
ZABURI 34
1.Nitamtukuza Mwenyezi- Mungu nyakati zote,sitaacha kamwe kuzitamka sifa zake.
2.Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi -Mungu wanyonge wasikie na kufurahi.
3.Mtukuzeni Mwenyezi - Mungu pamoja nami,sote pamoja tulisifu jina lake
4.Nilimuomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu ,na kuniondoa katika hofu zangu zote.
5.Mgeukieni Mungu mpate kufurahi ,nanyi hamtaaibishwa kamwe.

BABA Asante kwa kutuamsha salama,tunakushukuru sana kwani wapo wengi walitamani kuiona siku ya leo hawajaweza ,hatuna cha kukulipa bali kukushukuru,kukutukuza,kukuheshimu na kulisifu jina lako Takatifu daima.
Siku ya leo BABA tunakuomba tuponye,tufariji,tuongoze,tusaidie kukupenda wewe zaidi na zaidi,tuwapende wenzetu,tuwainue,tuwafariji tuseme nao kwa upendo,tufanye kazi kwa bidii na kukushukuru kwa kila jambo maana wastahili sifa Mfalme wa Amani.
Bariki kila kinachoendelea mahali hapa tukifanye kwa utukufu wa jina lako takatifu,mbariki kila KAPUKU mahali hapa auone ukuu wako na asipungukiwe Upendo,Amani,Mshikamano, Busara,Hekima na Maarifa maana umetuweka pamoja BABA na unalo kusudi nasi TUNAKUSHUKURU,Ondoa hofu kwa kila mmoja wetu BABA mwema.
ASANTE maana utatutendea sawa na mapenzi yako,Ondoa vikwazo na changamoto zinazoweza kutuweka mbali nawe.
Katika jina la YESU mpatanishi na mwokozi wetu Amen.
MUWE NA SIKU NJEMA WAPENDWA WANGU

MBARIKIWE