Muziki: Ijumaa ya Kimyakimya
Well, kabla sijakusalimia
Kapuku mwenzangu ningependa kutofahamu utafanya nini katika siku hizi mbili za mapumziko. Ni mapumziko, si ndiyo jamani, na kama ni mapumziko sasa kwanini nauliza utafanya nini (got any plans this weekend?). Binafsi nitapumzika sana maana wiki hii ilikuwa ndefu kidogo na yenye kona nyingi isingekuwa assist za wadau basi hata sare nisingeambulia. Tujipongeze kwa kutoa assist na kuwa assisted bila kuasiliwa.
Leo ni SabaSaba, sikukuu ya Wakulima hapo mwanzo na hujuma za wafanyabiashara wakaipoka kuifanya siku ya kuuza bidhaa za viwandani. Hongereni sana wote mliotumia siku ya leo kununua bidhaa za viwandani na kuwaunga mkono wafanyabiashara wetu nchini. Ukiwaunga mkono basi uchumi kupaa hakuepukiki. Nunua bidhaa za ndani, usipende za nje utakaa uchi.
Muziki sasa, leo ni Ijumaa sina haja ya kukukumbusha mdau na Kapuku mwenzangu ambaye uwepo wako tu hapa na wewe kuweza kusoma forum hii unakuanya kuwa mtu mwema sana, vinginevyo ungekuwa jela ukiishi bure. Kuwa raia mtiifu ni wajibu wetu kila mmoja.
Turudi zamani kidogo kwa sisi vijana wa jana enzi za kutembea na mabegi mgongoni (yamerudi tena) na story za mamtoni miguuni tumetinga raba mtoni. Anaitwa Dudubaya aka Mamba, kapafona- mshindi wa tuzo ya muziki tanzania kwa wimbo wake nakuppenda tu na zaidi navutiwa na wimbo wake mwanangu huna nidhamu.
Sakayo uliomba wimbo wowote wa Mapafu ya Mbwa (DuduBaya) sasa furahia na Makapuku wote
Furahia wakati huru huu tulionao. Nakupenda tu.
NB: Kwa matatizo ya kiufundi wasiliana na mtaalamu wa masuala ya ufundi mtaasisi
Nyagei