Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Ijumaa ya Kimyakimya

Well, kabla sijakusalimia Kapuku mwenzangu ningependa kutofahamu utafanya nini katika siku hizi mbili za mapumziko. Ni mapumziko, si ndiyo jamani, na kama ni mapumziko sasa kwanini nauliza utafanya nini (got any plans this weekend?). Binafsi nitapumzika sana maana wiki hii ilikuwa ndefu kidogo na yenye kona nyingi isingekuwa assist za wadau basi hata sare nisingeambulia. Tujipongeze kwa kutoa assist na kuwa assisted bila kuasiliwa.

Leo ni SabaSaba, sikukuu ya Wakulima hapo mwanzo na hujuma za wafanyabiashara wakaipoka kuifanya siku ya kuuza bidhaa za viwandani. Hongereni sana wote mliotumia siku ya leo kununua bidhaa za viwandani na kuwaunga mkono wafanyabiashara wetu nchini. Ukiwaunga mkono basi uchumi kupaa hakuepukiki. Nunua bidhaa za ndani, usipende za nje utakaa uchi.

Muziki sasa, leo ni Ijumaa sina haja ya kukukumbusha mdau na Kapuku mwenzangu ambaye uwepo wako tu hapa na wewe kuweza kusoma forum hii unakuanya kuwa mtu mwema sana, vinginevyo ungekuwa jela ukiishi bure. Kuwa raia mtiifu ni wajibu wetu kila mmoja.

Turudi zamani kidogo kwa sisi vijana wa jana enzi za kutembea na mabegi mgongoni (yamerudi tena) na story za mamtoni miguuni tumetinga raba mtoni. Anaitwa Dudubaya aka Mamba, kapafona- mshindi wa tuzo ya muziki tanzania kwa wimbo wake nakuppenda tu na zaidi navutiwa na wimbo wake mwanangu huna nidhamu. Sakayo uliomba wimbo wowote wa Mapafu ya Mbwa (DuduBaya) sasa furahia na Makapuku wote
Furahia wakati huru huu tulionao. Nakupenda tu.




NB: Kwa matatizo ya kiufundi wasiliana na mtaalamu wa masuala ya ufundi mtaasisi Nyagei

Asante saaana Obe wa Husna

Umejua kunibamba ile kinomaaa
 
MATHAYO 5

14.Ninyi ni nuru ya ulimwengu,Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15.Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi,bali juu ya kiango;nayo yawaangaza wote walio nyumbani.

16.Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu,wapate kuyaona matendo yenu mema,wamtukuze BABA yenu aliye mbinguni.

MBARIKIWE
 
MATHAYO 5

14.Ninyi ni nuru ya ulimwengu,Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15.Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi,bali juu ya kiango;nayo yawaangaza wote walio nyumbani.

16.Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu,wapate kuyaona matendo yenu mema,wamtukuze BABA yenu aliye mbinguni.

MBARIKIWE
Nakupenda mamy...
 
MATHAYO 5

14.Ninyi ni nuru ya ulimwengu,Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15.Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi,bali juu ya kiango;nayo yawaangaza wote walio nyumbani.

16.Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu,wapate kuyaona matendo yenu mema,wamtukuze BABA yenu aliye mbinguni.

MBARIKIWE


Ubarikiwe nawe pia, nuru yetu na iangaze. Hivi si kuna maneno yanasema Amka Uangaze?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom