Makapuku Forum

Makapuku Forum

Inaendeleaaaa. ...


"Basi twende wote mtoni German."
"Hapana Twaha. Huu ni wasaa mzuri wako kuweza kusoma kwa utulivu hilo daftari. Naamini nitaporudi kuoga utakuwa ushamaliza. Hapo tutakula magimbi kisha nitakufafanulia hiyo picha naamini kiu yako itaisha." Alisema German na kunifanya nitabasamu. Nilijituliza mkekani na sasa nikawa tayari kufungua kurasa moja baada ya nyengine kusoma daftari lile ambalo nje liliandikwa MIAKA 12 YA MATESO. Nilishusha pumzi na kutuliza akili kichwa kusoma kilichomo. Hakika nilisisimka na kila kilichoandikwa katika kila kurasa. Daah! Hakika ilikuwa miaka kumi na mbili ya Mateso yaliyobeba matukio ya kushangaza ndani ya maisha ya babaake German Machine.

||................||
Wakati wimbo wa maombelezo ukiendelea huku mawazo yameniteka kurudi miaka 12 nyuma, mara sauti ya Tina ilinivubua mawazoni.
"Twaha....Twaha...!" Aliniita huku akinitingisha mkono. Nilizinduka kama mtu aliyetoka usingizini nikiwa nimesimama.
"Usiwaze sana Twaha, naona fikra zako zimehama sana.!"
"Hapana Tina niko sawa tu. Tuko pamoja." Niliongea huku nikiitoa leso na kufuta machozi ambayo bado yalikuwa hayakomi kutoka. Muda huo msoma ratiba ambaye alikuwa mchungaji maarufu nchini alisimama na kuutangazia umati kwamba ule muda wa kusomwa historia ya marehemu umewadia.
"Hivi Twaha! Mbona German hakuwa na ndugu kipindi tunamfahamu? Au wewe uliwajua ndugu zake?" Aliniuliza Tina akionesha mshangao baada ya kusikia anakaribishwa mwakilishi wa familia kusoma historia ya maisha ya marehemu German Machine.
"Hapana Tina! hata mimi sijawahi kumjua ndugu wa German Machine." Nilimjibu huku nami nikitazama pale jukwaa kuu nikiwa na shauku ya kumjua huyo ndugu mwakilishi wa familia ya German Machine aliyetakiwa kusoma historia hiyo kwa ufupi.
"......Wapendwa katika jina la bwana, Mungu azidi kuwatia nguvu na utulivu. Sasa tusikilize historia ya maisha ya mpendwa wetu kwa ufupi. Na atakayesimama kuiwakilisha familia ni Profesa Robert Lahm Kepler kutoka Ujerumani."
Mchungaji alipotamka jina la mwakilishi wa familia kila mtu alishangaa kuona kwa mara ya pili akisimama mjerumani mwengine baada ya yule wa kwanza aliyefungua sala. Wengine walianza kunong'ona kuwa msiba unafanyika Tanzania lakini umetawaliwa na wajerumani tena mbele ya Rais wetu? Wengi walitarajia mwakilishi wa familia angesimama Mtanzania. Hata Tina alionesha mshangao kama ilivyokuwa wengine. Lakini binafsi sikushangazwa kuona Mjerumani akitajwa kusoma historia ya German Machine. Ila kilichonistua na kunishangaza ni jina la mjerumani huyo.
"ROBERT LAHM KEPLER!" Nilistaajabu huku macho yangu yakigota kwa mzungu yule mrefu mwenye nywele za kahawia punde aliposimama kuelekea panapo vipaza sauti tayari kwa kusoma historia fupi ya marehemu. Sikuamini kama nimefanikiwa kumjua Robert Lahm Kepler kwa macho. Jina lake halikuwa geni kabisa. Nilipozidi kumtazama usoni nilijikuta nahama tena fahamuni mpaka siku ya kwanza kulijua jina lile. Ilikuwa ni siku ile nilipoachwa na German Machine nisome daftari la marehemu baba yake lililoonesha miaka kumi na mbili ya mateso. Daaah! kupitia lile daftari ndipo nilipomjua Robert Lahm Kepler ambaye sikuwahi fikiria kama nitakuja kumuona kabisa machoni. Kumbukumbu zikanirudisha tena nyuma nikasafiri kimawazo mpaka ile siku.
* * * *
||MIAKA 12 NYUMA||
Baada ya German kuondoka kwenda kuoga mtoni, ndipo nilipokaa mkao wa kumakinika na kulifungua lile daftari. Moyo ulikuwa ukinipiga kwa shauku ya kujua kilichomo hasa baada ya kusoma kichwa cha habari nje kilichoandikwa miaka kumi na mbili ya mateso.
Nilishusha pumzi na kufunua ukarasa wa kwanza. Ingawa daftari lilichakaa lakini mwandiko ulikuwa bado unasomeka vyema. Nilishangazwa kwanza na hati nzuri ya mwandiko uliopangwa vyema na kubainisha kila tukio na mwaka. Nilianza kusoma kwa umakini bila kupepesa wala kuruka kurasa hata moja.
--------------
|MIAKA 12 YA MATESO|
=>Sura ya Kwanza<=
*JUNE 2063//2069*
|__|__|__|__|__|
Mnamo mwezi wa sita mwaka elfu mbili na sitini na tatu, ndipo nilianza kuchora kwa mara ya kwanza nikiwa na miaka 44. Sikuwahi kufikiri kama mimi ni mchoraji lakini siku hiyo nilishangaa kujikuta nimechora picha ya mtu. Ilikuwa ni ndani ya jiji la Dar es salaam. Jiji ambalo nililijua vizuri kila pembe kutokana na maisha yangu ya mtaani. Mimi ni mtoto niliyekua katika mazingira magumu ya mtaani baada ya kutelekezwa na wazazi wangu. Sikuwahi kuwajua ndugu zangu kama ilivyokuwa kwa mke wangu. Mwanamke ambaye tulikutana mtaani pia. Hakuwa na ndugu kama mimi. Sote hatukuwahi kusoma na tulichukuana kuishi pamoja tukitanga na kuganga mpaka tulipoweza kupanga chumba jijini. Kipindi nilipoanza kuchora mke wangu alikuwa na miaka 30. Mpaka muda huo hatukuwahi kupata mtoto. Picha niliyochora siku hiyo ilipendwa na kila niliyomuonesha hasa mke wangu. Picha ya mzungu mwenye ndevu nyingi ambaye sikuwahi kumuona popote wala kumfikiria kipindi nikimchora. Mke wangu alinishauri kuwa sasa niache wizi na nitumie kipaji kilichojitokeza ukubwani huenda kitatukwamua kimaisha. Wizi na utapeli ndiyo kazi niliyoitegemea jijini. Hata karatasi na rangi zilizonitia ushawishi wa kuchora nilizipata kwenye 'stationary' moja ambayo tulivunja na kuiba nikiwa na wenzangu. Awali nilipuuza ushauri wa mke wangu lakini ule mchoro aliutunza kwa kuununulia flem maalum ya kioo. Hakika ulipendeza lakini nilishindwa kujitangaza kuwa mchoraji kwa kuwa hata mimi sikujiamini kama naweza kuchora. Kila nilipojaribu kufikiria kitu cha kuchora sikuweza kuchora vizuri. Lakini nilipojichorea tu bila kufikiria wala kujali nilishangaa mwishoni mwa mchoro nimechora kitu kilichoeleweka. Kwa mara ya pili hali hii ilijitokeza mwaka 2064 nilipomchora mtu mwengine. Lakini ajabu naye alikuwa mzungu kijana asiye na ndevu na nyuma yake