THE DOM
Sehemu Ya 5
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Instagram....
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
SON OF PRESIDENT GU
"kijana wako kaja kujifunza mafunzo ya kijeshi, na kisheria alitakiwa kuanzia JKT, lakini kwa kutumia shotkati zenu, umemleta huku.. Sasa tulia akaribishwe"
"lakini imetosha afande, hebu ona alivyo kama chizi"
Mzee rashidi anajua sahi sio mtu wa mchezo ila inabidi afiche siri,... Sasa mkuu wa majeshi mheshimiwa General Nyange, alipofika alimuuliza sahi,.. Na Wakati huo sahi hata kuona vizuri haoni kutokana na ile oili chafu aliomwagiwa, na hata sura yake haionekani vizuri kwasababu ya hio hio oili
"huo ndio ukamanda kijana.... Karibu kambini kwetu"
Aliongea general huyo, huku akitaka kuruhusu waendelee kumpa mazoezi
"afande naombeni mnisamehe sirudii tena"
Sasa ghafla general akasita kuondoka baada ya maneno hayo kutoka katika kinywa cha sahi,..
"ebu rudia tena hio sauti yako"
General alimuuliza sahi kwa mara nyingine,..
"nisamehe afande"
General alipatwa na kichaa,...
"we mzee, huyu ni mtoto wako"
Nyange alimuuliza mzee Rashidy feki,
"ndio kwani vipi"
"hapana.... Nyie Hebu muosheni huyu kijana nimuone"
Heeeee kumbe general anamjua sahi, lakini sasa kumbe sio General tu, bali kuna vijana wengine wa kijeshi wanaijua sauti hio,....
"muosheni nimuone,... Fanyeni haraka"
ENDELEA...........
Ilikuwa ni siku sahi anapelekwa jeshini na baba yake, ila tunajua kiwa sio baba yake mzazi bali ni mtu aliochaguliwa kwa ajili ya kazi hio, mana akipelekwa na mtu ambaye ni mtumishi wa serikali, watakuwa na maswali mengi juu ya mwanafunzi hiyo, hivyo wamemtumia raia ili wajue ni mtu wa kawaida sana, kumbe ndio jembe la tanzania tena linalotegemewa mno,.... Sahi alijikuta akizunguka zunguka katika kambi za watu akiwa bado ni mgeni, na kama unavyojua sifa za mwanajeshi zilivyo, walimshambulia kwa kumteda hawakujali alivyo vaa, Lakini mkuu wa majeshi mr Nyange, alikuja katika eneo la tukio na kuwataka wamuache mara moja tena wamuoshe ili amuone vizuri, kauli hio ilikuja baada ya kusikia sauti ya kijana huyo kuomba msamaha juu ya kosa la kuchungulia kwenye makalandinga ya kijeshi,....
Pale pale wanajeshi walitii amri ya mkuu wao, walimchukuwa sahi na kumpeleka katika maji, nguo za jeshi zililetwa na hatimaye kuvalishwa, mana kakubaliwa kuingia jeshini, hivyo ana ruksa ya kuvaa nguo hizo pasina shaka, na alipewa kwasababu hakuwa na nguo zingine mana ndio kafika hata maandalizi vizuri hajafanya, hapo kama kaja kitambulishwa tu,...
Sasa mr Nyange alikuwa kakaa katika mti fulani uliopo katika eneo hilo la kijeshi, mti uliotoa kivuli kizuuri sana kilichomvutia mr nyange, wakati huo sahi anatolewa ndani na kuletwa kwa mr Nyange,... Na wakati huo hata mzee rashidi wa muda alikuwepo,....
Sahi alipendezwa sana na mavazi ya kijeshi aliokuwa kayavaa katika mwili wake, na hicho pia ni kitendo kilichozifi kumfanya nyange aamini huyo ni mtoto wake, na wakati huo sahi yupo mbali ndio anakuja kwa mr Nyange,...
Yaani jinsi anavyotembea hizo hatua zake, ni mtoto wake mtupu, na wake nae alikuwa mwanajeshi sasa hatujui kwanini anamhisi sahi,... Sahi alifika kwa mkuu wa majeshi na kutoa saluti ile ya kujifanya hawezi, lakini ndio mwenyewe katika fani hio,.. Mr Nyange aliipokea saluti lakini machozi yalikuwa yakimtoka mfululizo,
"mzee mwenzangu kuna nini tena"
Mzee rashidi alimuuliza mr nyange kuwa kuna nini, mbona machozi kumtoka kwa kumuona kijana huyo
"we acha tu... Kweli nimeamini duniani kuna watu wawili wawili,.. Yqani huyu kijana wako, anafanana na mtoto wangu kila kitu kasoro hio sura tu, lakini mwendo, sauti, hata hio saluti alivyopiga pia ni kama yeye jamani... Basi nimeamini sio mwanangu"
"kwani mwanao ilikuwaje"
"amefariki dunia, ila kijana wako kanikumbusha mbali sana"
"pole sana mzee mwenzangu"
Basi, hali hio iliishia hapo na hata sahi hakuweza kurudi nyumbani tena, mzee rashidi aliondoka zake na kumwacha sahi kambini hapo,.. Chumba chake alipatiwa kilicho cha nguo za kawaida lakini nazo ni za jeshi jeshi... Yaani ukiwa kambini kuvaa nguo za kiraia haitakiwi, hivyo nguo zao za kubadilisha zimekaa staili ya jeshi jeshi,... Sahi aliingia katika hicho chumba lakini kabla ya yote alijifungia ndani na kuanza kukikagua hakina kamera yeyote,... Sasa kumbe hata hio saa aliovaa sahi, ina miale ya kugundua kamera zilipo, na licha ya kazi hio pia saa hio ina rada maalum kwa ajili ya kazi yake, na licha ya kazi hio pia saa hio ina kamera ndani yake, na pia ina Voice recorder,.. Yaani kuna mahali ukibonyeza inakuja sistimu unayotaka, kisha unairudisha katika hali ya kawaida, hivyo hata mtu akiiona hawezi jua kama saa hio ina kazi kama hio, na pia ina kazi ya kupiga simu bila kutumia simu ya mkononi,... Hizo ni saa spesho kwa ajili ya wapelelezi kama hawa, na huku jeshini hakuna aliekuja kumpeleleza bali ni sehemu ya kujiweka ili akigundulika na hao wamiliki wa discate, wajue ni mwanafunzi wa kijeshi au wa TSS, lakini hakuja kulipeleleza jeshi na wala hana wazo hilo....
Sahi alikagua chumba kizima na kugundua hakukuwa na kamera zozote zile, na yeye kama mpelelezi spesho ni wajibu wake kujua hilo, isije kuweka kazi yake matatani
Tukija huku TSS jijini Dar es Salaam, ambako kuna makazi ya usalama wa taifa yaani wale wa siri zaidi,.. Mana kuna wale wa kawaida wanaojulikana na wananchi, lakini sasa kuna hao SECRET SERVICE hao ni zaidi ya hao wanaojulikana na wananchi,... Sasa hio TSS haijulikani mana ni usalama au jeshi la siri,.. Katika kitengo hicho yupo General mkuu wa kitengo hicho lakini kuna kijana mwingine mdogo mdogo hivi aitwaye JOSEPH JOHN POMBE MAGUFULI kwa jina hili tu ni dhahiri kuwa ni mtoto wa rais, ila ana nyota au cheo kikubwa katika kitengo cha TSS na ni kijana mdogo sana, nae ni mmoja wa wapelelezi walio hali ya juu zaidi,..
General alimwita Joseph katika ofisi yake, yaani baada ya General anaefata kwa cheo ni Joseph ambae kwa jina la misheni wanamuita JJ (Joseph John)
"habari yako"
"salama mkuu, hali yako"
Alijibu Joseph huku akipiga saluti kwa mkuu wake,...
"aahhh salama,.. Kuna kijana kaja kujifunza zaidi katika kitengo chetu, ivi ulimkagua"
"mmmhj nadhani sikuwepo wakati akiwasili hapa, ila naweza kumuona hata sasa hivi"
"no, kwa sasa kaenda jeshini, mana anatakiwa kuchukiwa mafunzo ya TMA na TSS, hivyo atasoma wiki moja kule kisha atasoma wiki moja huku"
"ok, kwahio atafika hapa tena baada ya wiki"
"ndio"
"sawa mkuu, nitamkagua pindi atakapokuja"
"ni vizuri, ila unaweza kwenda kumwona kele Arusha"
"hapana mkuu, Kiukweli toka nilipokuwa jeshini na rafiki yangu mtoto wa General Nyange na kupoteza maisha katika mazoezi, Kiukweli sitamani kabisa hata kuiona kambi ya jeshi"
"inaonekana uliumia sana kwa hilo"
"ndio, mana ni mpaka nimeachana na mafunzo ya jeshi baada ya rafiki yangu kipenzi kupoteza maisha... Yaani sitamani kuwa mwanajeshi"
Aliongea Joseph huku akikumbuka tukio la zamani rafiki yake alipokuwa mazoezi na kulipuka na bomu wakati wakiwa mazoezi, kwa kawaida mabomu ya mazoezi hua hayaui lakini haikujulikana ni nani alileta bomu la kweli ndani ya jeshi,...
Kesho yake asubuhi sana kama saa 11 hivi, tukiwa katika kambi ya jeshi kila mmoja alichukuwa begi lenye uzani wa kilo gramu 50 na kuliweka mgongoni, huku wakipiga kwata msituni katika sehemu zao za kufanyia mazoezi,... Wanafunzi walikuwa ni wengi sana huku walimu wao wakiwa kwa nyuma na mbele... Ndani ya wanafunzi kama kawaida wanawake hawakosekani kabisa, na kama unavyojua udhaifu wa wanawake,... Katika hali ya kukimbia hua wanashindwa kubeba lile begi lenye kilo gramu 50 na kukimbia nayo, hivyo wanabaki kuanguka,...
"angalia chalii mgeni anavyoteseka kule"
Aliongea mwanafunzi mmoja akimuongelea sahi au BB, sahi ni zaidi ya hao walimu wenyewe, lakini kaonywa aende kama mwanafunzi hivyo ajifanye hajui kitu, hivyo sahi alikuwa akianguka kila mara ili kuuonyesha uma kiwa kweli alikuwa hajui kitu
"alijua kuna baga huku"
"ahahahahahaha.... Anashindwa hata na baadhi ya wanawake"
Kuna baadhi ya wanawake walikuwa wakijikaza lakini kuna wengine waliokuwa wakishindwa na mazoezi hayo, hivyo huambulia adhabu kali yoka kwa walimu wao,...
Walifanya zoezi mpaka ilifika wakati wa saa mbili za asubuhi, na wakati huo tayari walishabadilisha mazoezi sasa ni kukroo chini huku wakiwa wameshika silaha ambazo hazikuwa na risasi,.. Na wakati huo mabegi yenye uzani yapo migongoni mwao..
"mambo"
Alikuwa ni dada mmoja hivi mrembo sana aliomsalimia sahi,
Sahi hakuitika kwasababu ya kuchoka kwa mazoezi, na sio kuwa kachoka kweli laa bali yupo kikazi zaidi, anatekeleza maagizo alio pewa na wakuu wake,
"haya mafunzo hayahitaji hasira kaka angu, utaumia"
Aliongea yule dada huku wakiendelea kusota chinj, mana wapo wengi sana na kelele zilikuwepo, hivyo wawili wakiongea kwa mwingine kusikia ni ngumu, sahi hakumjibu yule dada chochiukile, waliendelea na mazoezi lakini dada wa watu alikuwa tu kwa ajili ya kufahamiana na kijana huyo, ila sahi kwa kujifanya kuchoka hakuweza kumwitikia,...
Sasa walipokuwa wakiendelea kusota kimazoezi, ghafla sahi aliona baadhi ya wanafunzi kama saba hivi, wakiwa wanachepuka katika njia nyingine tena walimu wao ndio waliokuwa wakiwaamuru kufanya hivyo,.. Wakati huo hakukuwa na mtu alio ona zaidi ya wale wa mbele pale, hivyo watu wa nyuma au hata katikati hawawezi kuona kutokana na majani makubwa kutawala msitu,..
"Samahani dada angu, eti wale wanapelekwa wapi"
Sahi aliona bira avunje ukimya, japo hakuambiwa aipeleleze TMA yeye kaja ili kupata nguzo ya kazi yake, sasa alishangaa kuona baadhi ya wanafunzi wanapitishwa njia za pembeni na mwalimu wao
"nilikusalimia ukanichunia, sasa waniuliza nini"
"Samahani, nimechoka eti si unajua nimekuja jana tu"
"hata salamu pia"
"ok sorry kwa hilo"
Ilibidi aombe radhi kwa kutomwitikia salamu yake,... Lakini sahi kila akipiga jicho, anaona wanazidi kwenda tu
"sikiliza we mkaka, hapa jeshini fuata ulichokifuata, vinginevyo utapelekwa kua mpishi wa wenzako"
"una maana gani dada angu"
Aliuliza sahi huku wakizidi kupitwa na wenzao...
"salehe na mwajuma, naomba msimame"
Sahi na mwaju walionekana na mwalimu wao kuwa hawakuwa wakikroo bali walikuwa wakiongea huku wakiwa wamelala kama wanakroo kumbe laa,....
"umeona sasa, mpaka tumeonewa, we makaka vipi... Haya sasa tutapewa adhabu kubwa hapa"
Aliongea mwaju huku akitia hofu juu ya adhabu watakayo pewa na kamanda wao,
"mumekuja kufanya mazoezi au mumekuja kuongea"
Aliongea kamanda baada ya kuwatoa nje ya mstari,...
"Samahani afande, mimi ni mgeni hivyo nilikuwa nahisi maumivu katika tumbo, baada ya kuburuzika, sasa ndio huyu dada akawa ananiambia nijitahidi, ndipo ukatuona"
Aliongea sahi huku akishika tumbo kama vile anaumwa kweli,
"sasa kwa adhabu yenu, mnatakiwa mrudi mwisho, yaani wale wa kwanzo kutoka mwisho, wawe wa pili kutoka mwisho.. Tena muende kwa kuruka ruka"
Duuuu mwaju alishika kichwa mana hio mwisho yenyewe ilipo ni mbali sana afu uende kwa kuruka ruka kichura,... Hawakuweza kupingana na agizo la kamanda... Walitii japo kwa maumivu makali sana,..
Sasa sahi alpofika eneo la tukio, pale walipokuwa wanachepuliwa wale wanafunzi wengine,... Sahi alitamani sana kupita kwenye hako kamchepuko, mana yeye kama mpelelezi ana haki ya kujua kinachoendelea huku kwenye njia hii tofauti na wengine,...
"unataka ufanye nini"
Aliongea mwaju, huku sahi akijiandaa kuruka,..
Wakati huo mqaju anauliza yeye yupo mbali nae, mana wapo mwisho kabisa,..
"nataka nikajue wameenda kufanya nini wale, usikute wenzetu wanapewa mafunzo mazuri zaidi"
Sahi alisema hivyo, ili kumzuga mwaju asijue kama yeye ni mpelelezi,
"wewe mkaka, umekuja jana tu... Na hicho Kiherehere chako kitakuponza... Mazoezi ni haya haya hakuna mazoezi mengine"
Lakink wakati huo salehe wala hakutaka kumsikiliza mwaju, yaani kama kazi yake inavyomruhusu kufanya.... Sasa ile sahi anajiandaa kuruka ili kutua pembeni alishtukia kukamatwa mguu wake, na kujikuta anarudishwa katika line...
"lazima tukuchunguze kwa undani zaidi... Na utasema wewe ni nani hapa TMA"
Ilikuwa ni sauti ya mtu mwingine kabisa ambae hata hamjui, tena alivalia mavazi ya kiuwalimu, kana kwamba huyo ndio yule mwalimu aliowachepusha wanafunzi saba... Sasa sahi kaja na moto ambao hakutakiwa kuwa nao,.. Yaani kaanza kubainika akiwa na siku ya pili jeshini
Je? Nini Kitaendelea???? USIKOSE
ITAENDELEA.....