Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tuombe


Bwana Yesu asante kwa ljumaa njema ya leo.

Asante kwa ulinzi wako kwetu Mungu Mkuu

Umetulinda Jehova
Bwana wa majeshi

Ni wengi walitamani kuiona hii siku lakini hawakuweza kufika.

Tunaomba Toba kwa yote tuliyokukosea..ututurehemu twakusihi.

Baba siku ya leo ni siku ambayo wengi wanakuwa ktk maombi

Mungu ninakuomba ktk Jina la Yesu Kristo Maombi yetu Bwana yakawe ni manukato mazuri mbele zako.

Kumbuka wenye shida mbali mbali
Taabu na mateso na uchungu wa kila aina EeeMungu ukawakumbuke

Angalia ndoa ambazo hazina amani wala furaha

Mungu warudishie upendo wao wa kwanza

Ambao hawajakujua wewe Mungu wa kweli katika Yesu Kristo Bwana ukawaokoe.
Kumbuka wamama wanaohitaji Watoto
Bwana ukafungue matumbo yao.
Wanafunzi, wagonjwa ,Yatima ,wagane na wajane
Wakumbuke Yesu

Nimeomba haya nikiamini yamekuwa ni katika Jina la Yesu Kristo wa Nazareth
Amina aaaa.!!!!!.

SIKU NJEMA WAPENDWA
Amina, na kwako pia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom