Makapuku Forum

Mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, ametoa sharti la kuwa mchezaji anayelipwa zaidi- nyuma tu ya Cristiano Ronaldo- iwapo Real Madrid wanataka kumsajjili (Diario Gol).
 
Meneja wa Leicester City ametoa dau la pauni milioni 20 kumtaka mshambuliaji wa Watford Troy Deeney, 29 (Daily Mirror).
 
Tottenham wanataka kumchukua kiungo wa Everton Ross Barkley, 23, lakini hawapo tayari kulipa pauni milioni 50 wanazotaka Everton (Sun).
 
Juventus wamempa beki wao Alex Sandro, 26, mshahara wa pauni 84,000 kwa wiki ili kumshawishi asiondoke kwenda Chelsea ambao wapo tayari kutoa pauni milioni 61 kumnunua (London Evening Standard).
 
Beki wa Arsenal Hector Bellerin, 22, ameiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka, lakini meneja Arsene Wenger amekataa ombi lake la kutaka kuondoka. Barcelona wanataka kumsajili beki huyo kwa pauni milioni 35 (Daily Express).
 
Crystal Palace wanafikiria kusajili mabeki wawili Joel Veltman, 25, na Kenny Tete, 21, kutoka Ajax kwa pauni milioni 10 (Guardian).
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…