Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 183,582
- 1,105,382
Swali bado ni la jumla mno na kimantiki lina fatal flaw. Tunamlinganisha na waliomtangulia katika vigezo gani? Na ni kweli hao waliomtangulia ndiyo walistahili? Na kwa nini tunataka viongozi wetu wote wafanane kiutendaji, kimtazamo na hata kifalsafa? Hao waliomtangulia na kutuachia mamikataba haya mabovu ya madini yanayotutafuna mpaka leo, ESCROW, RICHMOND, PAP na madudu mengine ukiwemo ufisadi wa waziwazi ndiyo walistahili? Tena wengine kabla hawajaondoka ndiyo wakatutungia misheria hii mikali inayotunyima uhuru hata wa kuweka majina yetu humu. Pamoja na matatizo yote haya naamini pia walitenda mengi mazuri na tunaweza kuwapima kwa kulinganisha mema na mabaya yao lakini kuuliza eti kama walistahili ama la kidogo inashangaza! Si tuliwachagua wenyewe?Tuko pamojaa ..
Sijaweka kigezo chochote nikiwa na maana yangu ...
Anyway ni mda kadhaa tangu tumchague na tumeona au tunaweza kumlinganisha na baadhi ya waliotangulia ..
Je kutokana na maamuzi anayoyachukua mbalimbali (aina ya kigezo) ni sahihi anastahili ukilinganisha wadhifa alionao na maamuzi anayoyachukuaa ??
Nasema tena, na pengine kwa mara ya mwisho, bila vigezo vinavyopimika swali lako halitajibika sawasawa unless kama unataka lijibike kishabiki tu bila kuzingatia mwegamo wa hoja na ukweli. Na mjadala huu hautafika popote!
♂️