nilichora bendera na kupaka rangi nzuri zilizomvutia yeyote aliyeutazama mchoro wangu. Nilijiuliza kwanini nawachora wazungu? Na hawa wazungu kina nani? Hata mke wangu alishangaa kwa kuwa nilishindwa kumchora yeye alipotaka lakini niliweza kuwachora watu ambao sikuwahi kuwa nao karibu. Kuna rafiki yangu mmoja ambaye yeye alisoma kidogo ingawa naye alikuwa mwizi kama mimi. Nilipomuonesha mchoro ule alishangaa na kunambia kitu kimoja tu. Kwamba nimemchora mzungu na bendera ya ujerumani. Akanishauri ule mchoro kama nitawaonesha wazungu wanaweza kunipa hela lakini kwa waswahili wataishia kunisifu kwa maneno tu. Niliifanya kazi hiyo ya kuzurura na picha yangu mpya ya mzungu aliyesimama nyuma ya bendera niliyoambiwa ni ya Ujerumani. Kila nilipokutana na mzungu nilimuonesha ule mchoro na kumuashiria kuwa nataka pesa. Sikujua kuzungumza lugha yoyote zaidi ya Kiswahili. Tena kiswahili cha mtaani. Lakini mwaka mzima nilizunguka kuwaonesha wazungu niliobahatika kukutana nao bila mafanikio ya kuuza ule mchoro zaidi walitabasamu na kuniacha patupu. Nilikata tamaa lakini mke wangu alinipa moyo na kunishauri niende Bagamoyo ambapo kuna wazungu wanaopenda kazi za sanaa. Ingawa nilisita awali lakini mwishowe nilikubaliana na mke wangu na kuubeba ule mchoro mmoja wa mzungu kijana. Nilisafiri mpaka Bagamoyo maeneo ya sanaa nikiwa na picha ya mchoro wangu. Hakika kitu ambacho sikukitarajia kutokea ndicho kilichotokea. Nikiwa njiani natembea kuelekea kaole Bagamoyo nilipishana na wazungu wawili wakitokea ufukweni. Nilipomtazama mzungu mmoja moyo ulinipasuka sana na kustaajabu. Alifanana sana na mchoro wangu ambao ulikuwa ndani ya mfuko wa rambo niliobeba. Nilisimama na kumtazama kwa umakini. Hakika alifanana sana na yule niliyemchora. Hapo nilijikaza na kuwafata wale wazungu na bila kusema kitu niliwatolea ule mchoro na kuwakabidhi. Hakika nao walionesha kustushwa na kustaajabu. Moyo wangu ulifurahi nikajua sasa nisharamba dume. Huo ulikuwa ni mwaka 2066. Mwaka wa maajabu nilipokutana na ROBERT LAHM KEPLER. Mzungu niliyemchora bila kumjua wala kumuona. Hakika yeye ndiye aliyekuja kuwa chanzo cha mengine yote kutoka maisha mabaya hadi kuwa mabaya zaidi ingawa haikuwa chaguo lake.
 
ZABURI 121

5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

NAWATAKIA JUMAPILI NJEMA NA IBADA NJEMA NAWAPENDA MJUE... MJIPENDE ZAIDI KWA KUUTAFUTA UFALME WA MUNGU KWA BIDII..SHALOM SHALOM
 
ZABURI 121

5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

NAWATAKIA JUMAPILI NJEMA NA IBADA NJEMA NAWAPENDA MJUE... MJIPENDE ZAIDI KWA KUUTAFUTA UFALME WA MUNGU KWA BIDII..SHALOM SHALOM
luv u too mom
 
ZABURI 121

5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

NAWATAKIA JUMAPILI NJEMA NA IBADA NJEMA NAWAPENDA MJUE... MJIPENDE ZAIDI KWA KUUTAFUTA UFALME WA MUNGU KWA BIDII..SHALOM SHALOM
Ahsante n kwako pia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom