Ni vita kati ya wanaume na wavulana
Wachile wanatandaza ubabe uwanjani.....Wajerumani wao wanatandaza soka
Itakuwa ni mechi ngumu maana walishakutana hatua ya ma kundi na kisha 1:1 ila leolazima mmoja afungwe hata kwa penati
......
Wakuu tuko salama ...leo ndo leoo mm hapa naomba Tanesco wasifanye yao make nataka nishuhudie bila kuhadithiwa ....
Alichokianza Ujerumani na under 21 yake ndo anachokifikiria Chile ya wakubwa chini ya mtu wa thamani yake kipenzi cha clkey kabla ya Mjerumani mwenyewe kuwaonesha wajerumanii kuwa yeye ni mjerumani haswaaaa ....hii ndo raha ya kabumbu wanapigana wao na sisi tumo....swaaaaaaafiiiiii....ila mpira dakika 90 twasema ...
Wakiwa wanaendelea na majaribio ya Teknolojia yao sisi tunapambana kivyetu kuona kama ata siku moja tutakuja kutofautisha mpira na siasa ....siasa kweli kweliiii .....usichokee wee pitia twende wote nimepitia replay naona watu mshachagua timu zenu ....ongera ila ata ukifungwa kumbuka ata sisi tunatamani tuwe kuleee ...sio mbaya ata na sisi tunacheza robo leoo

japo yawezekana tunaocheza nao hawajui wanacheza na wakina nani ....kaziiiii kweliiii make wanataka watuchonganishe na Bitoz na wenzake wa pale katii mjini pembenii ......
Twende sawaaa sasa ...experience ya kikosi cha Chile katika hatua kama hii ya fainal ndio moja ya silaha tosha za kumwangamiza Ujerumani..... Aina ya kikosi chao kilichofika hatua kama hii mara mbili mfululizo kule CONMEBOL dhide ya ya Argentina ni kile kile.... Sina shaka na kasi yao katika kupanga mashambulizi kuanzia kwa golikipa mpaka kwa washambuliaji... Shaka yangu ni namna watakavyoweza kuwakabili Wajerumani ambao pamoja na vipaji, umri walionao Bado wanaonyesha mpira wao umeanzia darasani kwanza.....darasanii ndio usiniuluzee la ngapii
......Chile wamekuwa ni wazuri sana unapowaruhusu wafanye kile watakacho katika dk 90 za mchezo... Ila pia wamekuwa bora sana katika kutafuta ushindi kwa njia nyingi hii ni kutokana na quality ya wachezaji waliopo katika kikosi chao.... Wanaweza kuamua matokeo muda wowote kutokana na nafasi wanazopata ila pia kutokana na makosa yanayofanywa na mpinzani.
Wastani wa umri kwa kikosi cha Ujerumani nao ni kitu pekee kilichowafanya kufika hapo walipofika, ila pia wastani huo ndio unaweza kuwa kikwazo kwa ile kasi ya chile kutokana na uhalisia wa umri wakikosi cha Chile, Chile wanaonekana kuwa na umri ambao sio rafiki sana kukutana na timu yenye vijana na vipaji vyao..... Ukiachia ubora wa miguu ya Wajerumani basi umri ni kitu kilichowashangaza Wengi katika mashindano haya ya mabara huko urusi. Vijana wa Joachim Low wanaonekana Bado wana nguvu ya kucheza muda mrefu zaidi tofauti na chile ambao wamedumu kwa muda sasa na kikosi chao.
Kumbuka mchezo wao wa kwanza katika mashindano haya walikutana katika makundi na hakukuwa na mbabe baada ya wao kutoa sare ya bila kufungana.... Ubora wa safu ya ushambuliaji ya Ujerumani unaonekana kuwa juu sana hii ni kutokana na kufunga magoli 11 mpaka kufika katika hatua hii ya fainal tofauti kabisa na wenzao chile wao uzoefu umechangia sana kuwafikisha katika hatua hii huku safu yake ya ushambuliaji mkifunga jumla ya goli 4 tu mpaka kufika fainali.
Sebastian Rudi ni mjerumani ambaye amekuwa mhimili wa timu haswa katika eneo la kiungo cha chini anachocheza na kuwafanya Rudiga na Mustafi kuwa wagumu sana kupitika... Marcelo Diaz huyu naye amekuwa kiini cha ubora wa chile pale katikati na ubize wake umemfanya Vidal kuwa huru sana katika kushambulia pamoja na kuchezesha timu.
Pamoja na chile kuwa na uzoefu Mkubwa wa kucheza fainal, lakini pia bado watachangizwa na ubora wa Ujerumani katika kuufanya mchezo mgumu kuwa mrahisi....... Atakaye kuwa bora ndiye atakayenyanyua makwapa........
Sanaaa,ila mie nataman Ujerumani wafungwe bwana