alianza kunifokea baada ya kumaliza kupakiza mizigo kwenye teksi, nikawa nashangaa kwa nini baba ananiambia maneno hayo.
“Yule uliyekuwa umekaa naye kwenye basi ni nani?”
“Ni rafiki yangu.”
‘Unamjua wewe? Na hicho alichokupa una uhakika gani kama ni simu? Ujinga wako utaiponza familianzima,” alisema maneno ambayo yalinishangaza sana.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Muziki: Mvua ya Joto

Mmmh! Leo nitaaandika haraka haraka maana kuna ndoto nataka niiote nikilala na ninavyojijua nikiandika taratibu siwezi kuiota hii ndoto. FYI, hii ndoto ni mwendelezo tu wa ndoto zangu nyingi ukiacha ile moja ambayo ilinipaga jina baya ugenini. Nitakwambia kuhusu hiyo ndoto siku moja labda ijumaa nikiwa niko tingasi, na itabidi nikueleze mapema kabla mjomba wangu hajanikumbusha. Kwanza nakusalimia sana na ama baada ya salamu ninakukaribisha tena kwenye kipengele hiki cha muziki, haijalishi unakipenda au kinakuchukiza lakini kwa kuwa wewe upo hapa basi hakijaharibika kitu.

Nikushukuru sana Tumosa kwa kudhamini magazeti, wageni waliposikia mama JJ ni nani mimi nimeona niwape nyeupe na nyeusi, shululu alimaanisha kuwa wewe ndo unayempa usingizi. Asante BlessedHope kwa sala za muda wote na ambazo kiukweli leo zimeongezewa nakshhi na Transcend pamoja na SHIMBA YA BUYENZE , mnafanya vema sana wadau. Mnajua huwa sichoki kuwashukuru aunty yangu Shunie kwa hadithi bila kumsahau aliye moyoni mwangu hadi najisahau kukutambulisha kwake, la habibt husna muba, anko wangu Lyon Lee hongera kwa kutaka kutenganisha ngao ya maji na ngao ya kidonge. Ninakushukuru pia kwa kuendelea na neno lako kuwa nikienda Kigamboni nguo zangu zilowekwe na zianikwe kwenye mvua. You made my day na smile nililokuwa nalo nakumbuka ulinilazimisha kutabasamu pale tulipokuwa Morogoro kwenye ile bar tuliyokunywa Safari lager na chapati

Muziki sasa, hebu nitarudi tena

 
Muziki: Mvua ya Joto

Mmmh! Leo nitaaandika haraka haraka maana kuna ndoto nataka niiote nikilala na ninavyojijua nikiandika taratibu siwezi kuiota hii ndoto. FYI, hii ndoto ni mwendelezo tu wa ndoto zangu nyingi ukiacha ile moja ambayo ilinipaga jina baya ugenini. Nitakwambia kuhusu hiyo ndoto siku moja labda ijumaa nikiwa niko tingasi, na itabidi nikueleze mapema kabla mjomba wangu hajanikumbusha. Kwanza nakusalimia sana na ama baada ya salamu ninakukaribisha tena kwenye kipengele hiki cha muziki, haijalishi unakipenda au kinakuchukiza lakini kwa kuwa wewe upo hapa basi hakijaharibika kitu.

Nikushukuru sana Tumosa kwa kudhamini magazeti, wageni waliposikia mama JJ ni nani mimi nimeona niwape nyeupe na nyeusi, shululu alimaanisha kuwa wewe ndo unayempa usingizi. Asante BlessedHope kwa sala za muda wote na ambazo kiukweli leo zimeongezewa nakshhi na Transcend pamoja na SHIMBA YA BUYENZE , mnafanya vema sana wadau. Mnajua huwa sichoki kuwashukuru aunty yangu Shunie kwa hadithi bila kumsahau aliye moyoni mwangu hadi najisahau kukutambulisha kwake, la habibt husna muba, anko wangu Lyon Lee hongera kwa kutaka kutenganisha ngao ya maji na ngao ya kidonge. Ninakushukuru pia kwa kuendelea na neno lako kuwa nikienda Kigamboni nguo zangu zilowekwe na zianikwe kwenye mvua. You made my day na smile nililokuwa nalo nakumbuka ulinilazimisha kutabasamu pale tulipokuwa Morogoro kwenye ile bar tuliyokunywa Safari lager na chapati

Muziki sasa, hebu nitarudi tena


Asante Obe ,ila kwangu muziki haujafunguka..nakusanya nyimbo za mazoezi asubuhi nilipata mbili
.naendelea
.ubarikiwe
 
Muziki: Mvua ya Joto

Mmmh! Leo nitaaandika haraka haraka maana kuna ndoto nataka niiote nikilala na ninavyojijua nikiandika taratibu siwezi kuiota hii ndoto. FYI, hii ndoto ni mwendelezo tu wa ndoto zangu nyingi ukiacha ile moja ambayo ilinipaga jina baya ugenini. Nitakwambia kuhusu hiyo ndoto siku moja labda ijumaa nikiwa niko tingasi, na itabidi nikueleze mapema kabla mjomba wangu hajanikumbusha. Kwanza nakusalimia sana na ama baada ya salamu ninakukaribisha tena kwenye kipengele hiki cha muziki, haijalishi unakipenda au kinakuchukiza lakini kwa kuwa wewe upo hapa basi hakijaharibika kitu.

Nikushukuru sana Tumosa kwa kudhamini magazeti, wageni waliposikia mama JJ ni nani mimi nimeona niwape nyeupe na nyeusi, shululu alimaanisha kuwa wewe ndo unayempa usingizi. Asante BlessedHope kwa sala za muda wote na ambazo kiukweli leo zimeongezewa nakshhi na Transcend pamoja na SHIMBA YA BUYENZE , mnafanya vema sana wadau. Mnajua huwa sichoki kuwashukuru aunty yangu Shunie kwa hadithi bila kumsahau aliye moyoni mwangu hadi najisahau kukutambulisha kwake, la habibt husna muba, anko wangu Lyon Lee hongera kwa kutaka kutenganisha ngao ya maji na ngao ya kidonge. Ninakushukuru pia kwa kuendelea na neno lako kuwa nikienda Kigamboni nguo zangu zilowekwe na zianikwe kwenye mvua. You made my day na smile nililokuwa nalo nakumbuka ulinilazimisha kutabasamu pale tulipokuwa Morogoro kwenye ile bar tuliyokunywa Safari lager na chapati

Muziki sasa, hebu nitarudi tena

Binamu santee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom