Muziki: Fikiria Ajira
Ni jioni tena na ndo tumeshaimaliza siku. Hongera sana uliyemaliza kazi na kazi njema kwa wewe unayeelekea au bado unapiga kazi. kazi ni kazi ila iwe halali tu kwa mujibu wa sheria na kanuni bila kusahau taratibu zinazokubalika na familia.
Nilikuwa na siku nzuri leo, sana na muda wote nilitembea huku natabasamu hasa nikikumbuka kuwa nilitoka home bila kuoga ila nikajikandika mafuta usoni na kujipulizia pafyumu kibao (natumia Lara Wild Cologne) na deodorant ya Speed Stick magic 24. Nikawa natabasamu kama customer care wa Jaza Ujazwe. Safi sana kwenu wote mlioamua kuianza na kuimaliza siku bila kuoga, tupo wengine tunapenda harufu za vikwapa.
Nimesoma humu kuwa kuna nyuzi zimeanzishwa na kutishia uhai wa Makapuku Forum, hivi hizi zinazoanzishwa zina maudhui kama ya MF? na je MF inashindanishwa nazo kwa kipi? MF ni kokoro, kuna kila kitu utapata humu, mafundi wa siasa hadi wapigakura, wapenzi hadi wapenzi wasikilizaji, walimu hadi wanafunzi, maprofesa hadi mapropesa, waheshimiwa hadi watoa heshima. Wote tumo humu na hatushindani na yeyote, wanaweza kudhani wanashindana na MF ila ukweli unabaki kuwa ukweli hauna kutu MF ni zaidi ya thread, ni Jukwaa.
Muziki na utamu wa gitaa ndiyo sasa wakati wake, ndugu Makapuku wenzangu (fikiria kama natoa risala vile) mara nyingi tangu nianze kuleta hii kipengele ya muziki na utamu wa gitaa nimekuwa sijawaangalia sana wanaochipukia kwa kucopy nyimbo ambazo zimetamba. leo ni siku yao na kwa kuwa wako kwenye siku yao basi tuwaheshimu pia.
Kwetu hapa kulikuwa na BSS ambayo mwanzoni ilikuwa poa sana na niilifuatilia vizuri, baadaye ikawa too commercialized kiasi kwamba ikawa ni matangazo mengi kuliko kuwaandaa vijana kuibuka kwenye muziki. Nikahamia TPF hawa walifanya vizuri sana pia.
Leo nitakuonjesha ladha kidogo ya TPF, angalia muziki live ulivyotulia na kama kawaida gitaa linasikika kwa utamu kabisa.
Burudika na kitu cha Tabu Ley Muzinaaaaaaaaaaaaaaaa
Hadi wakati mwingine, nakupenda mdau mwenzangu wa Makapuku. Usisahau ajira uliyonayo na unayoisaka sio tu kwamba inafaida kwako bali ni muhimu kwa maendeleo yetu kama taifa. Zidi kutabasamu hata kama hujaoga.