Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Kila Mtu Apambane na Hali Yake

Ni Jumatatu na ndo inaelekea kuisha, nakusalimia Kapuku mheshimika sana. Unajua kabisa sitochoka kukwambia hapa KF ni sehemu bora sana tu kwa kuwa wewe upo hapa, bila wewe hapa ni sehemu tu ya kawaida kama maeneo mengine. Uwepo wako hapa unaongeza madini wacha wapiganie makinikia.

Nilikumiss wikend yote, ndiyo, kuna kumiss na kumissiana na kwangu missing someone so dear like you is a two way traffic, naamini ulinimiss pia. Asante kwa wadau wote ambao leo jumatatu sitowataja maana wao huwa wanatuamsha kwa magazeti, BBC, hadithi, sala (leo imekuwepo, asante aunt yangu), historia na picha bila kusahau kumi kubwa na leo tumeangalia magonjwa. Nimejua mengi kupitia nyingi wadau wote wa KF, michango yenu ni informative, civilized na zaidi inahimiza utangamano (harmony!!!!). Kwanini hili lisiwe Jukwaa bora kabisa kwa sasa hapa JF, ikiwa wewe ni sehemu yake! Shangaa hata wewe, kila mtu apambane na hali yake, naupenda huu msemo, jua hilo.

Muziki sasa, kuna muziki au wimbo unatengenezwa studio na ukitoka unaona kabisa kuna watu walikaa chini na kuvipa kazi vichwa vyao na si kuvipaka mate vichwa vyao. DJ Ganyani toka kwa mzee wa After Sex Shower (JZ) utamsikiliza hapa na utaupenda muziki wake, jamaa anajua kuchanganya muziki na ninamfananisha na DJ Kobo-

Burudika haka akiwa kamshirikisha FB



Baaday tutapata wadhamini na kama kawaida ni furaha kusikia chaguo lako

Asante Obe kwa music
 
HatersGonnaHateSkateBoard.gif
 
Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio na haki kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi

Nikasema moyoni ni kwa sababu ya wanadamu ili Mungu awajaribu nao waone ya kuwa wao wenyewe wafanana na wanyama

Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama jambo moja lawatukia anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu naam wote wanayo pumzi moja wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama kwa maana yote ni ubatili

Wote huendea mahali pamoja wote hutoka katika mavumbi na hata mavumbini hurudi tena
MUHUBIRI 3:17:20

Niwatakie usiku mwema mlindwe na damu ya Yesu
Amen, Asante mtoto wa Mama mchungaji kwa neno la uzima

Nawe pia usiku mwema
 
Yaani unajua wewe ndo mtu unayeniunga mkono kwenye mambo yangu muhimu.

ulinifundisha kuweka maua, kuna mharamia mmoja akayaficha na hajaniambia kayafichia wapi. Hebu nisaidie bhana.
Ujue usiponisaidia wewe hakuna mwingine wa kunielekeza kurudisha maua kwa kipenzi changu
Binamu nilikuelekeza mpaka screenshot nimekutumia sijui simu unayotumia jaman kwangu kuna emoj za aina mbili kuna emoji chini pembeni ya keyboard na kuna emoji nyingine juu ya keyboard hapo ndio mauwa yanapopatikana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom