Makapuku Forum

Makapuku Forum

HISTORIA YA CHE GUEVARA:

SEHEMU YA 02:

Baada ya kutoweka kwake baadae ilikuja kugundulika Kua alikua Congo akipigana na LAURENT KABILA dhidi ya wabelgiji.
Hata hivyo hakua peke yake alishirikiana na baadhi ya wapiganaji wa Cuba waliokua Africa. Vita ambayo ilishindikana kwn wabelgiji walikua vzr pamoja na kuangushwa na vibaraka wa Congo

Hali hiyo ilifanya Che akimbilie Tanzania na kukaa maeneo ya karibu na ziwa Tanganyika na baadae akahamia Dare es salam huku akiishi kw kujificha.

Baadae mwaka 1966 alirejea Cuba kw siri kumuunga mkono rafiki yake Fidel Castro na pia kumwona mke wake pamoja na watoto wake . Aliwaachia barua ambayo aliwataka waisome siku baada ya kifo chake. (Alihisi huko alikotaka kwenda sio salama).

Baadae tarehe 3/11/1966 alisafili kutoka Montevideo kwenda Bolivia ktk mji wa LA PAZ kuendekeza harakati zake za kuomba inchi za america ya kusini kutoka ktk mikono ya kibepari.

..Aliingia Bolivia km mfanyabiashara mwenye asiri ya URUGUAY na kutumia jina la uongo la ADOLFO MENA GONZALEZ na hii ilipelekea asijulikane kwasababu alinyoa upara, kuweka mvi za bandia na kunyoa ndevu zake zote.

. Aliweka kambi na baadhi ya wapiganaji wenzake aliowakuta Bolivia maeneo ya milima ya montane dry forest. huko aliunada kikundi kilichoitwa NATIONAL LIBERATION ARMY OF BOLIVIA.

Mnamo mwaka 1967, makachero wa Bolivia wakisaidiwa na CIA ambae akiwakilisha ndugu FELIX RODRIGUEZ waligundua maficho ya Che na kundi lake huko milimani BOLIVIA.

Asubuhi ya October 8 mwaka 1967 wanajeshi takribani 1,800 walizingira maeneo yote ya mlima waliokua wamejificha wakina Che GUEAVARA.
vita ikalindima masaa kadhaa na che alipigwa RISASI za miguu na kukamatwa na wenzake.

Ikumbukwe che alikua na jeshi Soho sana kwasababu raia wengi walikataa kujiunga na jeshi na kuogopa kufa. Waliona bora waendelee kunyonywa wakiwa hai kuliko wakafe wakose vyote uhai na haki yao. Basi hali hiyo ilipelekea wale raia MASHIKAWADU kupeleka taarifa serikalini eti wamelazimishwa kujiunga na kikundi cha Che GUAVARA.

Inasemekana baada ya kuzidiwa na mapigano Yale, Che alisema "" usifyatue RISASI mi ni Che GUEAVARA nina thamani kubwa Kua hai kuliko kunikamata nikiwa nimekufa. ...

ITAENDELEA KM ILIVYOPATIKANA MITANDAONI.......

NB: Huyu jamaa tumekua tukivaa T-shirt zake zenye picha inayomuonesha askari alievaa kofia nyekundu na kombati za jeshi.........
35543f0ebfe4ad3f1c7cffe8e23005a9.jpg
 
HISTORIA YA CHE GUEVARA:

SEHEMU YA 02:

Baada ya kutoweka kwake baadae ilikuja kugundulika Kua alikua Congo akipigana na LAURENT KABILA dhidi ya wabelgiji.
Hata hivyo hakua peke yake alishirikiana na baadhi ya wapiganaji wa Cuba waliokua Africa. Vita ambayo ilishindikana kwn wabelgiji walikua vzr pamoja na kuangushwa na vibaraka wa Congo

Hali hiyo ilifanya Che akimbilie Tanzania na kukaa maeneo ya karibu na ziwa Tanganyika na baadae akahamia Dare es salam huku akiishi kw kujificha.

Baadae mwaka 1966 alirejea Cuba kw siri kumuunga mkono rafiki yake Fidel Castro na pia kumwona mke wake pamoja na watoto wake . Aliwaachia barua ambayo aliwataka waisome siku baada ya kifo chake. (Alihisi huko alikotaka kwenda sio salama).

Baadae tarehe 3/11/1966 alisafili kutoka Montevideo kwenda Bolivia ktk mji wa LA PAZ kuendekeza harakati zake za kuomba inchi za america ya kusini kutoka ktk mikono ya kibepari.

..Aliingia Bolivia km mfanyabiashara mwenye asiri ya URUGUAY na kutumia jina la uongo la ADOLFO MENA GONZALEZ na hii ilipelekea asijulikane kwasababu alinyoa upara, kuweka mvi za bandia na kunyoa ndevu zake zote.

. Aliweka kambi na baadhi ya wapiganaji wenzake aliowakuta Bolivia maeneo ya milima ya montane dry forest. huko aliunada kikundi kilichoitwa NATIONAL LIBERATION ARMY OF BOLIVIA.

Mnamo mwaka 1967, makachero wa Bolivia wakisaidiwa na CIA ambae akiwakilisha ndugu FELIX RODRIGUEZ waligundua maficho ya Che na kundi lake huko milimani BOLIVIA.

Asubuhi ya October 8 mwaka 1967 wanajeshi takribani 1,800 walizingira maeneo yote ya mlima waliokua wamejificha wakina Che GUEAVARA.
vita ikalindima masaa kadhaa na che alipigwa RISASI za miguu na kukamatwa na wenzake.

Ikumbukwe che alikua na jeshi Soho sana kwasababu raia wengi walikataa kujiunga na jeshi na kuogopa kufa. Waliona bora waendelee kunyonywa wakiwa hai kuliko wakafe wakose vyote uhai na haki yao. Basi hali hiyo ilipelekea wale raia MASHIKAWADU kupeleka taarifa serikalini eti wamelazimishwa kujiunga na kikundi cha Che GUAVARA.

Inasemekana baada ya kuzidiwa na mapigano Yale, Che alisema "" usifyatue RISASI mi ni Che GUEAVARA nina thamani kubwa Kua hai kuliko kunikamata nikiwa nimekufa. ...

ITAENDELEA KM ILIVYOPATIKANA MITANDAONI.......

NB: Huyu jamaa tumekua tukivaa T-shirt zake zenye picha inayomuonesha askari alievaa kofia nyekundu na kombati za jeshi.........
35543f0ebfe4ad3f1c7cffe8e23005a9.jpg
Asante mpendwa wa binamu
 
HISTORIA YA CHE GUEAVARA:

SEHEMU YA TATU:

che Guevara alifungwa kamba na wenzake akakamatwa na kupelekwa kijiji cha LA HIGUERA ambapo baada ya raisi wa BOLIVIA ndugu Rene Barrientos kusikia amekamatwa alitoa amri auawe haraka sana. Wakati huo huo CIA walimtaka apelekwe panama akahojiwe kw kina na salama yake ili asiuawe ilikua apepelekwe MAREKANI japo haikutokea.

Siku moja kabla ya kuuawa alichukuliwq na baadhi ya wanajeshi na kupiga picha ya kumbukumbu na kesho yake ambayo ilikua tarehe 9/10/1967. Aliuawa na askari mmoja aliejitolea kumpiga RISASI sita za kifua na kufa palepale . na huo ndo ukawa mwisho wake akaiaga Dunia akiwa na miaka 39.

Kabla hajapigwa RISASI na askari huyo aliongea maneno yafuatayo.....

Najua umekuja kuniua, nipige RISASI mtu mwoga ww!!!. na ufahamu utakua umeua mwanaume kamili".

Baada ya kifo chake , Guevara alichukuliwa km nguzo ya vuguvugu la kimapinduzi ya jisoshalisti Duniani. picha yake na kofia aina ya BARET aliyopenda kuivaa vimekua km alama za mapinduzi DUNIANI.

....CHE GUEAVARA ktk maisha yake yote alifanikiwa Kua na wake wawili na watoto watano. Ambavyo mke wa kwanza aliitwa HILDA GADEA na alizaanae mtoto mmoja wa kike alieitwa HILFA GUEAVARA aliezaliwa Mnamo mwaka 1956 na kufariki.

Walikua ktk mahusiano kuanzia (1956-1959) waliachana baada ya HILDA kugundua bwana che anatoka na mwanamke mwingine . Hilda aliomba taraka mwenyewe kw wivu wa mapenzi na alikuja kufariki 1974. Miaka 52. hapo mke wa pili wa che Guevara alikuja Kua mchepuko wake huyo.

Mke wake wa pili yaani yule aliekua mchepuko hapo mwanzo aliitwa ALEIDA MARCH kuanzia 1959 mpaka che GUEAVARA anauawa. Wakiwa wamezaa watoto wanne waitwao ALEIDA(1960)CAMILA(1962), CELIA(1963)na ERNESTO(1965).

kuna baadhi ya source zinasema anawatoto zaidi ya watano ambao wengine wanadai wapo Congo na Tanzania .

Ambacho hicho kitu hakina uhakika labda angekuwepo yeye angetuambia ukweli. Ndomana inajulikana alikua anawatoto watano tuu, hao wanaojitokeza kwamba wanawatoto wake watakuja hata siku mie nikifa ila kw sasa Nina LOVENESS pekee.

Kwa ushauri muulize mama yako inawezekana ukawa ww unaesoma hapa ndie mtoto wake . ukibahatika Kua ww muulize mama yako alimpende a nn huyu shujaa Che GUEAVARA kipenzi cha watu Duniani na mpaka kesho usipovaa tishet yenye picha yake utaiona hata Dukani au hapa chini ukimaliza kusoma stori hii.

MWISHO ........kizuri hakidumu Mara zote hupingwa na wenye maslahi yao ..

.
a1146f4e889c99df6a51bd6914496c1e.jpg
 
HISTORIA YA CHE GUEVARA:

SEHEMU YA 02:

Baada ya kutoweka kwake baadae ilikuja kugundulika Kua alikua Congo akipigana na LAURENT KABILA dhidi ya wabelgiji.
Hata hivyo hakua peke yake alishirikiana na baadhi ya wapiganaji wa Cuba waliokua Africa. Vita ambayo ilishindikana kwn wabelgiji walikua vzr pamoja na kuangushwa na vibaraka wa Congo

Hali hiyo ilifanya Che akimbilie Tanzania na kukaa maeneo ya karibu na ziwa Tanganyika na baadae akahamia Dare es salam huku akiishi kw kujificha.

Baadae mwaka 1966 alirejea Cuba kw siri kumuunga mkono rafiki yake Fidel Castro na pia kumwona mke wake pamoja na watoto wake . Aliwaachia barua ambayo aliwataka waisome siku baada ya kifo chake. (Alihisi huko alikotaka kwenda sio salama).

Baadae tarehe 3/11/1966 alisafili kutoka Montevideo kwenda Bolivia ktk mji wa LA PAZ kuendekeza harakati zake za kuomba inchi za america ya kusini kutoka ktk mikono ya kibepari.

..Aliingia Bolivia km mfanyabiashara mwenye asiri ya URUGUAY na kutumia jina la uongo la ADOLFO MENA GONZALEZ na hii ilipelekea asijulikane kwasababu alinyoa upara, kuweka mvi za bandia na kunyoa ndevu zake zote.

. Aliweka kambi na baadhi ya wapiganaji wenzake aliowakuta Bolivia maeneo ya milima ya montane dry forest. huko aliunada kikundi kilichoitwa NATIONAL LIBERATION ARMY OF BOLIVIA.

Mnamo mwaka 1967, makachero wa Bolivia wakisaidiwa na CIA ambae akiwakilisha ndugu FELIX RODRIGUEZ waligundua maficho ya Che na kundi lake huko milimani BOLIVIA.

Asubuhi ya October 8 mwaka 1967 wanajeshi takribani 1,800 walizingira maeneo yote ya mlima waliokua wamejificha wakina Che GUEAVARA.
vita ikalindima masaa kadhaa na che alipigwa RISASI za miguu na kukamatwa na wenzake.

Ikumbukwe che alikua na jeshi Soho sana kwasababu raia wengi walikataa kujiunga na jeshi na kuogopa kufa. Waliona bora waendelee kunyonywa wakiwa hai kuliko wakafe wakose vyote uhai na haki yao. Basi hali hiyo ilipelekea wale raia MASHIKAWADU kupeleka taarifa serikalini eti wamelazimishwa kujiunga na kikundi cha Che GUAVARA.

Inasemekana baada ya kuzidiwa na mapigano Yale, Che alisema "" usifyatue RISASI mi ni Che GUEAVARA nina thamani kubwa Kua hai kuliko kunikamata nikiwa nimekufa. ...

ITAENDELEA KM ILIVYOPATIKANA MITANDAONI.......

NB: Huyu jamaa tumekua tukivaa T-shirt zake zenye picha inayomuonesha askari alievaa kofia nyekundu na kombati za jeshi.........
35543f0ebfe4ad3f1c7cffe8e23005a9.jpg
Mwanaharakati wa kweli
 
HII NDIYO HISTORIA HALISI YA MANENO "SHIKAMOO" NA "MARAHABA."
kuna idadi kubwa ya watu wanatumia neno shikamoo kama sehemu ya kuonyesha heshima au salamu kwa mtu aliyekuzidi umri.
Ila ni muhimu sana tukaelewa maana na historia ya na maneno “Shikamioo” na “Marahaba”. Kama ifahamikavyo kuwa kila jambo huwa na mwanzo na mwanzo huwa na sababu za kufanya hilo jambo kuibuka. Ni hivi kabla ya miaka ya 600 BK au BM, Wabantu walikuwa wameshafika Pwani ya Afrika mashariki. Na ukweli ni kwamba Wabantu walishapata kuishi hapo na hata wageni waliofika walikiri suala hilo. Na kwa kuwa Wabantu walipata kuishi hapo walikuwa na mitindo yao wa maisha na walikuwa wakiheshimiana.
Kikubwa zaidi Wabantu walikuwa na salamu zao. Kwa mfano Wazaramo (historia yao itaandikwa) walikuwa na salamu yao kama ifuatavyo, aliyekuwa akiamkia alionyoosha mikono mbele na kusema “simbamwenee” na kisha anayeamkia huitikia “utwaaa”. Na kila mtu alikuwa akifurahia salamu hiyo, iliyokuwa nzuri kuitamka mdomoni.
Lakini mambo yalibadilika pale walipokuja Waarabu na kuanzisha biashara ya utumwa. Na hapo tukapata makundi mawili yaani “mtumwa” na “bwana” na mtumwa alipaswa kumuamkia Bwana kwa neno la “Nashika Miuu” akiwa na maana ya “Nashika Miguu”. Na kila mtumwa alipaswa kujua na kutambua salamu hii.
Na mtumwa alipaswa kutoa salamu hii hata mara 100 kwa siku moja. Lengo la salamu hii ilikuwa ni kutenganisha kati ya mtumwa na bwana wake.
Kuanzia miaka ya 600-1700, salamu hii ilikuwa ikitumika maeneo ya Pwani tu. Na kuanzia miaka ya 1700 mwishoni na 1800 mwanzoni Waarabu walianza kuingia maeneo ya ndani ya Afrika mashariki. Na kila walipofika salamu hii waliitumia na baadhi ya machifu waliipenda sana salamu hii. Na kujikuta wakiwa na matamshi tofauti juu ya salamu hiyo. Na kwa wakati wote huo ilikuwa ni salamu ilikuwa ni "Nashika Miuu" na sio "Shikamoo" kama ilivyo sasa.
Kutokana na watu tofauti kutumia salamu hii, wapo waliotamka "Shikamuu" kama neno moja. Na mpaka miaka ya 1930, kipindi ambacho Kiswahili kinafanyiwa usanifishaji ndipo tukapata neno "shikamoo."
Na kuhusu neno "Marahaba", lina maana ya "asante". Na neno hili huitikiwa na Yule anaeamkiwa (Bwana) ambaye miguu yake imeshikwa na mtumwa. Na mpaka sasa salamu hii inatumiwa sana na Watanzania wengi licha ya kuwa na salamu zao za kikabila.
Hii ndio historia fupi ya neno "Shikamoo" na "Marahaba".
- Shukrani za pakee ziwafikie "Historia ya Afrika" .
- Kambi Kuu kwa ihsani ya Habari Forums.
 
THE DOM

Sehemu Ya 4

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Instagram....

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

SON OF PRESIDENT GU

Salehe aliondoka Ikulu na gari yake yenye usajili wa nymber za serikali, na gari hilo anaruhusiwa kuwa nalo ili usumbufu wa barabarani usitokee pale anapotakiwa kuwahi mahari fulani,..
Sahi alifika nyumbani kwake majira ya saa tano za asubuhi, aliweka kila kitu chake,... Kisha akalikagua vizuri lile begi aina ya dranka maalum la kuwekea vifaa vya upelelezi,... Sahi alicheka sana huku akitoa kifaa kimoja kilichokaa mfano wa Hard drive,... Huku akisema
"huu ndio utajiri unaotafutwa na serikali yangu,... The Discate Of Money,... Nazitaka hizo codes zake... AHahahahahahahah.."

Sasa cha ajabu na cha kushangaza, kumbe discate of money anayo sahi, au BB,.. Tena anataka na hizo codes zake,... Wakati huo anacheka kwa mbwembwe nyingi sana huku akiiangalia hio Discate ya noti ya shilingi lakini moja,.....
"How can get the codes?"
Salehe au BB alijiuliza atazipataje cedes hizo?.... Wakati huo sahi anacheka kwa dharau huku akiiangalia ramani ya Jengo la BOT lilivyo..

ENDELEA.............

Ama kweli ukijua kula na kipofu, basi utafaidi vingi sana, mana sahi ndie alie kabidhiwa jukumu la kuitafuta discate hio, alafu kumbe yeye mwenyewe ndio anayo katika mikono yake, tena wakati huo akiwa anapiga mahesabu ya kuingia, BANK OF TANZANIA (BOT) Ili kukamilisha codes za hio discate,.. Sahi au BB kwa jina la kazi aliweza kurudisha discate hio katika kisanduku maalumu cha discate hio kisha akakiweka katika dranka la vifaa vyake,...

Kesho yake asubuhi salehe akiwa na mtu mmoja hivi ambae kwenye uongizi hayupo, yaani ni mwananchi wa kawaida tu, huyo ndie aliekabiziwa jukumu la kumpeleka salehe katika kazi, na kitengo cha kwanza alipelekwa TSS kitendo ambacho kipo mjini kati lakini hakijulikani, hicho ni kitengo cha usalama wa taifa cha siri sana tena kinahusika na mambo mengi hususan upelelezi, na ndio mana salehe kaletwa huku mana kuna wapelelezi wenzake,... Na sio wapelelezi tu bali ni wapiganaji wazuri ila wao wamesomea Tanzania,

Mzee huyo yupo spesho kama baba wa salehe, na salehe yeye hajui popote anapo pelekwa hata huko TSS hapajui hata kidogo... Gari iliingia katika ghorofa moja safi sana, juu ni makazi ya wao wao wenyewe, lakini kwa chini sasa ndio kuna kila kiti, kwanza gari ikiingia geti linafungwa, afu papo hapo baada ya kulipita geti, mbele kuna kibanda, kama cha sevisi za gereji hivi lakini sivyo,.. Gari ikifika pale, hua panabonyea chini, kwahio makazi ya TSS yapo chini ya ghorofa katika underground, yaani chini ya ardhi ndipo makazi ya TSS yalipo,... Na mlango mkuu ni hio sehemu iliokaaa kama sevisi za magari kumbe ndio mlango mkuu wa kuingilia huko ndani,

Walipofika chini huko, yaani ni sehemu kubwa sana utafikiri ni nje, kumbe ni ndani,.. Hua mtu akishafika huko haulizwi sana kwasababu kama huhusiki huko, basi hata kwenye mlango mkuu pale hufiki, lakini kama umepita mlango mkuu basi unahusika,.... Sasa mzee ndio kipau mbele na hana wasiwasi, kwanza ni mtu mwenye pesa afu kaagizwa na kiongozi wa nchi, hivyo hakuwa na hofu kuingia ndani zaidi,.. Ukipita hapo kwenye maofisini kumejaa makompyuta ya kazi, na wakati huo watu wapo bize kana kwamba kila mtu kuna anchokitafuta au kuna kazi anaifanya, unaweza ukashirikiana na mwenzako lakini kila mmoja ana kazi iliomleta kama vile Salehe, kaletwa na kazi ya kutafuta discate na hapa sio kuwa discate ndio ipo ila awe na kazi ya kujizuia ili hata watu wanaomshtukia kuwa huyo ni nani, wakitafuta information zake wakute ni mwanafunzi wa TSS afu pia ni mwanafunzi wa TMA (TANZANIA MILITARY ACADEMY) Mana atakuwa anafanya kazi katika vitengo viwili kwa nyakati tofauti tofauti,... Lakini kazi hizo hazina maana kwake ispokua yupo kwa ajili ya kuitafuta discate,...
Mzee huyo alietambulika kwa jina la mzee Rashidy, na hata hilo jina sio lake ni ili tu kujifanya amemleta mtoto wake asomee upelelezi kwahio kitengo hiki kipo kwa ajili ya kukufunza practically jinsi ya kupeleleza,... Na pia hapo hapo kinafanya kazi, yaani unafunzwa huku unafanya kazi mpaka unakuwa afisa mkubwa hapo hapo na haruhusiwi kuacha kazi kirahisi mana ni kitengo kinachoijua nchi kwa undani zaidi... Mzee alionana na ofisa mkuu wa TSS yaani yule General mwenyewe ambae anaagiza tu,... Mzee aliongea mengi sana na General wa TSS, wakati huo mzee anaongea kule ofisini, huku Salehe yeye anazungukia ofisi za watu, na hapo wafanyakazi bado hawajamjua kama atakuwa mwenzao nini, kila akipita kwenye kompyuta anakuta wafanyakazi wanafuatilia information fulani kwa kutumia satalaiti,.. Yaani walikuwa bize sana hata kumuona mgeni hawamuoni,... Salahe aliipenda sana ile bize iliokuepo pale, na hapo hajui mtu hata mmoja,...

Huku ofisini mzee amemaliza kuongea na General wa TSS, sasa General anauliza huyo kijana yuko wapi, wakati huo sahi ndio kwanza yupo katikati ya maofisi ya watu,..
Mzee alimpigia sahi simu
"uko wapi wewe"
"nakuja mzee"
Sahi alitoka mbio mpaka ofisini, kwanza kaingia bila hata ya kupiga saluti, sio kwamba hajui ila kaambiwa aende kama mwanafunzi, hivyo ajifanye hajui ili ajue njia nyingi za kufanya kazi...
"ataweza kazi kweli huyu? Mbona kama kalegea legea hivi"
Aliongea general wa TSS, huku Salehe akijifanya kukakamaa kama mwanajeshi, lakini General akajua huyu kijana ni bure, hajui lolote...
Mzee rashidi alimaliza kila kitu na Salahe akawa kapata kazi au shule ya kujifunzi, mana unajifunza kuitumia kompyuta kwa ajili ya upelelezi zaidi, kisha unapelekwa practically kufanya upelelezi wa vitendo,...

Baada ya kumaliza hapo ikiwa ni mida ya saa sita za mchana,.. Sahi na mzee huyo aliekuwa kama baba yake wakiwa wanakwenda Airport kwa ajili ya kwenda Arusha kwenye chuo cha kijeshi, yaani anapelekwa zile sehemu nyeti za usalama wa taifa,... Walichukuwa ndege ya private kisha haooo, wakaondoka kuelekea TMA na huko ndipo atakapoanza kazi yake,.. Ilipofika saa nane ndege inatua arusha, kijijini munduli, ambako ndiko makao makuu ya jeshi,.. Hivyo katika mikoa yote mkiona kambi ya jeshi hayo ni matawi tu lakini makao makuu yapo arusha,.. Walipofika katika kambi hio au chuo hicho cha kijeshi, walishuka kama watu wakubwa fulani hibi, mana walikuja na private jet,

"salama afande"
mzee rashidi alisalimia kwa wakuu wa jeshi aliowakuta katika kambi hio, shamra shamra za mazoezi zilikuwa zikirindima, yaani kila kikosi na mazoezi yao, sahi sio mgeni na hivyo vitu tena kwa yeye anaona ni vitu vyepesi sana, mana ujeshi wake yeye kausomea korea, hivyo ana uwezo mkubwa kuliko mtu yeyote hapo kambini, na yupo kwa kazi maalumu..

"afande, kuna mgeni anahitaji kukuona"
"aingie"
Mkuu wa majeshi Tanzania nzima ndio anamruhu baba yake SALEHE aingie ndani,... Mheshimiwa Nyange akiwa katika kiti chake cha heshima ya ukuu wa jeshi Tanzania nzima,... Sasa sahi kama kawaida yake ya kubaki nyuma, yaani mzee anaingia ofisini yeye kabaki nyuma,.. Saa ngapi asianze kuizunguka hio kambi ya jeshi, palikuwa na vijana wengi sana ni zaidi ya wanafunzi elfu moja ukijumlisha na walimu, wenye vyeo vyao.... Sasa wanajeshi bado hawajamjua sahi kuwa ni nani afu kavalia nguo zkisharobaro hivi, saa ngapi mwanajeshi mmoja hajamtamani sahi,... Yaani ilimradi kumkomoa mana alikuwa akiangalia amgalia mabogi ya magari ambayo ni magari ya kijeshi, sasa sahi alijifanya kuchungulia... Kwanza alishtukia kavutwa kisha kawashwa kofi,
"umemueka baba yako uko chini ya gari"
Aliongea mmoja wa makamanda huku makamanda wengine wakizidi kujaa eneo la tukio,.. Sahi kaambiwa awe mpole, ajifanye hajui, sasa kama unavyojua maonevu ya wanajeshi yalivyo... Kabla sahi hajajibu kasukumwa na mtu mwingine,... Papo hapo akaanza kupewa zoezi la kushusha giabox la gari peke yake, kitu ambacho hakiwezekani kushusha giabox la kalandinga la jeshi peke yako, eti kisa alikuwa anachungulia....
"broo siwezi eti"
Wakati huo sahi akiongea hayo tayari keshalioga vumbi jinga sana, nguo zake za usharobaro tayari zimekuwa kama nguo za kichaaa.... Sasa walipoona anazidi kukataa, likaletwa galeni la oili chafu, yaani hawana utani na hata sahi anajua yaani hata ni kuchomwa mwanajeshi akiamua anakuchoma kweli,... Lile dumu lenye oili lote lilimwagikia yeye, uso mzima kwa mweusi,.... Sasa huku mzee keshamaliza kuongea wanageuka nyuma hawamuoni kijana husika,... Nyange alijua tu tayari kimeshanuka huko nje, mana anawajua makamanda wake walivyo, yaani wakiona raia hapa kambini kama haeleweki wanampa adhabu,... Kweli walipotoka wanaona kuna mahari kuna watu wengi sana, yaani wanajeshi wamekusanyika sehemu moja wakimchezea mtu mmoja yaani wana hamu ya kutesa ile mbaya,...
"waamuru basi vijana wako wamuache"
Aliongea mzee huyo ili sahi aachwe, lakini Nyange hakutaka kufanya hivyo
"kijana wako kaja kujifunza mafunzo ya kijeshi, na kisheria alitakiwa kuanzia JKT, lakini kwa kutumia shotkati zenu, umemleta huku.. Sasa tulia akaribishwe"
"lakini imetosha afande, hebu ona alivyo kama chizi"
Mzee rashidi anajua sahi sio mtu wa mchezo ila inabidi afiche siri,... Sasa mkuu wa majeshi mheshimiwa General Nyange, alipofika alimuuliza sahi,.. Na Wakati huo sahi hata kuona vizuri haoni kutokana na ile oili chafu aliomwagiwa, na hata sura yake haionekani vizuri kwasababu ya hio hio oili
"huo ndio ukamanda kijana.... Karibu kambini kwetu"
Aliongea general huyo, huku akitaka kuruhusu waendelee kumpa mazoezi
"afande naombeni mnisamehe sirudii tena"
Sasa ghafla general akasita kuondoka baada ya maneno hayo kutoka katika kinywa cha sahi,..
"ebu rudia tena hio sauti yako"
General alimuuliza sahi kwa mara nyingine,..
"nisamehe afande"
General alipatwa na kichaa,...
"we mzee, huyu ni mtoto wako"
Nyange alimuuliza mzee Rashidy feki,
"ndio kwani vipi"
"hapana.... Nyie Hebu muosheni huyu kijana nimuone"
Heeeee kumbe general anamjua sahi, lakini sasa kumbe sio General tu, bali kuna vijana wengine wa kijeshi wanaijua sauti hio,....
"muosheni nimuone,... Fanyeni haraka"

