
ZABURI 100
1.Mfanyieni BWANA shangwe,dunia yote;
2.Mtumikieni BWANA kwa furaha;Njoni mbele zake kwa kuimba,
3.Jueni kwamba BWANA ndiye MUNGU Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake.,na kondoo wa malisho yake.
4.Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru;Nyuani mwake kwa kusifu;Mshukuruni ,lihimidini jina lake;
5.Kwakuwa BWANA ndiye mwema ;Rehema zake ni za milele;Na uaminifu wake vizazi na vizazi.

Asante BABA kwa mchana wa leo ,tunakushukuru,tunakutukuza ,tunakuabudu ,tunakuheshimu maana wewe ni mwema kwetu unatulinda,unatutunza unatutia moyo hata hatuangamii kwa mapito yoyote..asante kwa yote yanayoendelea mahali hapa tunakushukuru maana wewe ndiye unayawezesha yote,asante kwa ajili ya MAKAPUKU WOTE Endelea kutubariki BABA na kuimarisha Upendo uliopo .
Tunaendelea kukabidhi kazi zetu,mipango yetu,changamoto zote,wagonjwa na wenye shida mbalimbali nyoosha mkono wako maana mkono wako si mfupi ,gusa kila mmoja wetu akakuone MUNGU wetu na AMANI ITAWALE
TUNAOMBA NA KUSHUKURU AMEN
MCHANA MWEMA
Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app