Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kipa wa Manchester United David de Gea, 26, anataka kujiunga na Real Madrid msimu huu na amemuambia wakala wake Jorge Mendes kufanikisha uhamisho wake. (Don Balon)
 
Manchester City wapo tayari kutoa pauni milioni 50 kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22. (Daily Mirror)
 
Chelsea watakamilisha usajili wa kiungo Tiemoue Bakayoko, 22, kutoka Monaco kwa pauni milioni 39.7 katika saa 24 zijazo, ingawa mchezaji huyo atakosa mechi kadhaa za mwanzo kutokana na kuwa majeruhi. (Daily Express)
 
Barcelona wameacha kumfuatilia beki wa Arsenal Hector Bellerin, 22, baada ya klabu hiyo ya Uhispania kufikia makubaliano ya kumsajili Nelson Semedo, 23 kutoka Benfica. (London Evening Standard)
 
Tottenham wanatarajia kuziba pengo la Kyle Walker kwa kumsajili beki wa Porto Rocardo Pereira, 23, kwa pauni milioni 22. (Times)
 
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anataka uhamisho wa Kyle Walker, 27, kwenda Man City uharakishwe ili wapate fedha za kusajili wachezaji wengine. (Daily Mail)
 
Tottenham wanakaribia kukamilisha usajili wa beki Juan Foyth, 19, kutoka Estudiantes, ambaye atakuwa usajili wa kwanza wa Spurs msimu huu. (ESPN)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom