Muziki: Heshima kwa Mtoto
Ni Furahiday leo! Usijibu kabla sijauliza maswali ya siku yako ilikuwaje leo. Naamini kabisa nikiuliza siku yako ilikuwa vipi basi hapa tutalkesha kwa majibu tofauti tofauti ya raha na karaha kwa pamoja, itoshe tu kujiaminisha kuwa wote tumekuwa na siku nzuri kabisa. asante kwa yule aliyetujaalia uwezo wa kufanya kazi na kujitafutia kipato kwa njia za halali. Hongera kwa wote mnaojitafutia vipato visivyo vya halali, jela nasikia kuna disco.
Leo ni siku ya Mtoto wa Afrika. Inaweza kuwa si maarufu sana upande wako lakini bila kujali nakujulisha tu kwa hisani ya
Mussolin5 kuwa siku hii ilitengwa maalum kabisa kama kumbukizi ya watoto waliouawa kule South Africa mwaka 1976 na OAU (AU ya enzi hizi) mwaka 1991 ikaitenga June 16 kuwa Siku ya Mtoto wa Africa, yes mtoto na sio wale mabeibe meno 32 na tayari hawaoti meno tena.
Nini tumfanyie huyu mtoto wetu. Tumhakikishie lishe bora akue mwili na ubongo sio kila siku wali maharage tu unasahau mchicha, mkarango, matunda. Tumpeleke shule ajipatie maarifa yanayohitajika na aweze kukabiri dunia hii, akikua kua tu umfundishe kuhusu uzazi ili aweze kuzalisha vizuri muda ukifika.
Tumpe nafasi afanye analopenda huku tukimguide tu na sio kumuonyesha apende nini. Tumfanye ajiamini sio unamfanya atumie mavyombo ya plastic siku zote, siku wakija wageni uakatoa zile sahani ulizofungia kabatini basi anabaki kung'aang'aa macho tu utasema wanasiasa wetu bungeni.
Nini tusiwafanyie watoto, moja tu kubwa. Tusiwabake, eeeh, mawazo machafu yamekujia, usibake haki zake, usimuangalizishe simu yako iliyojoo ponografia, usimsikilizishe muziki usioeditiwa na zaidi usimsikilizishe vipindi vya hovyo vya radia au kuangalia tv. usimruhusu alale anapotaka.
Unamjua Lokua Kanza wewe! kama humjui sio shida maana hata rais hamjui aliyetusainisha mikataba mibovu ya madini. Lokua ni mwanamuziki na mtayarishaji wa muziki, anaujua. Anapiga gitaa na ana sauti nzuri na utaifurahia kuisikiza.
Leo tunakwenda kislow na hakuna anayeruhusiwa kumbambia mwenzake labda hug za kimisonari au za kiislamu. na kwa upendeleo wa aina yake (haijapata kutokea) nakuwekea songi lake moja kaliimba sehemu mbili. Utapenda maana nakupenda sana Kapuku mwenzangu.
Mlinde Mtoto, Lipa Kodi Asome, Apate Tiba na mfundishe kusema kweli daima (sio kama ile ahadi ya TaNUOCSM)