Aksante sana1/Opray Winfrey
Alizaliwa katika familia fukara ya Single mother lakini akakomaa na kuja kuwa bilionea na mwendesha vipindi maarufu
Alibakwa utotoni na pia alipoteza kichanga chake sijui wakati wa kujifungua ndo mtoto walifariki
Ana vidole 6 mguu wa kushoto
.
.
.
.
.
Cha kujifunza wengi wao hao ni matajiri na walikuwa na uwezo wa kuviondoa vidole vyao ila wakaamua kujikubali na maumbile yao hata walipopata umaarufu au kuchekwa
.
.
.
.
Shukrani kwa mliosapoti mada
Tukutane Jumatatu
Mwisho
......
1939 - Meli ya MS St. Louis iliyokuwa imebeba wayahudi takribani 900 inakataliwa kuingia jimboni Florida nchini Marekani hivyo inageuza kurudi Ulaya ambapo Wayahudi 200 kati ya hao 900 wanaenda kuuwawa katika magerezaya mateso ya NAZI.
So sad. Ingefanywa na Rais wa Nchi nyingine sidhani kama wangemsamehe!!
Walikuwa ni wakimbizi,walikuwa wanakimbia Mauaji waliyokuwa wanafanyiwa na Hitler na genge lake la NAZI
Walifuata tartibu ikiwepo kuomba VISA lakini wakakaushiwa na Rais wa USA enzi hizo Franklin D. Roosevelt akisingizia mdororo wa uchumi (Great Depression)
Hivyo kujikuta meli inageuza na kurudi huko kwao na Hitler kufanya yake
.....
Pamoja KomrediAsante kwa leo katika historia musolini
Aksante Fundi wa music!!Safari na Muziki
Ni usiku sasa hapa kwetu, lakini JF na hasa Makapuku ni kama himaya ya Muingereza enzi hizo. Unaweza kuta saa hizi ni saa sita mchana sehemu fulani na wote tumo humu humu Makapuku.
Jukwani humu leo kama tulivyoona kulikuwa na vioja, well, kuna kutukanana na sababu, lakini kama mtu anakuja tu anaanza kutukana basi ukimtukana utakuwa umempa heshima. Ila kwa namna tulivyowaaacha tumeonesha kweli humu si mahali pa mchezo mchezo. Asante kwetu.
Furahiday kama kawaida, siongei sana maana sichelewi kuandika yale ninayopenda kiukweli, In vino veritas, (kwenye mvinyo, kuna ukweli). Na maongezi mazuri ni pale mnapoongea wote lock zimeactivatiwa kiweekend.
Tumwangalie mpiga gitaa na muimbaji mzuri wa kiingereza Michael David Rosenberg almaarufu Passenger, mshindi wa Tuzo za Brit Award kwa wimbo 'Let Her Go'.
hebu burudika wakati naangalie utaratibu wa namna gani nitaondoka hapa maana sipaelewi elewi hapa nilipokaa.
Nikutakie wikend Njema sana na sitochoka kukwambia, Wewe ni Mtu Muhimu Sana Hapa Makapuku Forum. LLL
Nimemwangalia Passenger naye nimeona ana vidole sita au well, sijahesabu sawasawa. Wakati wenzangu wanaenda na visoda kufundishwa kuhesabu mimi nilikuwa nachunga tu mbuzi
Duh, watu walijua utani!!Aisee, huwa inaleta shida sana
Dada mmoja tulikuwa tunafanya naye kazi, alifariki gafla tu asubuhi mme wake akanipigia simu ya kunijulisha, muda huo huo nikatuma sms kwa watu wote wa ofisini, kila mtu aliniambia mimi muongo nani siku ya wajinga humpati mtu, walipoona funguo ninazo mimi wakasema tumefanya dili, baadaye manager ndio akatoa tangazo, hawakuamini
Men at work!!Mike Tyson and David Tua - The Most Powerful Punchers in Boxing History...Na ukisikia Men at Work ndo hii sasa...
1979 - Luteni Jerry Rawlings anachukua madaraka ya Kuiongoza Ghana mara baada ya kupinduliwa kwa Jenerali Fred Akuffo katika Mapinduzi ya Kijeshi.
1986 - Jasusi wa Kimarekani, Jonathan Pollard anakutwa na kosa la kuuza siri nyeti za kijeshi za Serikali ya Marekani kwa Israel, anahukumiwa kifungo cha Maisha Jela.
Ok
Alikiri mwenyewe kosa Mahakamani ..hii inaitwa Plea of guilty
Alitiwa mbaroni kuanzia Nov 21 1985
.....
1915 - Modibo Keita anazaliwa.
Alikuwa ni Rais wa kwanza wa Mali.
1971 - Joseph Kabila anazaliwa.
Ni Rais wa Jamhuri ya Demokrasia ya watu wa Congo.
1975 - Angeline Jolie anazaliwa.
Ni muigizaji wa Movie kutoka nchini Marekani.
Moja ya movie zilizompa umaarufu ni Salt.
Amenogewa na madaraka. Anadhihirisha tabia halisi tulizonazo Waafrika.Aliingia madarakani Jan 2001 baada ya baba yake(Kabila Sr) kuuawa
Tangu hapo amekuwa ni king'ang'anizi wa madaraka ambapo mwaka huu ameahirisha Uchaguzi kabisa
.....
1982 - Abel Kirui anazaliwa.
Ni mwanariadha wa mbio ndefu nchini Kenya.
1983 - Emmanuel Eboue anazaliwa.
Beki wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Ivory Coast.
1985 - Lucas Poldoski anazaliwa.
Mshambuliaji wa zamani wa Fc Koln, Bayern Munich, Arsenal na timu ya taifa ya Ujerumani.
Alitwaa kombe la dunia la mwaka 2014