Nakisi ya umeme nchini kwa sasa ni kati ya Megawati 300 - 400 hivyo ni dhahiri tatizo la mgao wa umeme linakwenda kumalizika

MTANZANIA620

Member
Jun 20, 2023
34
30
Mgao mkali wa umeme uliopo unatokana na upungufu uliopo katika uzalishaji dhidi ya mahitaji. Kuwashwa kwa Mtambo namba 9 katika Mradi wa Bwawa la uzalishaji umeme la Julius Nyerere ambao unazalisha megawati 235 kuingia katika gridi ya Taifa kunakwenda kuleta nafuu kubwa kwa takribani asilimia 85.

Mwezi Machi, 2024 tutashuhudia mtambo namba 8 nao ukiwashwa ambao nao utazalisha megawati 235 kwenye Gridi ya Taifa. Hivyo kufanya katika kipindi cha miezi miwili kupata ongezeko la megawati 470.

Aidha mwezi Aprili, 2024 kupitia mradi wa uzalishaji umeme wa Rusumo unaotekelezwa na nchi tatu za Tanzania, Burundi na Rwanda chini ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) utakaozalisha Megawati 80 ambazo Kila Nchi mshirika itapata mgao wa megawati 26.66 katika Gridi yake ya Taifa. Hivyo mpaka mwezi Mei, 2024 Gridi yetu ya Taifa itakuwa imepokea Megawati 496.66

Nakisi ya umeme nchini kwa sasa ni kati ya Megawati 300 - 400 hivyo ni dhahiri tatizo la mgao wa umeme linakwenda kumalizika kabisa na kuwa na ziada ya Megawati 96.66

Mpaka mitambo yote iwashwe JNHPP tutakuwa na umeme wa kutosha. Kama Nchi ili kuondokana na kadhia hii na kutoa uhakika wa nishati ya umeme kwa wawekezaji, wafanyabiashara na wajasiriamali ni lazima kuendelea kutekeleza mpango mkakati wa uzalishaji zaidi wa umeme kwa manufaa ya miaka mingi ijayo kazi ambayo serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan wanaendelea nayo.

Pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwani wakati anaingia madarakani mwaka 2021 aliupokea mradi ukiwa asilimia 33 za utekelezaji huku ukiwa umeshalipwa kiasi cha shilingi trilioni 1.45 kati ya shilingi trilioni 6.5 gharama za utekelezaji wake. Leo mradi upo asilimia 98 na mkandarasi akiwa ameshalipwa asilimia 90 ya fedha zote za mradi.

Tuendelee kuziamini hatua ambazo serikali yetu inachukua ili kuondokana na tatizo hili la umeme nchini kwetu.

Mtoto wa Mama Kizimkazi

#HakunaKilichosimama #2025TunaendeleaNaSamia
#KaziIendelee
 
Hapo sasa tutahamishia tatizo kwenye miundombinu ya usafirishaji. Mara utasikia kuna tatizo grid ya taifa!
 
Kuisha kwa tatizo hilo kuendane sambamba na kushuka bei kwa unit kama ilivyokua mipango ya mwendazake
 
WEWE UKO WAPI NDUGU

swala la umeme mambo yako safi kabisa kwa sasa ..tuliwambia mambo ni kimya kimya sasa
 
Vipi ukitokea ukame ? Hatutakuwa na mgawo?

Akili ya mtu mweusi ni Mungu tu anajua alivyoiumba!!

Badala muweke nguvu kwenye vyanzo ambavyo hata nchi ikiwa na ukamwe mwaka mzima bado tutakuwa na umeme mnaendeleza ujinga ule ule.
 
Utaambiwa tumeongeza umeme lakini tatizo ni nyaya bado zilezile nyembamba hivyo umeme unajibana wakati wa kupita, utasemaje? Kumbuka kuawakati tuliambiwa vikombe vya kwenye nguzo vina tope!
Hawa jamaa sijui wanatuonaje, juzi hapa nilishangaa kumsikia mbalawa eti bila kutafuta mwekezaji wa kuongeza gati bandarini suala la foleni za meli za mizigo haliwezi kuisha, huyohuyo alisema dp world ikija foleni ya meli kwisha habari yake
 
Mgao mkali wa umeme uliopo unatokana na upungufu uliopo katika uzalishaji dhidi ya mahitaji. Kuwashwa kwa Mtambo namba 9 katika Mradi wa Bwawa la uzalishaji umeme la Julius Nyerere ambao unazalisha megawati 235 kuingia katika gridi ya Taifa kunakwenda kuleta nafuu kubwa kwa takribani asilimia 85.

Mwezi Machi, 2024 tutashuhudia mtambo namba 8 nao ukiwashwa ambao nao utazalisha megawati 235 kwenye Gridi ya Taifa. Hivyo kufanya katika kipindi cha miezi miwili kupata ongezeko la megawati 470.

Aidha mwezi Aprili, 2024 kupitia mradi wa uzalishaji umeme wa Rusumo unaotekelezwa na nchi tatu za Tanzania, Burundi na Rwanda chini ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) utakaozalisha Megawati 80 ambazo Kila Nchi mshirika itapata mgao wa megawati 26.66 katika Gridi yake ya Taifa. Hivyo mpaka mwezi Mei, 2024 Gridi yetu ya Taifa itakuwa imepokea Megawati 496.66

Nakisi ya umeme nchini kwa sasa ni kati ya Megawati 300 - 400 hivyo ni dhahiri tatizo la mgao wa umeme linakwenda kumalizika kabisa na kuwa na ziada ya Megawati 96.66

Mpaka mitambo yote iwashwe JNHPP tutakuwa na umeme wa kutosha. Kama Nchi ili kuondokana na kadhia hii na kutoa uhakika wa nishati ya umeme kwa wawekezaji, wafanyabiashara na wajasiriamali ni lazima kuendelea kutekeleza mpango mkakati wa uzalishaji zaidi wa umeme kwa manufaa ya miaka mingi ijayo kazi ambayo serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan wanaendelea nayo.

Pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwani wakati anaingia madarakani mwaka 2021 aliupokea mradi ukiwa asilimia 33 za utekelezaji huku ukiwa umeshalipwa kiasi cha shilingi trilioni 1.45 kati ya shilingi trilioni 6.5 gharama za utekelezaji wake. Leo mradi upo asilimia 98 na mkandarasi akiwa ameshalipwa asilimia 90 ya fedha zote za mradi.

Tuendelee kuziamini hatua ambazo serikali yetu inachukua ili kuondokana na tatizo hili la umeme nchini kwetu.

Mtoto wa Mama Kizimkazi

#HakunaKilichosimama #2025TunaendeleaNaSamia
#KaziIendelee



Sent from my Infinix X678B using JamiiForums mobile app
Ama hakika tupo vizuri, tunaendelea vizuri na kwakweli tunaelekea pazuri Zaidi 🐒

Mungu Ibariki Tanzania

Mungu mbariki sana Dr.SSH Rais na kiongozi wetu wa nchi, ambae sote tunampenda sana na anaaminika sana kwa umadhubuti wake kitaifa na kimataifa Duniani 🐒
 
Back
Top Bottom