Je? Sahi ni nani??? Mbona kila kona anajulikana??? Na je kwanini general anamjua sahi,.. Huyu sahi ni NANI??

ITAENDELEA.....
 
THE DOM

Sehemu Ya 5

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Instagram....

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

SON OF PRESIDENT GU

"kijana wako kaja kujifunza mafunzo ya kijeshi, na kisheria alitakiwa kuanzia JKT, lakini kwa kutumia shotkati zenu, umemleta huku.. Sasa tulia akaribishwe"
"lakini imetosha afande, hebu ona alivyo kama chizi"
Mzee rashidi anajua sahi sio mtu wa mchezo ila inabidi afiche siri,... Sasa mkuu wa majeshi mheshimiwa General Nyange, alipofika alimuuliza sahi,.. Na Wakati huo sahi hata kuona vizuri haoni kutokana na ile oili chafu aliomwagiwa, na hata sura yake haionekani vizuri kwasababu ya hio hio oili
"huo ndio ukamanda kijana.... Karibu kambini kwetu"
Aliongea general huyo, huku akitaka kuruhusu waendelee kumpa mazoezi
"afande naombeni mnisamehe sirudii tena"
Sasa ghafla general akasita kuondoka baada ya maneno hayo kutoka katika kinywa cha sahi,..
"ebu rudia tena hio sauti yako"
General alimuuliza sahi kwa mara nyingine,..
"nisamehe afande"
General alipatwa na kichaa,...
"we mzee, huyu ni mtoto wako"
Nyange alimuuliza mzee Rashidy feki,
"ndio kwani vipi"
"hapana.... Nyie Hebu muosheni huyu kijana nimuone"
Heeeee kumbe general anamjua sahi, lakini sasa kumbe sio General tu, bali kuna vijana wengine wa kijeshi wanaijua sauti hio,....
"muosheni nimuone,... Fanyeni haraka"

ENDELEA...........

Ilikuwa ni siku sahi anapelekwa jeshini na baba yake, ila tunajua kiwa sio baba yake mzazi bali ni mtu aliochaguliwa kwa ajili ya kazi hio, mana akipelekwa na mtu ambaye ni mtumishi wa serikali, watakuwa na maswali mengi juu ya mwanafunzi hiyo, hivyo wamemtumia raia ili wajue ni mtu wa kawaida sana, kumbe ndio jembe la tanzania tena linalotegemewa mno,.... Sahi alijikuta akizunguka zunguka katika kambi za watu akiwa bado ni mgeni, na kama unavyojua sifa za mwanajeshi zilivyo, walimshambulia kwa kumteda hawakujali alivyo vaa, Lakini mkuu wa majeshi mr Nyange, alikuja katika eneo la tukio na kuwataka wamuache mara moja tena wamuoshe ili amuone vizuri, kauli hio ilikuja baada ya kusikia sauti ya kijana huyo kuomba msamaha juu ya kosa la kuchungulia kwenye makalandinga ya kijeshi,....

Pale pale wanajeshi walitii amri ya mkuu wao, walimchukuwa sahi na kumpeleka katika maji, nguo za jeshi zililetwa na hatimaye kuvalishwa, mana kakubaliwa kuingia jeshini, hivyo ana ruksa ya kuvaa nguo hizo pasina shaka, na alipewa kwasababu hakuwa na nguo zingine mana ndio kafika hata maandalizi vizuri hajafanya, hapo kama kaja kitambulishwa tu,...

Sasa mr Nyange alikuwa kakaa katika mti fulani uliopo katika eneo hilo la kijeshi, mti uliotoa kivuli kizuuri sana kilichomvutia mr nyange, wakati huo sahi anatolewa ndani na kuletwa kwa mr Nyange,... Na wakati huo hata mzee rashidi wa muda alikuwepo,....
Sahi alipendezwa sana na mavazi ya kijeshi aliokuwa kayavaa katika mwili wake, na hicho pia ni kitendo kilichozifi kumfanya nyange aamini huyo ni mtoto wake, na wakati huo sahi yupo mbali ndio anakuja kwa mr Nyange,...
Yaani jinsi anavyotembea hizo hatua zake, ni mtoto wake mtupu, na wake nae alikuwa mwanajeshi sasa hatujui kwanini anamhisi sahi,... Sahi alifika kwa mkuu wa majeshi na kutoa saluti ile ya kujifanya hawezi, lakini ndio mwenyewe katika fani hio,.. Mr Nyange aliipokea saluti lakini machozi yalikuwa yakimtoka mfululizo,
"mzee mwenzangu kuna nini tena"
Mzee rashidi alimuuliza mr nyange kuwa kuna nini, mbona machozi kumtoka kwa kumuona kijana huyo
"we acha tu... Kweli nimeamini duniani kuna watu wawili wawili,.. Yqani huyu kijana wako, anafanana na mtoto wangu kila kitu kasoro hio sura tu, lakini mwendo, sauti, hata hio saluti alivyopiga pia ni kama yeye jamani... Basi nimeamini sio mwanangu"
"kwani mwanao ilikuwaje"
"amefariki dunia, ila kijana wako kanikumbusha mbali sana"
"pole sana mzee mwenzangu"

