Makapuku Forum

Makapuku Forum

Utusamehe deni zetu kama sisi nasi tuwasamevyo wadeni wetu

Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu, kwa ufalme wako ni wako na nguvu na utukufu hata milele Ameeen.

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nanyi

MATHAYO:6:12:15

Muwe na usiku ulio mwema


Tujifunze kusamehe wapendwa hata kama umekosewa vipi msamehe aliyekukosea ili Mungu atusamehe nasi tuliyomkosea nimejifunza kitu kutokana na neno la leo achia roho we samehe tu
91add5b4a66d6594187c875a9fe22055.jpg
 
Obe. Najua kuna kipindi nilikukosea sana. Naomba unisamehe mkuu. Moyo wangu ni mweupe. Kwako na wengine wote katika thread hii. Ukinisamehe nitafurahi sana!


Shimba, nilijua tunafanya utani, na huwa napenda utani na ilipozidi upande wako nilijisikia vibaya maana KF ni sehemu nzuri kila mmoja akiwepo.
Na mind you, kukosoana ni sehemu ya kueleweshana na makosa huwa na kosa pia.
Binafsi sijaweka wala sina kinyongo na kilichotokea as I know wewe ni gentleman. Tunakosea wote , kwangu sina nongwa na kama ulikwazika nami let's move on.
Tuna mengi ya kuifanya KF kuwa Jukwaa bora na hii inawekana tu ikiwa utakuwa mmoja wa member wake.
Pamoja sana
 
Aliumia sana Asha mara baada ya kukumbuka yote yale yaliyopita na kujikuta akilia kwa uchungu mno na kuijutia nafsi yake.
"Nilikuamini sana Mr X, siku zote nilijua wewe ndie mtu muhimu kwangu na umejitolea kufanikisha maisha yangu kuwa bora kumbe ulikuwa na vitu unavitaka toka kwangu na ulijua fika mimi ni nani na kwanini unanitumia. aaah!! Umenifanya kipofu wako kwa muda mrefu sana.. Nadiriki kusema wewe ni zaidi ya SHETANI. Ndio wewe ni Shetani Mr X shetani mkubwaaa na lazima Ufe kikatiri..."
Alinung'unika Asha huku akigugumia kwa maumivu na kuhisi kama nafsi zote za watu alizozikatisha uhai zimesimama mbele yake zikimshutumu na kumzomea.

Ukweli hakupanga mwenyewe kuwa na mahusiano na Shebby japo baada ya tendo lile la kikubwa walilofanya siku moja ndio lilichochea kasi zaidi na ashki ya kumpenda kweli Shebby.
"Nimeua weeeengi wasio na hatia kwa ajili ya Shetani mmoja!!? hapana sikubali kwa hili hata kidogo lazima Nilipe vifo vya watu wote japo nilivitenda mwenyewe kwa mikono yangu lakini nina sababu zote za msingi. LAZIMAAAAAA.."
Alizidi kupayuka mwenyewe Asha kwa hasira huku akizidi kupiga mateke vitu vilivyokaa jilani yake na kuchomoa connector zote zilizofungwa chumbani kwake zilizokuwa zinamuwezesha kuwasiliana na Mr. X baada ya Connector zote kuzima signal zenyewe automatic mara baada tu ya mr X kutuma ujumbe ule wa sauti akimcheka kwa nguvu na ndipo alizima kabisa mitambo yote iliyokuwa inamuunganisha na Asha.

Lengo la Mr. X ni kusambaratisha kila aliyekuwa na kisasi nae na hapo alitumia akili nyingi kutengeneza mchezo ule wa vipofu ambao wachezaji walimuhusudu bila kujua wanaomuhusudu ndie adui yao waliyepaswa wapambane nae na kwa kuwa walikuwa hawalioni hilo ndio maana mchezo wake akauita wa vipofu.
Alifikiria mateso mazito aliyokumbana nayo babaake.
Alikumbuka vifo vya wafadhili wake na kugundua kuwa yote ilikuwa ni trick ya kuingizwa ktk mchezo na Mr X akimtumia Tyga ambae pia aliamini kuwa amehadaika na mchezo wa Vipofu aliokuwa anaucheza mr X lakini kitu kimoja hakujua kabisa Asha kama yule mzee Aly77 aliyemuua kule Mkuyuni ni baba mzazi wa Tyga.

Alivalia mavazi yake ya kazi Usiku ule ule alikaa tayari kwa ajili ya kuianza kazi ya kumsaka Mr X na alijua wapi aanzie japo hakujua wapi amalizie.
"I Must Find You Mr. X"
Alijiapiza Asha baada ya kuyatinga mavazi yake ya Kininja na silaha zake zote muhimu usiku huo huo aliharibu kila kitu kilichokuwa kinamuunganisha na mr X mule ndani kisha akafanya uchawi wake wa Kininja na mara ulitokea moshi wa ajabu mule ndani akatoweka na kuibukia nje ya nyumba yao ambapo style aliyotembea nayo sasa hivi ilikuwa tofauti kabisa na awali kwani alienda mwendo wa haraka mno na sehemu zengine aliweza kudanda kwenye mistimu na kupita juu ya nyaya sa umeme pasi na kuonekana.

Asikwambie mtu hakuna Ninja aliyekamilika asiyekuwa na mazingaombwe na ndivyo ilivyokuwa kwa Lady Ninja Asha ambae alifundishwa mambo mengi na mzee wa Kijapani ambae alikuwa ni Full Ninja Master na aliyatii mafunzo na kuyafata kwa moyo wote huku uvumilivu akiuweka mbele na hiyo ndio ikawa sifa ya uwezo wa ajabu aliokuwa nao leo hii.
Aliamua sasa kujitolea maisha yake kupambana na mtu asiyefahamika anayetumia akili nyingi huku akiwa na wafuasi wasiofahamika.
Alijua ni hatari lakini alijiamini pia hakuifikiria kabisa ndoa yake iliyo mbeleni yeye na Kamishna Shebby wala hakuona umuhimu wake kwa wakati huo zaidi ya umuhimu wa kukatisha uhai kwa mtu aliyeamini ni Shetani aliyepindukia Mr X.

Safari yake ya wizi wizi usiku ule huku jiji likiwa limepoa kabisa ilimpeleka hadi maeneo ya mbagara na mbele yake aliliona jengo kubwa la hoteli ambayo alipangiwa babaake pale.
("Lazima nifanye mbinu nimuhamishe hapa baba kabla huyu Chizi hajatuma kinyago wake mwengine aliyempofua kuja kumaliza azma yake")
Aliwaza Lady Ninja Asha na kutoa tena ile dawa yake ya unga maalum ambayo akiishika kwa style maalum aliyofundishwa na kutamka maneno ya Mzimu wa Kininja aliyoyajua mwenyewe, basi hupotea na kuacha moshi mdogo eneo lile na hutokea mahala ambako alikukusudia akilini kabla hajafumba macho na kusema yale maneno.
Na ndivyo ilivyokuwa ambapo Asha alinuia na kuieka akilini picha ya nyuma ya hoteli ile ili iwe rahisi kuingia kimya kimya lengo kuu likiwa ni kumuhamisha babaake pale hotelini na kumpeleka sehemu nyengine ambayo aliamini inaweza kuwa salama ili amuondoe kwenye Rada ya Mr X.

* * * * * *

Kwa upande wa Cj4 yeye alikuwa ndani ya nyumba moja iliyokuwa jilani na ile hoteli alipokuwa amepangiwa Hussein babu bubu huku muda wote alikuwa makini mno na kila kitu kilichokuwa kinaendelea hotelini pale mara baada ya kutega kamera maalum ya kijeshi kwenye usawa wa dirisha lake na kuchukua upande wa V ya hoteli ile kwa mbele, pia kamera nyengine aliitega kwenye chumba cha guest iliyokuwa upande wa nyuma ya hoteli ile na kwa jinsi alivyoitega ilikuwa ngumu mno mtu kuona ama kujua na kwa kutumia kamera hizo mbili aliweza kurekodi kila kilichokuwa kinaingia na kutoka kwenye ile hoteli kwa kutumia compyuta yake aliyoiconect na zile kamera.

Usiku huo kama kawaida alikuwa anawascan watu aliokuwa anawatilia shaka na kuchukua picha zao pasi na wao kujua kila aliyekuwa anaingia au kutoka mule hotelini na kwa kutumia compyuta yake maalum aliyoiconect na zile kamera.
Vilevile kitu kilichozidi kuzipa upekee zile kamera za Cj4 ni setting zake za moja kwa moja pindi inapommulika mtu yeyote mwenye silaha ama silaha yoyote ilikuwa inatuma Alarm kwenye compyuta yake na kumpiga picha muhusika na kutuma moja kwa moja kwa mtaalam Cj4.

("Mh! kila kitu kipo sawa, mbona huu mchezo Mr X hauvagai au kashaustukia...!! Camoon Mr X")
aliwaza Cj4 pindi alipokuwa anacheki cheki jengo la hoteli hususani usawa wa ghorofa kilipokuwa chumba cha Hussein ambako napo kulifungwa kamera kwa siri na Kamishna Shebby ambayo ilikuwa inaonesha kinachoendelea mule ndani na kutuma moja kwa moja kwa Cj4 na kwenye simu ya Kamishna Shebby.
Yote hayo walifanya kwaajili ya usalama wa Hussein bubu na kumtega Mr X kwa kumtumia Hussein bubu kama chambo pale hotelini kwani walijua kuwa shabaha iliyobaki kwa Mr X ni kwa Hussein bubu tu na akifanikiwa kumuua na huyo atakuwa kamaliza kila kitu na kamwe hakutakuwa na sababu ya kumtaja wala kumzungumzia tena.
Lakini yote yale yalikuwa yanaendelea pasi hata na Hussein mwenyewe kujua japo na yeye alikuwa na kiu na shauku ya kumuua Mr X na kila siku alikuwa anasali ili utokee muujiza amuue kwa mkono wake Mr X.

Lakini Cj4 akiwa amejipumzisha baada ya kuangalia kona zote kuwa ni salama mara Alarm ilibeep ktk kompyuta yake kumuashiria kuna hatari katika zone moja ya eneo alilotegesha kamera na hapo ndipo kwa speed alifungua kuangalia na alimshuhudia mtu aliyevaa mavazi ya Kininja akiingia kinyemera kwenye nyuma ya jengo la hoteli kulipokuwa na bustani kubwa na tayari alishaua walinzi wawili pasi na eneo la mbele ya Hoteli kujua chochote.
"Karibu kwenye Mchezo wee Mbuzi"
aliongea kwa Hasira Cj4 na kuchukua Kisu chake kikubwa kilichokuwa na dira kwenye mpini wake sambamba na wire maalum wa silva kwa niaba ya kwenda kuoneshana kazi na yule Ninja aliyeamini ametumwa na Mr X na alienda pale kwa niaba ya kumaliza kazi aliyotumwa na Mr X nayo ni kummaliza Hussein babu bubu.

...... Ndipo muda ule ambo Cj4 anatoka na kuanza kupita Kikomando akichanganya na Uninja ndani yake alishangaa alipokuwa anakaribia kwenye ile bustani kukukuta kuna timbwili limeibuka lililomshangaza mno na lililomfanya kwanza ajibanze sehemu kulishuhudia mwisho wake utakuaje.
Naam lilikuwa ni Timbwili la Maninja wawili tena wote wakiwa wamevaa mavazi meusi yanayofanana sana.
Hali hii ilimchanganya Cj4 na kuamua kubanza pale kwenye moja mti uliokuwa kwenye ile bustani huku akiwa haelewi wapi ametokea Ninja mwengine wakati awali alimuona mmoja na je yule Ninja mwengine ni nani na kwanini wanapigana pale? Pia kati ya wale Maninja wawili yupi Ninja mwema na yupi Ninja m baya?
Alijiuliza maswali haya Cj4 ambayo hakujua majibu yake na alijua ni ngumu kujua majibu yake hadi atapozidiwa Ninja mmoja ndipo ataangalia yule mwengine atachukua maamuzi gani akimmaliza mwenzake, kama atachukua maamuzi ya kupanda kwenye hoteli kwa nia ya kwenda kummaliza Hussein bubu basi atadeal na huyo kwani ni mbaya lakini kama atachukua hatua ya kuondoka basi huyo atakuwa Ninja ambae hana chuki na mtu yeyote bali huenda kaja kutoa msaada kwa Hussein bubu ama alikuwa na kisasi na yule Ninja mwengine ambacho kaja kumlipizia.
Lakini pia alijiuliza Cj4 kama kuna Ninja kati ya wale anapigana kwa niaba ya kumtetea Hussein ni Ninja gani huyo? maana mission ya usalama wa Hussein ipo katika mikono yake na mikono ya Kamishna Shebby sasa huyo Ninja ametokea wapi? ama hakika Cj4 alipata mtihani wa maamuzi kipindi akiangalia ule mpambanu lakini pia aliamini katika moja ya mawazo yake basi kuna wazo sahihi kabisa kuhusu wale maninja waliokuwa wanaendeleza kasheshe pale bustanini.

Mapigano makali ya wale maninja huku mmoja akiwa mwepesi sana kuruka na kukwepa vidubwana alivyokuwa anarusha mwengine ambavyo vilikuwa vikimkosa vinazunguka na kurudi kwenye mikono ya mrushaji wake na katika harakati zile mara Ninja yule aliyekuwa anaruka mno alipokitwa na kile kidubwana kimoja maeneo ya tumbo mara baada ya Ninja mwenzangu kumzidi ujanja mdogo katika urushaji na kumsababishia akwepe tofauti na kuingia kwenye kumi na nane za Ninja mrusha vidubwasha.
Hapo sasa Cj4 kuna kitu alianza kukigundua baada ya yule Ninja aliyechomwa kile kidubwasha mithili ya msumeno wa round kuanza kuzidiwa kutokana na maumivu na kumpa nafasi ya kushambuliwa zaidi na Ninja mwenzake mpaka ikafikia sasaameanguka chini hana ujanja huku mkono mmoja ameshikilia pale tumboni mwake ndipo yule Ninja alipoanza kumsogelea na kumsimamia mbele yake huku akimwambia maneno ambayo Hussein yalimsaidia kuwatofautisha wale Maninja na kumjua m baya ni yupi mwema ni yupi.
Na wakati yule Ninja akimtambia kwa maneno makali mwenzake aliyekuwa katika hali mbaya tena akimtambia zaidi kwa kuamua kuvua maski ile ya Kininja inayoficha uso na kumuwezesha Cj4 kumuona sehemu za Kisogo na kugundua yule ni Ninja dume tena alionekana kichwa chake kikiwa na mchanganyiko wa nywele nyeupe na nyeusi kuonesha kuwa yule ni Ninja mwenye umli mkubwa yaani sio kijana japo alionekana bado strong na mwenye mbinu kwa vile alivyomuona akipambana.
Hapo sasa Cj4 alimshuhudia yule Ninja mzee akichomoa lile panga lake kubwa la Kininja kwa niaba ya kummaliza Ninja yule aliyezidiwa kwa kuchomwa na kidubwasha ambae tayari Cj4 aligundua kuwa ndie Ninja mwema na hapo aliona itakuwa uzembe mkubwa kuacha Ninja yule mwema auawe mbele ya macho yake wakati ana uwezo wa kutoa msaada na aliamini anaweza kumdhibiti yule Ninja mzee baada ya kumsoma toka awali alipokuwa anapambana na Ninja mwenzake na alizigundua mbinu alizomshindia Ninja mwenzake ambae aliamini pia ingekuwa si mbinu zile za ujanja ujanja basi hata yule aliyejeruhiwa angeweza kumdhibi.
Alichungulia Cj4 na kupiga mahesabu ya haraka pindi yule Ninja aliponyanyua panga kwa dhumuni sasa la kummaliza mwenzake bila huruma ambae alikuwa na dariri zote za kukata tamaa na kusubiria kifo na hapo ndipo Cj4 alipoinunua ile kesi kwa style ya kipekee na ajabu.

* * * *

Baada ya Asha kufanya mazingaombwe yake na kuyayuka then kuibukia pale bustanini, alistaajabu kuona maiti mbili za walinzi na alipocheki kwa mbele alimuona Ninja kama yeye akisota mpelampela kuelekea usawa wa chumba kile cha Hussein bubu kwenye ghorofa la ile hoteli.
Alijua sasa tayari kumekucha, na kama ilivyokuwa kwenye mawazo yake kuwa mr X lazima kuna kipofu wake atamtumia kuja kufanya ile kazi baada ya yeye kuikataa na kujua kuwa amejua hadi kufikia kumzimia mitambo ya mawasiliano kati yao alijua sasa na yeye ni miongoni mwa adui wa mr X na yule Ninja katumwa kuja kufanya ile kazi akimaliza lazima atumwe kwake pia hivyo akaona ule ndio wasaa na kwakuwa amewahi lazima kapambane nae.

Aliruka beki kavu mfurulizo Lady Ninja Asha na kumzuia kwa mbele yule Ninja ambae nae alikuwa hajategemea ujio wake lakini alijua kuwa yule kaja kumzuia kufanya kazi muhimu aliyotumwa na hapo ndipo kasheshe likaanza.
"Wee ni Muasi, Lazima Ufe leo hapa hapa ni bora umejileta"
aliongea yule Ninja lakini Lady Ninja hajajibu chochote zaidi alianza kumshambulia kwa mateke ya angani mfurulizo hadi akaanza kumrudisha nyuma japo nae yule Ninja hakuwa wa mchezo.

Pambano lilikuwa kali sana na ikafika sasa Asha alikaribia kummudu yule Ninja lakini mara yule Ninja akabadili mapigo na kuanza kutumia 'Invisible Knifes'.
Ni visu special vidogo sana vya duara vyenye meno makubwa sita ambavyo hurushwa kwa uchawi wa kininja na kama huujui uchawi huo hata kidogo kamwe huwezi kukikwepa hata kimoja lakini uzuri japo Asha yeye hakuwa na vile visu lakini alikumbuka mafunzo aliyopata kwa yule babu wa kijapani kule India na maelekezo ya maneno ya kichawi anayopasa kutamka pindi anaporushiwa 'Invisible Knife' na Ninja yeyote na jinsi ya kuvikwepa.
Na ndivyo alivyofanya Asha kwa wepesi wa ajabu aliweza kuvikwepa kwepa vile visu kwa kubinuka binuka huku nae akijaribu kupeleka mashambulizi lakini kwa bahati mbaya kisu kimoja kilimpata mara baada ya yule Ninja kumzidi ujanja na kumuhadaa kwa kumtishia kisha akamtokea upande wa pili na kuvirusha vitatu kwa mpigo na hapo ndipo Lady Ninja Asha alishindwa kuvikwepa vyote.
"Hhahahahahahaha"
kilisikika kicheko cha yule Ninja na kuendelea na pambano huku Lady Ninja akiwa na maumivu makali sehemu za chini ya tumbo kutokana na kunasiwa na kile kisu lakini alijitahidi kupambana ili kumzuia yule Ninja asiende kumuua babaake.
Alizidi kuelemewa Asha na yule Ninja kibaraka wa mr X hasa kutokana na kutoneshwa palepale na yule Ninja na kuzidi kukisukumia ndani ya nyama zake za tumbo kile kisu kidogo kilichonasia na hatimae Lady Ninja alikosa kabisa nguvu na kuanguka chini.
"Hahahahahaaa 9121 Lady Ninja, sikuwahi kutegemea kama utakuja kuwa msariti kiasi hiki."
Alicheka kwa dharau yule Ninja na kuongea kwa uchungu huku akimsogelea taratibu Asha pale alipoanguka.
"Wewe ni kipofu uliye kwenye Mchezo wa Mr X hujui ukweli wowote, kama unaniua tafadhali Niue mimi tu lakini si babaangu, tafadhali huyo uliyetumwa kumuua ni babaangu tafadhali sana badala yake niue mimi"
aliongea huku akisota sota kurudi nyuma Lady Ninja Asha hakuwa na ujanja wowote, maumivu yalimzidia hakuweza kupambana tena, alikuwa tayari kufa yeye lakini si babaake aliyemjua siku moja tu kabla ya matatizo yote yale.
"Aaaahaaa, vizuri sana kumbe ni babaako hahahahaha yaani hata kama isingekuwa amri ya mr X lakini kwa vile nimejua babaako basi lazima ningemuua tu, na Nitamuua ila kwanza naanza na wewe"
alijibu yule Ninja mara baada ya kusikia kumbe Hussein bubu aliyetumwa akamuue ni baba wa Lady Ninja.
"Lakini mbona unataka kufanya unyama kwa mzazi wangu ambae hana hata muda toka arudi Uraiani? mbona huna huruma wewe...! hebu fanya ingekuwa mzazi wako wewe ungejisikiaje?"
"Ahaaaaa Umeongea vizuri sana Lady Ninja, wewe ni mtoto mdogo kwenye vita vya wanaume lazima utoe mikojo... Umeongea vizuri sana, labda nataka ukumbuke vile ulivyoasi na kumuua babaangu. Ulitegemea na wewe babaako atabaki mzima? Laiti ningejua kama mtoto ninayempa msaada siku zile ndie atayekuja kumuua babaangu basi ningekuua palepale India ulipomwaga mikojo ya hofu"
aliongea safari hii yule Ninja akiwa kasimama jirani kabisa na Asha ambae alisota mpaka kwenye ukuta wa jengo na hakuwa na pa kuendelea zaidi.
Muda wote Asha alipigwa na butwaa mara baada ya yule Ninja kuongea maneno yale, hakufahamu ni babaake gani aliyemuua ila kauli ya kusaidiwa India ndio iliyomstua zaidi na zaidiiii.... ni pale yule Ninja alipoamua kuvua mask yake iliyokuwa inaficha uso na kumfanya Asha azidi kutaharuki japo yeye hakuvua ya kwake.
"AAAH!! UNCLE TYGA..!?"
"Ndio Mimi Mtoto wa Mzee ALY77"
Aliongea Ninja Tyga huku akichomoa kisu kikubwa cha kininja kwaajili ya kummaliza kabisa Asha ambae aliamua kufumba macho baada ya mwili wote kufa ganzi na kukumbuka kuwa ni kweli alimuua mzee Aly77 lakini ilikuwa ni agizo toka kwa Mr X na hakuwahi kujua kama ni babaake na Tyga ambae aliagana nae miaka michache iliyopita kule India.
Lakini ghafraaaaaaaaaaa alishangaa Asha kusikia ukelele wa maumivu kutoka kwa Uncle Tyga uliomfanya afumbue macho na hakuamini alichokuwa anakiona mbele yake juu ya ujio wa kidume ambae alikuwa hajavaa Kininja wala nguo za sare ya aina yoyote iliyomtambulisha yeye ni nani, huku chini alimuona Uncle Tyga akiwa ananyanyuka kwa hasira na usoni damu zikimvuja hali iliyomfanya Asha ashangae zaidi asijue kapigwapigwa vipi sekunde zile chache na yule mtu ambae alisimama mbele yake na alipomuangalia kwa umakini kwa jinsi alivyosimama tu... Aliamini huyu ni zaidi ya Ninja.
Na huyo si mwengine bali ni Cj4.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom