Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: A Fail Not a Fall

Najua hujali kila mara ninapoanza na maandishi yale yale kwenye aya ya kwanza!? Ujue nini, hakuna kitu kigumu kama kusalimia, unaanzaje sasa wakati hujui kama wamekukuta au umewakuta, mimi ukinikuta sianzi kukusalimia na kwa kuwa nimekukuta jioni hii basi ninakusalimia kwa heshima nyingi sana wewe Kapuku mheshimika. Hujambo sana?sijasema ujibu maana kusema hujambo sana sijauliza kama swali eti ujibu.

Kwa sisi tulioanza shule kwa kushika sikio, not sure if my message reachs home here, nasema hivi, enzi zile kuanza la kwanza lazima upitishe mkono wa kulia juu ya kichwa ili ushike sikio la kushoto, kama huelewi, piga picha na kama hata kupiga picha hujui basi nakukaribisha kwenye muziki. Enzi hizo tuna mtihani wa darasa la nne, kwanza nilishindwa kushika sikio mara mbili kisa nina mikono mifupi. Shukuru sana kapuku uko hapa maana ungekuwa na mikono mirefu ungekuwa jela sasa hivi. Hii misemo bhana eti mkono mrefu, mara mkono wa birika. Na kwa sababu mimi ni mkongwe ndo maana sijawashukur wote waliotuamsha kwa Magazeti (shululu , BBC (lee empire , Sala (Shunie ), Historia na Picha (Jimena na Bitoz ), sports (Nyagei )

Nimekumbuka tu mambo ya mitihani ya darasa la nne na namna ilivyokuwa ngumu kufaulu hasa ukizingatia lazima uupige sana umande ndo ufike shule kuwahi namba. Lakini ni jambo zuri tuko hapa na si shule tu hata kwenye maisha yetu ya kazi na yote tunayofanya kumbuka kuwa A Fail means First Attempt In Learning, yaani kama hujashindwa basi hujajaribu, fanya kile unachoona kinafaa kukuletea maendelea ukishindwa haimaanishi ndo mwisho, mlango mmoja ukifungwa basi mwingine uko wazi na kama kuna mlango mmoja tu basi dirisha liko wazi.

Muziki sasa, nani asiyemjua Robert Kelly, R kelly, achana na kashfa zake kama za anko wangu, fuata muziki wake utaupenda, ana tuzo kibao na ni mtunzi mzuri sana na bila kusahau ni mpigaji mzuri wa kinanda. Yeah, ndo maestro wao na ndiye atakayetuburudisha usiku huu.

 
Utusamehe deni zetu kama sisi nasi tuwasamevyo wadeni wetu

Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu, kwa ufalme wako ni wako na nguvu na utukufu hata milele Ameeen.

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nanyi

MATHAYO:6:12:15

Muwe na usiku ulio mwema


Tujifunze kusamehe wapendwa hata kama umekosewa vipi msamehe aliyekukosea ili Mungu atusamehe nasi tuliyomkosea nimejifunza kitu kutokana na neno la leo achia roho we samehe tu
Asante kwa neno mtoto wa Mama mchungaji
 
Utusamehe deni zetu kama sisi nasi tuwasamevyo wadeni wetu

Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu, kwa ufalme wako ni wako na nguvu na utukufu hata milele Ameeen.

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nanyi

MATHAYO:6:12:15

Muwe na usiku ulio mwema


Tujifunze kusamehe wapendwa hata kama umekosewa vipi msamehe aliyekukosea ili Mungu atusamehe nasi tuliyomkosea nimejifunza kitu kutokana na neno la leo achia roho we samehe tu

Amen mtumishi, hili ndo neno kubwa na kama ulikuwa akilini mwangu nami leo nimerusha kustep in the name of love
 
Muziki: A Fail Not a Fall

Najua hujali kila mara ninapoanza na maandishi yale yale kwenye aya ya kwanza!? Ujue nini, hakuna kitu kigumu kama kusalimia, unaanzaje sasa wakati hujui kama wamekukuta au umewakuta, mimi ukinikuta sianzi kukusalimia na kwa kuwa nimekukuta jioni hii basi ninakusalimia kwa heshima nyingi sana wewe Kapuku mheshimika. Hujambo sana?sijasema ujibu maana kusema hujambo sana sijauliza kama swali eti ujibu.

Kwa sisi tulioanza shule kwa kushika sikio, not sure if my message reachs home here, nasema hivi, enzi zile kuanza la kwanza lazima upitishe mkono wa kulia juu ya kichwa ili ushike sikio la kushoto, kama huelewi, piga picha na kama hata kupiga picha hujui basi nakukaribisha kwenye muziki. Enzi hizo tuna mtihani wa darasa la nne, kwanza nilishindwa kushika sikio mara mbili kisa nina mikono mifupi. Shukuru sana kapuku uko hapa maana ungekuwa na mikono mirefu ungekuwa jela sasa hivi. Hii misemo bhana eti mkono mrefu, mara mkono wa birika. Na kwa sababu mimi ni mkongwe ndo maana sijawashukur wote waliotuamsha kwa Magazeti (shululu , BBC (lee empire , Sala (Shunie ), Historia na Picha (Jimena na Bitoz ), sports (Nyagei )

Nimekumbuka tu mambo ya mitihani ya darasa la nne na namna ilivyokuwa ngumu kufaulu hasa ukizingatia lazima uupige sana umande ndo ufike shule kuwahi namba. Lakini ni jambo zuri tuko hapa na si shule tu hata kwenye maisha yetu ya kazi na yote tunayofanya kumbuka kuwa A Fail means First Attempt In Learning, yaani kama hujashindwa basi hujajaribu, fanya kile unachoona kinafaa kukuletea maendelea ukishindwa haimaanishi ndo mwisho, mlango mmoja ukifungwa basi mwingine uko wazi na kama kuna mlango mmoja tu basi dirisha liko wazi.

Muziki sasa, nani asiyemjua Robert Kelly, R kelly, achana na kashfa zake kama za anko wangu, fuata muziki wake utaupenda, ana tuzo kibao na ni mtunzi mzuri sana na bila kusahau ni mpigaji mzuri wa kinanda. Yeah, ndo maestro wao na ndiye atakayetuburudisha usiku huu.


Asante kwa music bora kabisa dj Obe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom