Makapuku Forum

8/James Hogue Alizaliwa 1959
Huyu bwana alifanya udanganyifu wa vyeti ili asome Princeton University kama alichofanya Daudi Bashite huku bongo ila huyu mzungu ndo kiboko
Kwanza kabisa alitengeneza/iba vyeti vya marehemu wa miaka 16 aliyekuwa mwanafunzi wa Sekondari huko Nevada kisha akajifanya pia ni yatima kwa vyeti vingine na kufanikiwa kugusa "Mlimani" tena kwa kusoma km yatima na hivyo kupiga assist sehemu kibao ila mwaka wa kwanza tu akaharibu baada ya kuiba baiskeli
Ila mwisho wa Siku utambulisho wake halisi ukagundulika mwaka 1991
......
 
7/Eduardo de Valfierno
Huyu ni tapeli wa Kiargentina
Huyu bwana ndo aliyefanikisha kuibwa kwa picha ya Monalisa
Alijifanya Marquis na kutafuta watu na kuwalipa kisha wakaiba picha ikiwa Makumbusho mwaka 1921
Baada ya aliyemtuma kuiba na kusepa huyu jamaa akala kamisheni na watunzaji na kutoa kopi 6 za picha hiyo
Na msala ulikuwa mrefu kiasi Ni ngumu juuelezea wote
.......
 
Ila sasa huyu Bashite nae alikuwa mpuuzi. Sasa baiskeli aliiba ya nini???
 
6/Soapy Smith Alizaliwa nchini Marekani 1860
Alikuwa ni msanii,tapeli na pia alimiliki genge lililokuwa lokijihusisha na Organised Crimes nchini humo
Alikuwa maarufu kwa kuanzisha "tripe and keister" katika kona zenye msongamano mkubwa wa watu mtaani na na kuuza keki za sabuni(keki feki) na kukusanya makumi kwa mamia ya watu kisha kuanza ujanjaujanja ila mwisho wa siku aliondoka na mpunga mrefu kwa kitapeli
.......
 
Duh!
 
Huyu mlatino nae ni kiboko kabisa kwanza mwizi halafu pia anajua ku-assist

Maana aliiba picha kisha aka assit vile vile
 
Hahahahaha hizo
Kwani keki ina gharama gani hata mtu utengeneze feki?? Huyu alitakiwa hata kufungwa maisha
 
5/George Parker
Alizaliwa 1870
Huyu ni Rainyundo katika historia nchini Marekani ....alifanikiwa hadi kuwatapeli watalii kwa kuwauzia mji(ardhi) ya jiji la New York
Hakuishia hapo, alifanikiwa kuliuza Brooklyn Bridge mara mbili kwa wiki kwa miaka kadhaa
Alifanikiwa kuwatapeli watu kibao pia kwa kuwauzia Madison Square Garden na utapeli kibao ambao naweza kujaza page nzima hapa
Huyu kwangu Ndo mpiga assist japo matapeli wanatogautiana
......
 
Alivyo na macho mazuri sasa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…