Ukimwangalia vibaya akiwa chumbani kwako unaweza kufikiri mtu kadondosha mguu wake wa tatu
Tafsiri rahisi ya naked ni uchi sasa jamii hii ya panya hawana mabyoya hivyo ni kama watu wasiovaa nguo pia wanafanana na uume
Hawa wana macho ila hawapni au pengine uono wao ni hafifu sana yaani hata papai tu hawalioni
Wanasayansa na watafiti wamejaribu kuwaweka kwenye giza na mwanga lakoni hawa panya hawakuonesha tofauti yoyote
Yaani wanategemea milango mingine ya ufahamu badala ya kuona/kuangalia vitu
......
Salamander ni jamii ya amphibia ila mwonekano wao ni kama mijusi reptilia
Sasa hapa nawazungumzia Texas Blind Salamander ambao kama jina lao linavyoonesha wanapatikana huko kwa Trump
Anapatikana kwenye maji ya chinichini(underground) na hupendelea kukaa kwenye mapango
Anatumia mgandamizo /shinokizo la maji(water pressure) kujongea pamoja na kuwinda badala ya macho
Kwa Wachina Salamander ni chakula kitamu na huongeza pilipili na kachumbari pembeni
Huko wapo wa jamii nyingine tena wakubwa balaa kumzidi kenge
.
.....
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.