Makapuku Forum

Makapuku Forum

9/Diane Schuur
29f084d5519b68813cfdff19c1485466.jpg
21b9790ea7b6c8401d524598cb208c51.jpg
9d4fa9fa7e0a67528c449bba492ee1b2.jpg

Alizaliwa Disemba 10 mnamo mwaka 1953
Huyu ni kipofu mwingine mjanjamjanja ambaye anakimbiza tu kwenye muziki wa Jazz yaani huyu kwa wasioona ndiye Madonna wao
Siyo tu anafanya muziki kutafuta sifa bali anaingiza mpunga wa maana kupitia sanaa
Huyu amenyanyapaliwa sehemu kibao ila akakomaa nao na kuwadhihirishia kwamba kukosa macho/kuona sio kukosa akili na kipaji
Kapiga ngoma kibao kama vile
Louisiana Sunday Afternoon
Deedle's Blues
Easy To Love
TheMan Ilove

Ana album 23 na zinskimbiza tu sokoni na kuongiza mpunga The Man I Love
.....

Asantee
 
8/David Paterson
7e45a2092e4c17a2dd149febefcc9b53.jpg
2420594bc117726b51df5fc0a777f271.jpg
534e3ac1cad099c597c8dc7b4a3d4d6a.jpg
Alizaliwa Mei 20 mwaka 1954
Mlemavu huyu wa macho aluamua kujikita kwenye siasa na kufanikiwa kuwa Gavana huko Marekani
Alikuwa Gavana wa 55 wa New York yaani aliliongoza moja kati ya jiji la maana kabisa huko Marekani....ni bora huyu mlemavu mwenye busara kuliko kuongozwa na Bashite !!
Aliliongoza jiji la New York kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2010
Ni msomi kutoka Colombia University na hakuridhika hivyo akaenda kumalizia na shule ya sheria (uwakili) huko Hofstra Law School :
Huyu ni Mmarekani mwenye asili ya Afrika kama Barack Obama na mpambanaji haswa na alisifika kwa hotuba zenye kuvutia
.......

Hawa ni miongoni mwa watu wanaojitambua.... Kwanza amejikubali, na akasonga mbele
 
7/Helen Keller
a0a42f251cfeaa2fa56b7d4d0388ef66.jpg
3f024c3dcf129a3548a1d9009a87f3c6.jpg

Ni mzaliwa wa Alabama
Alizaliwa mwaka 1880 na kufariki dunia mwaka 1968 akiwa na umri wa miaka 88
Huyu sio tu alikuwa haoni bali pia hasikii kitaalamu wanaitwa Kiziwi asiyeona ukienda pale shule ya Uhuru Mchanganyiko utawakuta watoto wa aina hiyo hawa kueafundisha ili wakuelewe ni jambo gumu linalohitaji moyo na kujitolea
Sasa huyu pamoja na hali yake alikomaa na shule na kufanikiwa kuwa Kiziwi asiyeoona wa kwanza kupata Shahada ya Sanaa yaani alikomaa na nukta nundu tena bila kumsikia mtu hadi chuo kikuu !!!
Huyu alikuwa ni Mhadhiri &Mtunzi
12d211f08e6ca70b1bb1a6a80575d6b8.jpg
8d5165b903205c9ab20670fc8355f3e0.jpg
054d9be0f15e834cf3957b455d676501.jpg
c3f72047efe8791c19a1717a68de345b.jpg

Kaandika vitabu kibao vilivyotikisa na kuishangaza dunia
Huyu ndiye kiziwi asiyeona maarufu zaidi duniani
.......
Aiseee!!!
 
6/Jose Feliciano
7b4aab9675e34f84aa459269dccdd255.jpg
7bcfcf9b8dabeb19b978464369574b7d.jpg
666ba94c0f40e5dad4154346b54ed0db.jpg

Alizaliwa Septemba 10 mwaka 1945
Huyu ni msanii kutoka Puerto Rico
Ni mwimbaji na mtunzi/mwandika nyimbo mwenyenye mafanikio makubwa nchini humo na duniani kwa ujumla
:
Wimbo wake wa Feliz Navidad unakimbiza duniani kwa ujumla kila unapofika msimu wa sikuu ya Christmass
Jamaa anaimba kwa kutumia lugha za Kilatini na Kiingereza hivyo kufanikiwa kuliteka soko
Nyimbo zake nyingine ni kama vile
Su Hija Me Gusta
Light My Fire


.
.......................................
Zitaendelea baadaye

Kama usingeuweka basi ningemuomba Obe auweke hata kama sio msimu wa sikukuu
Cc ankali shululu ngoma yako imewekwa hapa!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom