
ZABURI 67
1.MUNGU atufadhili na kutubariki,Na kutuangazia uso wake.
2.Njia yake ijulike duniani,Wokovu wake katikati ya mataifa yote.
3.Watu wakushukuru Ee Mungu,Watu wote na wakushukuru.
4.Mataifa na yashangilie,Naam,waimbe kwa furaha,Maana kwa haki utawahukumu watu.Na kuwaongoza mataifa walioko duniani.
5.Watu na wakushukuru,Ee Mungu,watu wote na wakushukuru.
6.Nchi imetoa mazao yake MUNGU ,Mungu wetu ametubariki.
7.MUNGU ametubariki sisi ;Miisho yote ya dunia itamcha Yeye.
MUWE NA SIKU NJEMA,TUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO...MBARIKIWE