MARA YA MWISHO SIMBA KUCHUKUA UBINGWA:
1. Sukari kilo ilikuwa 700.
2. Ze comedy ilikuwa eatv.
3. Leicester city ilikuwa champion ship(Division 1 League)
4. Diamond bado alikuwa tandale.
5. Nauli ya daladala ilikuwa 300/=
6. Flat screen na smart phones hazikuwepo.
7. Sudani kusini ilikuwa siyo nchi
8. EAC ilikuwa na nchi tatu tu
9. Papa Francis alikuwa bado Kardinali tu
10. Osama Bin Laden alikuwa bado yuko hai
11. Al Shabab ilikuwa haijaundwa
12. Uhuru Kenyata alikuwa hajawa rais
13. Magufuli alikuwa hajawa raisi
14. Kinana alikuwa hajawa katibu mkuu wa CCM
15. Dr. Slaa alikuwa bado katibu mkuu wa CHADEMA
16. Zito Kabwe alikuwa bado naibu katibu mkuu wa CHADEMA
17. ACT na ADC zilikuwa hazijazaliwa
18. TV za analojia zilikuwa bado zinafanya kazi
19. Sep Blatter alikuwa bado raisi wa FIFA
20. Tenga alikuwa bado raisi wa TFF
21. Dionizi Malinzi alikuwa bado mwenyekiti wa BMT
22. Barabara za mabasi yaendayo kasi hazikuwepo Dar
23. Daraja la Kigamboni halikuwepo
24. Mbeya ilikuwa haina hata jengo moja lenye lift
25. Uwanja wa ndege wa Songwe ulikuwa haujazinduliwa
26. Mwanza ilikuwa haijapata taa za kuongozea magari barabarani.
27. Mbeya City ilikuwa haijaundwa
28. FastJet ilikuwa haijaanza kuendesha biashara zake nchini Tanzania
29. Nokia ilikuwa ndiyo bado simu bora kabisa
30. Gesi ya Mtwara ilikuwa haijaanza kuchimbwa
31 - 100 zitaendelea toleo lijalo.
......................