Basi, hali hio iliishia hapo na hata sahi hakuweza kurudi nyumbani tena, mzee rashidi aliondoka zake na kumwacha sahi kambini hapo,.. Chumba chake alipatiwa kilicho cha nguo za kawaida lakini nazo ni za jeshi jeshi... Yaani ukiwa kambini kuvaa nguo za kiraia haitakiwi, hivyo nguo zao za kubadilisha zimekaa staili ya jeshi jeshi,... Sahi aliingia katika hicho chumba lakini kabla ya yote alijifungia ndani na kuanza kukikagua hakina kamera yeyote,... Sasa kumbe hata hio saa aliovaa sahi, ina miale ya kugundua kamera zilipo, na licha ya kazi hio pia saa hio ina rada maalum kwa ajili ya kazi yake, na licha ya kazi hio pia saa hio ina kamera ndani yake, na pia ina Voice recorder,.. Yaani kuna mahali ukibonyeza inakuja sistimu unayotaka, kisha unairudisha katika hali ya kawaida, hivyo hata mtu akiiona hawezi jua kama saa hio ina kazi kama hio, na pia ina kazi ya kupiga simu bila kutumia simu ya mkononi,... Hizo ni saa spesho kwa ajili ya wapelelezi kama hawa, na huku jeshini hakuna aliekuja kumpeleleza bali ni sehemu ya kujiweka ili akigundulika na hao wamiliki wa discate, wajue ni mwanafunzi wa kijeshi au wa TSS, lakini hakuja kulipeleleza jeshi na wala hana wazo hilo....
Sahi alikagua chumba kizima na kugundua hakukuwa na kamera zozote zile, na yeye kama mpelelezi spesho ni wajibu wake kujua hilo, isije kuweka kazi yake matatani

Tukija huku TSS jijini Dar es Salaam, ambako kuna makazi ya usalama wa taifa yaani wale wa siri zaidi,.. Mana kuna wale wa kawaida wanaojulikana na wananchi, lakini sasa kuna hao SECRET SERVICE hao ni zaidi ya hao wanaojulikana na wananchi,... Sasa hio TSS haijulikani mana ni usalama au jeshi la siri,.. Katika kitengo hicho yupo General mkuu wa kitengo hicho lakini kuna kijana mwingine mdogo mdogo hivi aitwaye JOSEPH JOHN POMBE MAGUFULI kwa jina hili tu ni dhahiri kuwa ni mtoto wa rais, ila ana nyota au cheo kikubwa katika kitengo cha TSS na ni kijana mdogo sana, nae ni mmoja wa wapelelezi walio hali ya juu zaidi,..
General alimwita Joseph katika ofisi yake, yaani baada ya General anaefata kwa cheo ni Joseph ambae kwa jina la misheni wanamuita JJ (Joseph John)
"habari yako"
"salama mkuu, hali yako"
Alijibu Joseph huku akipiga saluti kwa mkuu wake,...
"aahhh salama,.. Kuna kijana kaja kujifunza zaidi katika kitengo chetu, ivi ulimkagua"
"mmmhj nadhani sikuwepo wakati akiwasili hapa, ila naweza kumuona hata sasa hivi"
"no, kwa sasa kaenda jeshini, mana anatakiwa kuchukiwa mafunzo ya TMA na TSS, hivyo atasoma wiki moja kule kisha atasoma wiki moja huku"
"ok, kwahio atafika hapa tena baada ya wiki"
"ndio"
"sawa mkuu, nitamkagua pindi atakapokuja"
"ni vizuri, ila unaweza kwenda kumwona kele Arusha"
"hapana mkuu, Kiukweli toka nilipokuwa jeshini na rafiki yangu mtoto wa General Nyange na kupoteza maisha katika mazoezi, Kiukweli sitamani kabisa hata kuiona kambi ya jeshi"
"inaonekana uliumia sana kwa hilo"
"ndio, mana ni mpaka nimeachana na mafunzo ya jeshi baada ya rafiki yangu kipenzi kupoteza maisha... Yaani sitamani kuwa mwanajeshi"
Aliongea Joseph huku akikumbuka tukio la zamani rafiki yake alipokuwa mazoezi na kulipuka na bomu wakati wakiwa mazoezi, kwa kawaida mabomu ya mazoezi hua hayaui lakini haikujulikana ni nani alileta bomu la kweli ndani ya jeshi,...

Kesho yake asubuhi sana kama saa 11 hivi, tukiwa katika kambi ya jeshi kila mmoja alichukuwa begi lenye uzani wa kilo gramu 50 na kuliweka mgongoni, huku wakipiga kwata msituni katika sehemu zao za kufanyia mazoezi,... Wanafunzi walikuwa ni wengi sana huku walimu wao wakiwa kwa nyuma na mbele... Ndani ya wanafunzi kama kawaida wanawake hawakosekani kabisa, na kama unavyojua udhaifu wa wanawake,... Katika hali ya kukimbia hua wanashindwa kubeba lile begi lenye kilo gramu 50 na kukimbia nayo, hivyo wanabaki kuanguka,...
"angalia chalii mgeni anavyoteseka kule"
Aliongea mwanafunzi mmoja akimuongelea sahi au BB, sahi ni zaidi ya hao walimu wenyewe, lakini kaonywa aende kama mwanafunzi hivyo ajifanye hajui kitu, hivyo sahi alikuwa akianguka kila mara ili kuuonyesha uma kiwa kweli alikuwa hajui kitu
"alijua kuna baga huku"
"ahahahahahaha.... Anashindwa hata na baadhi ya wanawake"
Kuna baadhi ya wanawake walikuwa wakijikaza lakini kuna wengine waliokuwa wakishindwa na mazoezi hayo, hivyo huambulia adhabu kali yoka kwa walimu wao,...

Walifanya zoezi mpaka ilifika wakati wa saa mbili za asubuhi, na wakati huo tayari walishabadilisha mazoezi sasa ni kukroo chini huku wakiwa wameshika silaha ambazo hazikuwa na risasi,.. Na wakati huo mabegi yenye uzani yapo migongoni mwao..
"mambo"
Alikuwa ni dada mmoja hivi mrembo sana aliomsalimia sahi,
Sahi hakuitika kwasababu ya kuchoka kwa mazoezi, na sio kuwa kachoka kweli laa bali yupo kikazi zaidi, anatekeleza maagizo alio pewa na wakuu wake,
"haya mafunzo hayahitaji hasira kaka angu, utaumia"
Aliongea yule dada huku wakiendelea kusota chinj, mana wapo wengi sana na kelele zilikuwepo, hivyo wawili wakiongea kwa mwingine kusikia ni ngumu, sahi hakumjibu yule dada chochiukile, waliendelea na mazoezi lakini dada wa watu alikuwa tu kwa ajili ya kufahamiana na kijana huyo, ila sahi kwa kujifanya kuchoka hakuweza kumwitikia,...
Sasa walipokuwa wakiendelea kusota kimazoezi, ghafla sahi aliona baadhi ya wanafunzi kama saba hivi, wakiwa wanachepuka katika njia nyingine tena walimu wao ndio waliokuwa wakiwaamuru kufanya hivyo,.. Wakati huo hakukuwa na mtu alio ona zaidi ya wale wa mbele pale, hivyo watu wa nyuma au hata katikati hawawezi kuona kutokana na majani makubwa kutawala msitu,..
"Samahani dada angu, eti wale wanapelekwa wapi"
Sahi aliona bira avunje ukimya, japo hakuambiwa aipeleleze TMA yeye kaja ili kupata nguzo ya kazi yake, sasa alishangaa kuona baadhi ya wanafunzi wanapitishwa njia za pembeni na mwalimu wao
"nilikusalimia ukanichunia, sasa waniuliza nini"
"Samahani, nimechoka eti si unajua nimekuja jana tu"
"hata salamu pia"
"ok sorry kwa hilo"
Ilibidi aombe radhi kwa kutomwitikia salamu yake,... Lakini sahi kila akipiga jicho, anaona wanazidi kwenda tu
"sikiliza we mkaka, hapa jeshini fuata ulichokifuata, vinginevyo utapelekwa kua mpishi wa wenzako"
"una maana gani dada angu"
Aliuliza sahi huku wakizidi kupitwa na wenzao...
"salehe na mwajuma, naomba msimame"
Sahi na mwaju walionekana na mwalimu wao kuwa hawakuwa wakikroo bali walikuwa wakiongea huku wakiwa wamelala kama wanakroo kumbe laa,....
"umeona sasa, mpaka tumeonewa, we makaka vipi... Haya sasa tutapewa adhabu kubwa hapa"
Aliongea mwaju huku akitia hofu juu ya adhabu watakayo pewa na kamanda wao,
"mumekuja kufanya mazoezi au mumekuja kuongea"
Aliongea kamanda baada ya kuwatoa nje ya mstari,...
"Samahani afande, mimi ni mgeni hivyo nilikuwa nahisi maumivu katika tumbo, baada ya kuburuzika, sasa ndio huyu dada akawa ananiambia nijitahidi, ndipo ukatuona"
Aliongea sahi huku akishika tumbo kama vile anaumwa kweli,
"sasa kwa adhabu yenu, mnatakiwa mrudi mwisho, yaani wale wa kwanzo kutoka mwisho, wawe wa pili kutoka mwisho.. Tena muende kwa kuruka ruka"
Duuuu mwaju alishika kichwa mana hio mwisho yenyewe ilipo ni mbali sana afu uende kwa kuruka ruka kichura,... Hawakuweza kupingana na agizo la kamanda... Walitii japo kwa maumivu makali sana,..

Sasa sahi alpofika eneo la tukio, pale walipokuwa wanachepuliwa wale wanafunzi wengine,... Sahi alitamani sana kupita kwenye hako kamchepuko, mana yeye kama mpelelezi ana haki ya kujua kinachoendelea huku kwenye njia hii tofauti na wengine,...
"unataka ufanye nini"
Aliongea mwaju, huku sahi akijiandaa kuruka,..
Wakati huo mqaju anauliza yeye yupo mbali nae, mana wapo mwisho kabisa,..
"nataka nikajue wameenda kufanya nini wale, usikute wenzetu wanapewa mafunzo mazuri zaidi"
Sahi alisema hivyo, ili kumzuga mwaju asijue kama yeye ni mpelelezi,
"wewe mkaka, umekuja jana tu... Na hicho Kiherehere chako kitakuponza... Mazoezi ni haya haya hakuna mazoezi mengine"
Lakink wakati huo salehe wala hakutaka kumsikiliza mwaju, yaani kama kazi yake inavyomruhusu kufanya.... Sasa ile sahi anajiandaa kuruka ili kutua pembeni alishtukia kukamatwa mguu wake, na kujikuta anarudishwa katika line...
"lazima tukuchunguze kwa undani zaidi... Na utasema wewe ni nani hapa TMA"
Ilikuwa ni sauti ya mtu mwingine kabisa ambae hata hamjui, tena alivalia mavazi ya kiuwalimu, kana kwamba huyo ndio yule mwalimu aliowachepusha wanafunzi saba... Sasa sahi kaja na moto ambao hakutakiwa kuwa nao,.. Yaani kaanza kubainika akiwa na siku ya pili jeshini

Je? Nini Kitaendelea???? USIKOSE

ITAENDELEA.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom