Makapuku Forum

Makapuku Forum

762b4f648bff7f6af91665a4950a210a.jpg
55c06662e1fd96295664ec3dfd54c34d.jpg
02ab06c3ee326d5c3d82263c826b53f4.jpg
d813ca6514852718a30f5db07cf86f8f.jpg
0e547a8e3c43d1ad6b0ec25e225faded.jpg
c9cf6451913516a1bb3cddc9fb23d037.jpg
39d9341ab3157dcb038acafb9b4b7f06.jpg
517c01d3b22cc564c44cb4642c1454a6.jpg
6ee1b299aee8544aa27beed1c19733f1.jpg
cea02784b6664111bf7c923e807f99fd.jpg
acc90a6a9df03ed987b9fd97c73477ba.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahaaa
Siku hizi ishakuwa balaa afadhali hata upige stori na demu maana atakutunzia siri na utamu pia unaweza pata kuliko kidume mwenzio hasara itakuwa X 2


.......


Na wanaume wambea ni wavivu wavivu tu kutwa kwenye kahawa,bao hakuna wanaloliwaza....



post using my macbook air using jamiiforums app
 
Wale wa simulizi yetu ....amka nayoo

.... Siku hiyo tofauti na siku zote Kamishna Shebby alitoka alfajiri sana majira ya saa kumi na moja kasoro na baada ya Kamishna Shebby kutoka tu ndipo Asha alipoamka haraka na kuchukua simu yake na kupiga tena ile namba ya siri aliyopewa na Cj4 kule hospitali kwa shauku akiwa anataka ushauri kwa Cj4 nini afanye juu ya ukweli anaouficha kwa mumewe juu yake na mr X.
["Hallow kaka Inspekta"]
aliongea Asha mara baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
[["Lady Ninja, leta ripoti ulichopata."]]
ilisikika sauti upande wa pili na kumfanya Asha ashushe kwanza pumzi baada ya kuona yule mtu ambae yeye alikuwa anadhani ni Inspekta kuwa anajua mengi sana kuhusu yeye hasa baada ya kusikia anamwita Lady Ninja.
["Naomba unisaidie ushauri kwani natamani kumwambia ukweli mume wangu lakini nahisi huu ukweli unaweza kuwa ndio mwisho wa upendo baina yetu isitoshe nami nampenda kweli sasa. msaada tafadhali huu uongo unaniumiza nafsi"].
[["Hupaswi kuwa na haraka kumwambia sasa, unachotakiwa uwe unakwenda mara kwa mara kule kwa wakwe zako naamini sasa Mr X rada yake haipo kwenu kwanza ipo kwa babaako."]]
aliongea Cj4 na kumpa maelekezo yale Asha ambae aliyakubari kwa moyo mmoja na baada ya kukata simu alianza kutafakari yale maneno ya Cj4 kuwa kwanini Mr X sasa hana habari na wao bali ataendelea kwanza kudeal na Hussein ambae ni babaake aliyekuwa kule kwenye Jumba kubwa la mzee Mwinchande?
("Mr X sawa anadeal na babaangu, lakini kwanini Inspector ananambia niende mara kwa mara?! Mh!! nina wasiwasi na haya maneno kitaalam kama anamaanisha mr X hayuko mbali na pale..!")
aliwaza Asha baada ya kukata simu.

Wakati huo nae Shebby alikuwa njiani akienda huko huko kwa Cj4 kama kawaida toka amefariki Kimaro na kupona kwake mguu hakutaka kabisa kuendeeshwa hata alipobembelezwa na serikali kutokana na heshima aliyokuwa ametunukiwa lakini alikataa katakata na alifanya hivi kutokana na mission zake za siri sambamba na Cj4.
Shebby akiwa kwenye gari yake mawazo yote alifikiria sana mazungumzo ya mkewe na aliona kama kulikuwa na kitu cha zaidi alichotaka kusema yule mwanamke lakini alighairisha ghafra na kuzuga story nyengine na kumbe Shebby hata alivyokuwa anamuitikia haikumaanisha alikuwa hajastukia kama kuna kitu Asha alikuwa ameficha lakini alichofikiria kwa nini anaficha?
Lakini kwa kuwa alikua na mtu wanaesaidiana kwenye mission yao ya kumnasa mr X na kwa sababu ya kuamini huyo mtu ana uwezo mpana sana wa mbinu na fikra aliamua kwanza kukutana nae alfajiri amuelezee na kile alichokuwa anakihisi yeye ili wapate ufumbuzi zaidi wa mambo.

Ulikuwa ni ujanja wa Cj4 alioutengeneza kwa Shebby na Asha na sasa ilikuwa ni yeye tu anawacontrol wote wawili pasi na kujitambua wenyewe.
Asha ametoka kuongea nae na mara alipokata simu hazikupita dakika ishirini na Shebby nae aliingia.

* * * *

"Asalamu alykum bwana, swala muda ndio huu Mwenyezi Mungu anatuamuru tuamke tumuombe nae atatujibu..."
aliongea mzee Mwinchande mara baada ya Hussein kufungua mlango na kutoka.
"hahaaa Kweli kabisa daah!"
alijibu Hussein kwa kujichekesha machoni lakini moyoni alikuwa na hasira kupita kifani juu ya mzee Mwinchande baada ya kumgundua kuwa ndie alikuwa mr.X mwenyewe.
Lakini kilichomsaidia Hussein ni vile jinsi alivyoweza kuyaficha ya moyoni na kuvaa uhalisia wa kitu tofauti kabisa na hii kwa kuwa alijua mtu hatari mr X yupo mbele yake kwa hiyo itakuwa hatari zaidi kama akiwahi kugundua yaliyo moyoni mwake.

Walisimama sehemu ile ya kusalia na mzee Mwinchande alisimama mbele yake akiwa ndie Imam (kiongozi wa sala) huku Hussein bubu akisimama nyuma ya mzee Mwinchande akiwa maamuma (muongozwaji wa sala) na hapo ndipo Mwinchande alipofungua sala.
"Allaaaaaaaahu Akbaaar." (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa)
alitamka mzee Mwinchande na Hussein aliongoza vile japo moyo ulimuuma na kujikuta machozi yanaanza kumdondoka tena kipindi Mwinchande akisoma pale mbele kuiongoza sala yao.
("Yaaani nakubali kabisa kusalishwa na adui yangu? Yani eti nimuombe Mungu pamoja na adui yangu tena yeye ndie awe ananiongoza kumuomba Mungu? hapana... Hapanaaa")
aliongea mwenyewe Hussein moyoni mwake huku akimuangalia mzee Mwinchande kwa hasira pale mbele akijaribu kutafakari nini amfanye ili aweze kutimiza azma yake na nafasi aliyoiomba zaidi ya miaka ishirini?
Nafasi ambayo aliona ndio ile leo hii iko mbele yake na mr X adui yake aliyesubiri muujiza wa kumjua utokee kwa miaka mingi na sasa imekuwa hivyo yuko mbele yake na amempa kisogo.
("Inawezekana bahati hii nisiipate tena akaja kuniwahi huyu mshenzi.")
alifikkiria tena Hussein huku akigeuka geuka kutazama maeneo yale yalivyokaa kaa akiwa kama mwenye kutafuta kitu wakati sala ilipokuwa inaendelea na alijua kwa upande wake lile jambo la kugeuka geuka tayari lilikuwa lishamuharibia sala lakini aliona yuko sahihi kwani hawezi akasalishwa na shetani harafu hiyo sla ifike kwa Mungu.

Aliamini kabisa mr X ni shetani wala hapaswi kabisa kuishi na aliamini kuwa asingeweza kuendelea kuvumilia kwa siku tatu zaidi bila kustukiwa na mr X kilichokuwa moyoni mwake.
Na katika kugeuka geuka kwake hatimae alibahatika kukiona alichokuwa anaaangaza angaza macho kukitafuta na hakikuwa chengine bali ni kipande cha chuma kilichokuwa kinatumiwa kwaajili ya kupasulia nazi na alikiona jana yake usiku pindi yule mfanyakazi wa ndani alipokisahau kukirudisha sehemu husika mara baada ya kukitumia kipindi akiangalia filam kwa sebuleni na kukisahau juu ya sink dogo karibu na mlango wa jikoni nyuma kidogo na eneo walilokuwa wanasali.
("Shabbashhhhhh, najua hii yote ni Mungu amemfanya yule bint kukisahau na kunikumbusha mimi nikitumie kama silaha ya kummaliza adui wa watu aliyesimama mbele yangu")
aliongea Hussein wakati huo walikuwa wamesimama tena baada ya lakaa (sujuda) ya kwanza ambapo mzee Mwinchande akiwa hana habari aliendelea kusoma kwa madaha kabisa taratibu bila kujua wala kuhisi nini kinaendelea nyuma yake ambapo Hussein bubu alikuwa ananyata taratibu sana kinyume nyume hadi kulipokuwapo kile chuma na kukikamata kwa nguvu na kuanza kunyata tena kumsogelea mzee Mwinchande huku mapigo yake ya moyo yakizidi kasi kadri alivyozidi kupiga hatua hadi alipofika mita chache kabisa na kujiandaa kwa nguvu zote kumshambulia adui yake.
("Leo ndio Historia inaandikwa.")
aliongea kimoyo moyo na kujihesabia mwenyewe Hussein lakini mara ghafra alistuka kusikia sauti ya miguu ya mtu akishuka ngazi kwa haraka kutoka juu kuja kule sebureni tena akiwa anakimbia.
...

Mume wanguuu Mume wanguuuuuu Babaaaaa......"
alikuwa ni Zainab mamaake Kamishna Shebby akikimbia kuwahi kule chini mara baada ya kuona kinachotaka kutokea kupitia kwenye screen yao maalum iliyokuwa chumbani inayoonesha maeneo ya nyumba ile kupitia kamera ndogo zilizotegwa kila kona kwaajili ya usalama na kurekodi kila kinachoendelea mule ndani.

Lakini pindi anatoa ule ukelele kumpa tahadhari mzee mwinchande ambae alikuwa anajiandaa kusujudu ndipo Hussein bubu alipowahi kwa kumtandika vyuma vya kichwa mfurulizo na kwa nguvu zote.
"KUFAAA KUFAA KUAFAA"
Alipiga kelele Hussein kipindi anamshambulia mzee Mwinchande kwa nguvu zote mpaka walipodondoka pale chini ambapo kwa sekunde zisizozidi arobaini tayari damu nyingi zilikuwa zinamvuja mzee Mwinchande aliyekuwa anapapatika sebule nzima huku Hussein bubu akiwa kamng'ang'ania bado anampelekea dozi ya kutosha kwa kumpiga kwa nguvu na kile chuma hali iliyosababisha sasa damu kuwa inamrukia Hussein na mbaya zaidi alianza kupasua hadi fuvu la kichwa.
"Hoooooooooooooooooooooooooooooooooo..."
alipiga kelele na kuanguka pale mwisho wa ngazi Zainab huku akiwa haamini kile alichokuwa anakiona kikitokea mbele ya macho yake.
"Uuughhhhrrrrr..Ughhhrrrrrr.."
alikoroma koroma kwa nguvu Mwinchande kila Hussein alivyokuwa anamporomeshea kipigo cha kihistoria.
"Kufaaaaaaa Mshenzi weweee kufaaaaaaaa, Kufaaaaaaa"
alikuwa nusu kapagawa Hussein na alizidi kupata nguvu pindi alipokuwa anatoa dozi kwa mzee Mwinchande ambae sasa alionesha wazi tayari alikuwa anamalizikia roho huku akiwa amepasuka vibaya sehemu za kichwani na paji la uso damu zikiwa zimetapakaa sehemu ile ya kusalia hadi maeneo ya jikoni katika kikirikakara zilizokuwa zinaendelea.

Kelele za Zainab na Hussein ziliweza kumuamsha dada wa kazi aliekuwa chumba cha chini karibu na jiko ambapo alipotoka hakuamini kile kilichokuwa kinaendelea mara baada ya kumshuhudia Hussein bubu akiwa anamshambulia kwa nguvu zote mzee Mwinchande pale chini huku kwa mbele maeneo ya ngazi zilizoelekea vyumba vya juu alionekana mamaake Kamishna Shebby akiwa ameanguka huku kaishiwa nguvu akilia bila kutoa sauti.
Ubaya wa nyumba ile ilivyotengenezwa ni kuwa na vioo vya tinted pia madirisha yalikuwa hayafunguliwi kutokana na AC iliyokuwa inawashwa masaa 24 na kama ukitaka upepo halisia unapandisha sehemu za juu kabisa, na kwa sababu hiyo hata walinzi waliokuwa nje hawakujua chochote kilichokuwa kinaendelea ndani.

["Hlloooo, halloooooo, halooo kakaa shebiiii babaaa hukuuu aaaah muwahi babaaaaanakufaaaa... "]
aliongea huku nae akilia yule msichana wa kazi mara baada ya kukimbilia tena ndani mwake na kuamua kumpigia Kamishna Shebby kumpa taarifa ili awahi kuja kutoa msaada kwa kile kilichokuwa kinaendelea pale.
"HAHAHAHAHAHAHAHAAAAA"
alicheka kwa nguvu Hussein mara baada ya kuona Mzee Mwinchande katulia na kaacha kupapatika.
"hahahahahahahahahahaaaaa"
Alicheka tena huku safari hii akimpiga piga kwa nguvu sehemu za mdomo na kuanza kumvunja meno bila kujali hata zile damu zilizokuwa zinamrukia huku akiwa na Furaha ambayo toka anaingia Jera hajawahi kufurahi kwa nguvu Hussein kama siku hiyo.
"ASANTE BABA MUNGU"
Aliinua kichwa juu na kushukuru Hussein bubu kwa kuona ile ndoto yake na maombi kuwa aje kumuua Mr.X kwa mikono yake muda ule ilikuwa imetimia na hatimae kweli Mzee Mwinchande ambae ndie alikuwa Original MR.X aliuawa kwa mikono ya Hussein babu bubu baada ya usumbufu wa zaidi ya miaka 28.
Baada ya Hussein Kuhakikisha hakuna Jipya tena kwa Mr X aliinua uso wake na kumtazama mama Shebby pale chini ambae alikuwa amekosa nguvu kabisa hakuweza hata kunyanyuka zaidi ya kuwa anasota kuelekea juu ya ngazi zile kwa hofu huku akilia mara baada ya kumuona Hussein amenyanyuka kwa hasira na macho yote alikuwa kayaelekeza kwake.

* * * * *

"Leo kuna kitu kimoja tu, kilinichanganya kuhusu mke wangu."
alionekana Kamishna Shebby akiongea na Cj4 kwenye sehemu yao maalum waliyokuwa wanakutana kwa mazungumzo pasi na mtu yeyote kuona.
"Kitu gani hiko?"
aliuliza Cj4
"Kwenye mazungumzo yake nikiwa kama askali mzoefu sasa niligundua kuna kitu ananificha kinachonihusu kabisa"
"Mh! hebu nipe nukuu yake."
"Alianza maongezi akiwa makini na kunimaanishia kuwa niamini kama ananipenda, lakini alivyoendelea alinambia kuwa ila anaona hastahiri mimi kumpenda vile na nilipomuuliza sababu akanambia ana wasiwasi kwa vile ninavyompenda kuwa sitompenda hivyo siku zote. Nilipomuuliza kwanini ana wasiwasi huo ndipo akanambia kuwa anahisi kuna siku nitakuja kumchukia sana na hata kumuua.... Dah! hapa ndipo nilipochoka na kuhisi lazima kuna kitu tu. Hawezi kuanzisha mada yenye maneno makali kama yale yaani mimi Nimuue mke wangu mwenyewe?"
aliongea Shebby wakati huo Cj4 alikuwa anmsikiliza kwa umakini mkubwa.
"kwa hiyo hukumuuliza kwanini amefika mbali hivyo?"
"Nilimuuliza kiongozi."
"Akasemaje"
"aagh! jibu lake nililiitikia tu lakini halikuwa na ukweli wowote nilijua tu ni Zuga"
"sawa aliemaje?"
aliuliza Cj4 lakini wakati Shebby anataka kujibu mara simu yake ambayo ilikuwa na line ile ya nyumbani tu ndipo ilipoita na kuipokea ambapo sauti ya upande wa pili ilimfanya abadilike ghafra uso.
"Vipi Shebby?"
"Kumekucha Mkuu Mr X ameamua kuivamia nyumba yetu alfajiri hii kule kwa mzee."
aliongea Shebby ndipo mkuku alikimbilia kwenye gari pamoja na Cj4 ili kuwahi nyumbani kwao ambako ilionesha wazi kuna matatizo mazito.
 
9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa;

Isaya 41 :9
10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

Isaya 41 :10
11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.

Isaya 41 :11
12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.

Isaya 41 :12
13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.

Isaya 41 :13
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom